mkuu kama ni hivyo basi hakuna faida ya klabu kufanya usajili wa wachezaji kama ishu ni kuhofia young players kutoka academy hawatopata game time ya kutosha, hata huyo maguire kwa mujibu wa hoja yako ujio wake utasababisha tuanzebe na vijana wengineo kutoka academy watumie muda mwingi kukaa benchi au kucheza mechi za under 23.
nilichokuwa nakihitaji mimi ni kuona kwanza tunaziba madhaifu yetu kwa kufanya usajili wa sehemu zote zenye ufa baadae ndio tuwape nafasi vijana ila alichokifanya OGS msimu huu ni kuwabebesha mzigo wa misumari vijana wadogo wasiokuwa na uzoefu wa mapambano kwa kuwategemea wawe wazibaji wakubwa wa nyufa zetu.
nitatoa mfano mwengine wa manchester city tumeona timu yao jinsi ilivyoimarika kila eneo kiasi ambacho hata ikitokezea david silva amewekwa benchi nafasi yake inazibwa vizuri na kijana phil Foden kutoka academy.
kwa nini phil foden anacheza vizuri?
jibu ni rahisi tu ni kwamba pindi akiwa uwanjani hujikuta amezungukwa na mafundi wa mpira kila pembe jambo ambalo humpunguzia presha ya kuwa tegemeo kwenye mechi husika.
lakini ukija kwetu sisi unapomuanzisha angel gomez au greenwood kwenye kikosi kinachoundwa na dead players mfano wa ashley young, fred,jones, perreira, matic na wengineo wanajikuta wanabeba mzigo mkubwa sana wa matumaini ya kuwa wabebaji wakubwa wa timu kimatokeo.
nikatoa mfano wa barcelona nyakati ambazo kwa muda tofauti wanawakuza kisoka sergio bosquets, messi, gerrard pique,pedro, sergio roberto, thiago alcantara, cristian tello, bojan krkik na wengineo hawakuwabebesha majukumu sana kwa sababu walikuwepo wachezaji watakaowafanya ile presha ya kuibeba timu isiwepo kwenye mabega yao.
yupo henry, etoo, gaucho, deco,guily, abidal, toure, puyol, marquiz,xavi, iniesta, david villa, zambrotta, dani alves,alba na wengineo kwa nini usiufarihie mpira wako?
kama ni young players kwa nini usiufurahie mpira wako kwenye timu inayozungukwa na kevin debruyne, gundogan,aguero, sane, sterling, silva double, concelo, mendy,otamendi, walker, aguero?
kama ni young player kwa nini usiufurahie mpira wako kwenye timu inayoundwa na roy keane, rooney, scholes, giggs, ferdinad, vidic, evra, nistelrooy na wengineo?