Unless huelewi hizo hela wanazipataje mkuu mashabiki Wana haki ya kulalamikia.
Unaenda kwenye Banda la Mpira unatoa 500 ama 1000 unaangalia Mpira, mwenye Banda anajichanga mwisho wa mwezi analipa DSTV. Mwenye uwezo anakua na DSTV nyumbani na mwisho wa Mwezi analipa DSTV.
Mkataba wa mwisho Supersport wameilipa ligi Uingereza ya Uingereza pound milioni 296 (almost 300M hio) kuonyesha EPL, hio ni kusini mwa jangwa la Sahara Tu, kaskazini Nchi za kiarabu na Nigeria Wana licence zao wenyewe. Hivyo unakuta Africa tu tunachangia Hata 500M kwenye ligi ya Uingereza kwa kila mkataba.
Hizo Hela zinakuja zinagawanywa kwenye timu, Msimu wa juzi man U walipata 36M Kama sijakosea Toka Nchi zetu za mbali.
Hivyo ndio Mtanzania wa kawaida anavyozichangia Timu za Uingereza.
Bado Kuna watanzania wengine wananunua magari ya Chevrolet, wananunua jezi za Adidas, na Commerical nyengine ambazo zinaingiza Hela kwa man U pia.
Sisi mashabiki ndio tunaingizia club hela hivyo Wana haki ya kusikiliza na kuwafurahisha mashabiki.