Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Kuweka kumbukumbu sawa aliyepigwa saba na bayern alikuwa Tito Villanova.
 
Unaongelea dominance gani ?
PSG tangu imeanzishwa imechukua ubingwa (Ligue One) mara 8 tena baada ya kununuliwa na hao waarabu ,Ferguson amechukua ubingwa mara 13
PSG hawajawahi hata kucheza fainali ya Champions league ,Feguson amechukua Champions league mara 2
Ferguson kwenye career yake kama kocha ameshinda makombe mengi kuliko timu ya PSG tangu ianzishwe
 

Mourinho peke yake ndio mwenye rekod ya kutofungwa mara mbili

Huyo ni conte kamfunga pep huku na kule fikiria city ile ilivyokuwa

Narudia hamna anaemchukia pep ila mpunguze kumkweza bila pesa epl asingebeba hata chembe

Fikiria pelegrin kabeba kikombe na ile city yeye alipigania top 4


Vitu vingine mnavyoongea muwe makini sana wenzenu tunapoongea tunamaanisha
 

Mech ya wolves watu walijaa ule usiku lakin hapo ma upinzan ndo yalikuwa mengi balaa
 
Huwa napenda kujenga hoja kwa stahili hii, siyo "mimi nasema"
 

Tofauti ya PEP na SAF ni:-

SAF alidominate EPL kwa foundation ya kujenga timu imara.
PEP anataka kudominate EPL kwa foundation ya Nguvu ya pesa.

Sasa Nguvu ya pesa haiwezi kudominate kwa muda mrefu kwenye EPL kwani hilo ndiyo alilotaka kulifanya Abramovic kutaka Chelsea idominate EPL kwa Nguvu ya Hela hatimae akatesa misimu miwili kwa kununua mchezaji anayemtaka mwishowe karudi alikotoka SAF akakamata nafasi Yake.

Nahuyo Man City atarudi alikotoka kwani Hakuna mchezaji bora mwenye ndoto ya kucheza Mancity Bali hao kina Aguero na Sterling wapo kwasababu ya Pesa tu (Wages), Hata Sane anataka kukimbilia Bayern.

Man City ikianza kubalance Wages tu itarudi ilikotoka, na kama haibebi CL hata Pep mwenyewe ataikimbia arudi Barcelona kabla Messi hajastaafu.

Bila ya Foundation imara ya kuwa na Wachezaji wanaoipigania Badge basi hawezi kudominate EPL zaidi ya Miaka 3 kwa Wachezaji wanaopigania Mishahara kina Sterling.
 
Tena EPL haina utan, na anadhan mbio za ubingwa zitabak za timu mbili kama mwaka Jana,

Bingwa wa msimu huu sio city EPL. Watu wamekariri subiri ni muone kuna timu zimejipanga ila hamuzioni. Mm ni shabiki wa united mnoo bila siwezi kua kimya na mnafiki lazima niseme uweki Spurs na Arsenal wamejipanga vizuri msimu huu. Wako vizuri sana itakua ni ajabu sana wasipo challenge for a trophy msimu huu na Pep ni mzuri sana bila naamini hizi timu zikiamua kua serious na kumaintain consistency zitaleta mabadiliko makubwa mwakani may.
Hii ligi haina mwenyewe.
 
Hakuna wa kumzuia Pep
 
Kwa EPL hao Spurz wameboresha timu wasitoke nje ya Big 4 na kwa hilo hakuna ubishi wako vzr sana ila sio Ubingwa.
Arsenal amefanya usajili mzuri pia... Ila sio wa kumpa EPL labda wa kumrudisha big 4 na kuwania Carabao Cup tu kama Utd.
City timu ya kumpa EPL anayo kabisa usitishwe na droo ya Spurz mkuu, labda UEFA ndio huo upepo hana..
Liverpool ataendelea kumchalenji City, ili aupate ubingwa itabidi aongeze nguvu dirisha dogo la usajili tofauti na hapo kazi ipo.
 

Nakubaliana na ww mkuu
 

Nahisi pengine ndugu yangu MASAMILA huwa anatania mambo mengine yaani psg na juventus wanatawala soka la ulaya?
 

Mi sio mdau sana wa hili jukwaa ila huwa napita weekend kusoma opinions za wadau km nyie kuhusu timu yetu

Ila Mkuu to be honest nashindwa kujua kwanini unam underate pep kiasi hiki

Tukubali tukatae pep is the current best coach in the world for almost 10 years after the retire of sir Alex

Tunaweza tukatumia sababu kwamba Pep ana spend sana sokoni Ndio maana anapata mafanikio
Lakini ni timu gani kubwa ulaya isiyospend pesa? Zote zinaspend pesa kubwa kama kuna tofauti sio kubwa sana

Pep ni kocha bora Tukubali hata kama anafundisha hasimu wetu katika Epl na kila shabiki wa Manchester United alipenda kuwa na kocha kama huyu

Ubora wa pep huwa unaanzia pale kwenye usajili huwezi kumuona pep anahangaika na Wachezaji ambao tayari kila timu Inatamani kuwa naye
Yeye anachikua mchezaji ambaye anakuja kumpika yeye jinsi ya kucheza mpira tofauti na makocha wengine

Football is fact...
Tumpe heshima yake Pep kwanza amekuja kuamsha na kuleta hamasa kwenye ligi kwa mid table teams jinsi ya kupambana ilikuwa ni rahisi kwa bingwa wa Epl kutangaza ubingwa kwa point 78-86 Lakini ndani ya misimu miwili kabadilisha iyo

Wengine watasema mbona ana muda mrefu hajachukua UEFA kiukweli ni kuwa uefa is about lack and DNA ya timu hata sir Alex ilikuwa inamchukua miaka kumi ndio ananyanyua ndoo ya uefa

To me Pep is the second best coach after sir Alex kama kuna utaratibu wa malkia kutoa Sir kwa watu wasio raia wa Uingereza ampe tu na pep naamini atafanya makubwa kabla ya kuondoka kwa the citizens

Na akiondoka Epl kwenda Juventus ligi itapoza kiaina Kwasababu nasikia ana pre aggrements na bibi kizee cha turin

Ni Hayo tu mkuu
 
Issue ya usajili man City tumeshaizungumzia Sana Humu Ni Mambo ya Kina Txiki Begiristain ambaye alikuwa anasajili wachezaji wanaofit mfumo wa tiki taka toka hata pep hajakuja. Man city wameanza ku poach viongozi wa Barcelona hata kabla ya pep.

Mbona Bayern pep alipokuwa Hana Dof wa Tikitaka usajili wake ilikuwa Ni wa kawaida tu? Majina makubwa mengi na wengine hata hawakufit mfano Mario Gotze, pep Reina, Mehdi Benatia, Arturo Vidal Etc, wote walikuwa tayari Ni established super stars wanatakiwa na timu nyingi akawasajili yeye na wakaflop.

Na wewe nakuuliza swali Kama nilimuuliza mwenzako juu kitu gani kafanya pep ambacho kocha mwengine yoyote ameshindwa kufanya?
 
Nimeishia kusoma uliposema Pep anakuza vipaji
 
26/13 maana yake Fergie alikuwa akichukua kombe kila baada ya msimu ukiweka average.

Hii kama siyo dominance ni nini ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…