Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Umeeleza vema ndugu!
 
Chief-Mkwawa ukipata muda naomba uniondolee mavumbi yaliobaki kwenye ubongo wangu kuhusiana na hii sheria ya financial fair play kuna mambo bado sijayafahamu kiundani

barcelona wamemuuza golikipa cillesen kwa euro millioni 35 siku chache zilizopita kuelekea valencia.
barcelona wamemsajili golikipa neto kutoka valencia kwa euro millioni 26 na ongezeko la euro millioni 9.

ukiziangalia hizi gharama walizozitumia kwa malipo zinafanana, kwa nini hawakufanya swap deal?

nimesoma taarifa kupitia vyanzo tofauti klabu ya valencia wanahitaji takribani euro millioni 30 kwa ajili ya kufunga vitabu vya matumizi kwa mwaka huu unaoelekea kuisha ili wasipate hasara, ina maana mkataba wa cillesen kwa elimu yangu dhaifu utafungwa July 1 ambapo ndio mwanzo wa mwaka mpya wa soka barani ulaya ili valencia waepukane na rungu la FFF.
 

Mkuu nimesoma online hapa Barcelona watawalipa Valencia 30 mwezi huu na Valencia watazirudisha hizo hela tarehe 1 july. Hivyo Barca wanawasaidia wasifungiwe.
 
Mimi sitamlaumu wakija watatu, CB, right wing na midfield. Timu yetu itakuwa imekamilika.
 
Mimi sitamlaumu wakija watatu, CB, right wing na midfield. Timu yetu itakuwa imekamilika.
right wing tumeshamsajili danny james na ndio maana tetesi za kutafuta winga mwengine hazipo.
midfield ningependa kumuona bruno fernandez anasajiliwa lakini tatizo dau lake kubwa kwa bwana ed woodward hivyo basi si ajabu klabu kumgeukia mtoto wa kiingereza anayeitwa sean longstaff
 
James ni wa kushoto japo anacheza kulia pia. Ingesajiliwa source ya magoli kulia ingekuwa vizuri zaidi.

Hata mimi nahitaji Bruno aje zaidi. Longstaff sidhani kama ni upgrade ya Mctominay, atakuja tu kumzibia mwenzake.
 
Sisi na nyie hatuchekani, Atleast Spurs Ama Arsenal Kidogo wanaweza wakajisifu. maana mna Rundo la maflop kina Ings, Caroll, lambert, Balotteli, benteke, Grujic, karius etc
mkuu lakini wao hiyo hatua kwa kiasi kikubwa wameshaipita lakini kwetu sisi bado tunaendelea nayo.
maisha yote anayeshinda vita ndiye mwenye haki ya kuandika historia haijalishi ni uongo.
nimemkumbuka david ngog, lazar markovic pamoja na alberto aquilani
teh teh
 
Yah kiasi fulani, ila kina karius na Keita sio wa zamani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…