Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Peter Drury:- "You look at Marcus Rashford, he has the speed and the shooting style of Cristiano Ronaldo but the brains of Christian Benteke "

Nimecheka kweli na huyu jamaa. Rashford anaspidi ila ubongo wa Benteke..
Uyo jamaa mbna kama ameleta dharau kwa Benteke..
 
ujio wa maguire, james na bissaka kwa kuziangalia hizi mechi tatu tulizocheza wameonyesha kiwango chenye kuleta matumaini makubwa sana pia wamechangia kwa kiasi kikubwa sana kuziba baadhi ya nyufa zetu zilizokuwa zinatishia kuiangusha nyumba yetu ya matofali.

eneo linalotufanya tuonekane kwa mara nyengine tena ni underdog mbele ya wapinzani wetu ni middle third, hii ndio sehemu nyengine tuliopaswa kuifanyia uwekezaji mkubwa sana kama zinavyofanya timu nyenginezo lakini kwa bahati mbaya au kwa makusudi tumeshindwa kufanya hivyo kana kwamba klabu ya manchester united wana umasikini wa fedha.

ukiziangalia hizi mechi zetu mbili za mwisho tunamiliki mpira kuliko hata wapinzani wetu lakini tunashindwa kupata matokeo ya ushindi kwa sababu ya kukosa ubunifu kwa wachezaji wetu tunapofika eneo la adui.
wolves na crystal palace kwa viwango walivyovionyesha kwenye mechi zetu laiti kama nafasi hii wangeliipata liverpool au man city basi wangelipata alama zote sita.

ndio maana nilisema humu ndani tokea mechi za pre season ya kwamba timu yetu bado ipo ovyo, haiwezekani tunamiliki mpira kwa asilimia 60 baadae tunapiga shots on target mbili kwa dakika takribani 70 then tujisifu tumeimarika kiuchezaji, kwangu mimi kumiliki mpira pamoja na kuwa na defence ngumu ya ulinzi bila ya kuwa na safu hatari ya viungo washambuliaji ni kazi bure kwa sababu mwisho wa siku utawafanya mabeki wachoke kwa kukimbia ovyo muda wote na hatimaye kuwafanya waonekane ni vilaza.

tusipobadilika kiuchezaji tutaendelea kupoteza pointi pindi tutakapokutana na timu zinazokaba chini kama walivyotuonyesha wolves na crystal palace na bahati mbaya sana timu nyingi za kiingereza ndio mfumo wao na hazichezi mpira wa pressing kama ule waliocheza chelsea dhidi yetu (wazee wa kuachia nafasi).

hivi tokea tufanye usajili wa henrikh mkhitaryan kuna kiungo mshambuliaji mwengine tuliemsajili?
dirisha lijalo tunapswa tuwekeze eneo la viungo washambuliaji kama tunataka turudishe zama zetu za kufunga wastani wa magoli matatu kwa mechi.
 
Baada ya kuondoka kwa Bissaka sisi Chelsea bila ya huruma tukawadondoshea CP beki bora kabisa upande wa kulia ivi.. Garry Cahill..

Sasa ameenda kuwa new Bissaka pale..

We are proudly of you Captain Legendary..

Kila la kheri Chelsea


#KTBFFH
 
mkuu hata kama fred atapewa nafasi basi si ajabu kumkuta OGS anampa nafasi lingard awe namba 7 huku daniel james akitokea benchi.
teh teh teh

nemanja matic uhusiano wake na man utd ndio unaelekea mwishoni kama OGS ataendelea kuwa mwalimu.
 
Mkuu Dimaria alii prove Dunia kwamba ni world class, je alipokuja United kina nani walimfanya ashuke kiwango, Falcao, Sanchez wakishushwa na akina nani n.k

Kwa mfano hapa unasema akina Lingard ndio wanamsababisha Pogba asicheze vizuri. Nikikuuliza Lingard na nani sidhani kama utataja hata wachezaji 4 ambao utawaingiza kwenye hiyo blame game

Swali linakuja, akina Degea, Wan Bissaka, Shaw, Maquire, Lindelof, Tony Martial, Rashy, James je wote wanamuangusha Pogba? Je Pogba pale Ufaransa ana world class players tu wanaomzunguka, Pavard, Giroud, namba 3 wao yule n.k

Je pale Juve alikuwa amezungukwa na wachezaji wote world class players? Je unapotaja mafanikio ya Juve kwa wakati ule, ulikuwa unamtaja kama Pogba ndio ameibeba timu au Pogba was just another Juventus player

Pogba kucheza timu yote duniani, sidhani. Ana hiyo potential, KWELI na pengine mpaka anastaafu atabaki kuwa na POTENTIAL tu, lakini sio timu yoyote duniani anaweza kucheza. City hawezi kupata namba, na Pep alimkataa, Madrid pamoja na Luka kuwa kikongwe sidhani kama anaweza kumvua namba. Barca ndio kabisaa.

