Manchester United (Red Devils) | Special Thread

£75 ml ..........Harry Maguire inaweza kana jamaa ni the same level na Van Djik......MANCHESTER UNITED wakeup hahahahahahahahah wazee wa kupigwa.
Man UTD Hata asajili jiwe ama kibakuli kinaingiza hela zaidi ya iliotumika kusajili, kwenye financial point of view Woodward yupo vizuri Sana, anajua afanye nini timu ipate faida ndio maana Kila mwaka timu inavunja rekodi za mapato japo uwanjani haipo vizuri.

Hayo ya kupigwa mnatakiwa mu discuss nyie.
 
sisi ndiyo mashabiki wa Manchester kama hatutasajili beki tutalialia hapa tukisajili tutalialia pia, tukisajili cheap options bado tutalialia hata tukisajili kwa mihela mingi tutaendelea na vilio

hatujui tunachotaka pathetic
 
sisi ndiyo mashabiki wa Manchester kama hatutasajili beki tutalialia hapa tukisajili tutalialia pia, tukisajili cheap options bado tutalialia hata tukisajili kwa mihela mingi tutaendelea na vilio

hatujui tunachotaka pathetic
Sisi muda mwingine tunazingua sana..

Maguire kwa hiyo hela watu hawamtaki na tukileta option nyingine labda ya Alderwield kwa bei chee bado tutapinga tena..

What do we actually need??
 
sisi ndiyo mashabiki wa Manchester kama hatutasajili beki tutalialia hapa tukisajili tutalialia pia, tukisajili cheap options bado tutalialia hata tukisajili kwa mihela mingi tutaendelea na vilio

hatujui tunachotaka pathetic
Ed Woodward ndio amesababisha hata hamjui tatizo la Manchester United ni nini,situation haikuwa hivi 8/10 years ago
 
Mkuu sidhani Kama lazima awe muingereza tupo linked na Bruno, Ben Yedder, diop etc timu Sasa hivi inataka tu wachezaji wadogo wenye potentials kubwa ambao watakaa pamoja kwa muda mrefu wakue pamoja.

Kwa hiyo mmeamua kufuata playbook ya projects za Poch na Klopp?
The question is: Mna patience ya rebuilding process ambayo normally takes 3-5 years hadi muwe true contenders?
Ama mtaamua kufuata Projects za Mourinho na Guardiola ambazo ni kumwaga mapesa ili kupata instant success in 1-2 years?
 
Ed Woodward ndio amesababisha hata hamjui tatizo la Manchester United ni nini,situation haikuwa hivi 8/10 years ago
kwa ninavyoiona hii timu hata ED akiondoka bado tatizo litakuwepo.
 
Wakala wa Maguire huenda akawa ni mwanafunzi wa Raiola.
Yani Beki wa kawaida ambaye hata husikii kung'ang'aniwa na timu kubwa kama ilivyokuwa kwa De Ligt lakini still anamuongeza thamani kila Siku.
 
Hio ni Manchester way, haijaanza kwa poch na klopp ipo miaka na miaka kuanzia kwa Busby Hadi Fergie. Na Fergie mwenyewe pia ashaifanya zaidi ya mara 1, miaka ya around 2003 timu ilipokuwa haifanyi vizuri alianza upya Tena wakasajiliwa Rooney, Ronaldo, kleberson, Anderson, Djemba Djemba, Nani, kilichotokea unafahamu.

OLE anacopy tu falsafa za Man U.
 

Kwa hiyo unatuaminisha kabisa kuwa Ole white maasai ana uwezo was sir Fergie tena kwa mtaji wa wachezaji mediocre waliopo kwa sasa?
 
Habari njema hizi mizigo iondoke

Madrid sijui wamewapendea nini
 
Sisi mashabiki tunataka mabadiliko uwanjani.

Hayo ya faida tuwaachie wamiliki.
 
kwa ninavyoiona hii timu hata ED akiondoka bado tatizo litakuwepo.
Tatizo litatuliwa kwa install mfumo unaotakiwa kuendesha soka kisasa.

Ed anazuia mabadiliko muhimu.

Tungekuwa na DoF mwenye mamlaka kamili, na hela inatolewa kwa target sahihi, tungeona mabadiliko.

Ed amezuia hayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…