Hapa nazungumzia uwezo wake uwanjani na influence yake kwenye timu, hivi vitu ukiviunganisha kuna viungo wengi duniani wanaweza kuwa mbele ya Pogba.

I would rather have Ericksen, Madson, BF, Milinkovic than Pogba in my team
 
❌ Crystal Palace
❌ Southampton
❌ PSG
❌ Arsenal
❌ Wolves
❌ Watford
❌ Wolves
❌ Barcelona
❌ West Ham
❌ Barcelona
❌ Everton
❌ Man City
❌ Chelsea
❌ Huddersfield
❌ Cardiff
✅ Chelsea
❌ Wolves
❌ Crystal Palace

Man Utd have kept ONE clean sheet in their last 18 games 😬
 
Naona umeanza kumkubali Bissaka taratibu

Kuna siku ulimponda sana humu
Bissaka sijawai kumponda mkuu nilimwesabia mechi ..lakini ameonesha kiwango kizuri ila tatizo timu ya Man united itamtumia tu bila mafanikio yeyote ..hii Man united ya sasa inaeza Ku struggle ata misimu kadhaa mpka kurudi kwenye uwezo wake tunaoujua. Hii timu itakuwa inapanda na kushuka hivi hivi hadi msimu unaisha. Hivyo Bissaka na Pogba naona kwa mtizamo wangu watafute timu za kwenda tu kama wanataka mafanikio ya makombe ..ila kama ni pesa basi wabaki wazichote tu
 
Nyie vibonde wetu, hata tukipanga under 18's,tunawagonga 4G kama kawa
Hahaha unaifunga Chelsea yenye watoto waliotoka championship msimu uliopita..jana umekutana na wazee wa kazi na ndo tutajua man united khalisi ni ipi..
 
Nakukumbusha mkuu radika kuhusu comment yako juu ya timu yetu.
 
mkuu hata kama fred atapewa nafasi basi si ajabu kumkuta OGS anampa nafasi lingard awe namba 7 huku daniel james akitokea benchi.
teh teh teh

nemanja matic uhusiano wake na man utd ndio unaelekea mwishoni kama OGS ataendelea kuwa mwalimu.
Hahahaa

Mimi kiukweli Lingard naona anaweza kutumiwa katika baadhi ya mechi kimkakati lakini si mechi zote

Lingard hana uwezo wa kumuweka DJ especially kwa nafasi za pembeni

Kinachonifurahisha, naona kama umeanza kumuelewa swala
 
Chelsea sijaona mchezaji wa kushauri aondoke maana wote ni wa level za Chelsea
 
Nikumbushe mara mwisho Liverpool kuwa na clean sheet, maana United mara ya mwisho ilikuwa ni Agost 2019
 
Mourinho anazingua Sana, aliulizwa juzi timu ambazo zinaweza chukua EPL mwaka huu jamaa akataja Manchester City, Liverpool, Tottenham na Manchester City "B" team...
Kwamba hata wachezaji waliopo benchi pale Manchester city wanaweza compete for tittle wakipewa nafac....
 
Hahahaa

Mimi kiukweli Lingard naona anaweza kutumiwa katika baadhi ya mechi kimkakati lakini si mechi zote

Lingard hana uwezo wa kumuweka DJ especially kwa nafasi za pembeni

Kinachonifurahisha, naona kama umeanza kumuelewa swala
yes, swala analeta matumaini lakini unakuta wachezaji kama wale wanaotoka timu ndogo baadae wanajikuta wanaingia first eleven kwenye timu kubwa wanachoka mapema sana au wanajisahau pindi wanapokosa upinzani.

jana alifunga goli zuri sana.
dogo anahitaji zaidi utulivu wa nafsi ndio maana sikutamani awe winga pekee aliyesajiliwa kwa kuhofia kumbebesha mzigo mzito wa majukumu haliyakuwa bado ni kijana mdogo.​
 
Utageuka tu maneno yako, Kuna siku nyingine ukasema Azpilikweta ni bora kuliko Bissaka
 
yes, alikuwa anajaribu kuonyesha jinsi gani majirani zetu walivyojaaliwa utajiri wa wachezaji wenye viwango visivyopishana sana.

baadhi ya nyakati ni bora uwe na wachezaji 18 wenye uwezo mkubwa kuliko kuwa na kundi la wachezaji 23 wenye uwezo wa kawaida.
 
Man united zamani ilikuwa ni dream ya wachezaji wengi kucheza. Ilikuwa ni heshima sana kukipiga ndani ya dimba la OT ..

Kama ilivyo Anfield ya sasa ..ndivyo ilivyokua OT, lakini kumekuwa shamba la bibi timu yeyote tu ata Yanga ikija inashinda tu
..unaona hata haina mvuto kwa wachezaji kuja kucheza apo..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…