Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

juzi kati tulisikia uongozi wa timu yetu ulimpa De Gea wiki moja ili asaini mkataba mpya ama wampige bei....lakini mpaka leo kimya sijui imeishia wapi ile!
Ed alimpa huo muda mana kias anachotaka de gea hawataki kukitoa....psg wanamtaka sana na wanampa kama 430 kwa wiki kama akienda.
Tuzid subr official statement yao
 
Anaongea sana **** huyu
Ed Woodward: "Preparations for the new season are underway and the underlying strength of our business will allow us to support the manager and his team as we look to the future."
Yan haya maneno inaonyesha ni jins gani anawaza biashara zaid kuliko performance ya team. Business? What the hell? Haya maneno anaongea kila mwaka ila nothing new
 
Juninho Pernambucano "mzee wa dead balls" ameteuliwa kuwa technical director wa klabu ya Lyon

United???
“The mission is accomplished”
B
wana ed woodward kwa takribani miezi sita alikuwa anatuchezea anavyotaka na ameshafanikiwa.
nilishawahi kuandika humu ndani siku za nyuma ya kwamba ed woodward hana nia ya dhati ya kutafuta mwanadamu atakayemuingilia kimawazo kwenye mission zake za usajili kwa msimu huu.

kwenye dirisha hili la usajili hata kama leo hii klabu itamchagua michael zorc wa dortmund awe DOF basi hatokuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa ufasaha zaidi kwa sasa, ina maana stering atabaki kuwa comando ed woodward a.ka.a usiyempenda ndiye aliyependeza harusini.

acha tuendelee kuchezea tetesi mpaka tunyooke then ndio tutaletewa wachezaji wawili kila baada ya mwezi, baadae atachukua likizo ya kwenda Australia kimapumziko utadhani amemuua simba mnyama.
hivi darren fletcher atakabidhiwa madaraka lini?

hizi tetesi za Moussa Dembele wa lyon sizielewi jamani, nadhani tunaukumbuka moto wa lacazzete pale lyon lakini alipokuja england alikuwa ni zaidi ya mwehu.
wajuzi wa soka naomba munisaidie juu ya uwezo wa huyu jamaa.

tutafanya makosa makubwa sana endapo tutamuondoa romelu lukaku then tukamsajili huyu jamaa ashirikiane na mjinga rashford.
tutafanya la maana sana endapo tutamsajili huyu jamaa huku tukiendelea kumbakisha romelu lukaku.

bila ya kusahau mpaka muda huu bayern munich wameshatumia takribani paundi millioni 100 kwa ajili ya wachezaji wawili tu.
1101762

1101763
 
Sitasahau zile tetesi za kumsajili mahrez mwisho wa siku huyoo city kaenda wapa ubingwa
 
Kwa hizi tetesi na sajili za united siioni timu kuinuka ... Huu ni ukweli mchungu...


Mimi ni mshabiki lialia wa ligi ya German, Spain na Italy.


Kuna wachezaji ninawafahamu (Average) players kutoka kwenye hizo ligi sioni hata wakihusishwa ... Unabaki kusikia wakina James Rodriguez etc .

Anyway Ngoja tuone ila kama kinachoendelea kwenye tetesi ndicho kitafanyika tusitarajie lolote next season .
 
Kwa hizi tetesi na sajili za united siioni timu kuinuka ... Huu ni ukweli mchungu...


Mimi ni mshabiki lialia wa ligi ya German, Spain na Italy.


Kuna wachezaji ninawafahamu (Average) players kutoka kwenye hizo ligi sioni hata wakihusishwa ... Unabaki kusikia wakina James Rodriguez etc .

Anyway Ngoja tuone ila kama kinachoendelea kwenye tetesi ndicho kitafanyika tusitarajie lolote next season .
Hizo tetesi za kwenye magazeti zingine za kutengeneza tu hazina ukweli wowote.
 
Hizo tetesi za kwenye magazeti zingine za kutengeneza tu hazina ukweli wowote.
Mwisho wa siku wachezaji wa kwenye tetesi ndio miongoni mwao husajiliwa... Hakuna mchezaji anaesajiliwa bila tetesi .. Yaani ukichukua tetesi 20 za usajili lazima atasajiliwa mchezaji hata mmoja .. Vyombo vya habari vya wenzetu vinajua maana ya "Kazi'

Sasa ukiangalia tetesi ni utumbo mtupu...
 
“The mission is accomplished”
B
wana ed woodward kwa takribani miezi sita alikuwa anatuchezea anavyotaka na ameshafanikiwa.
nilishawahi kuandika humu ndani siku za nyuma ya kwamba ed woodward hana nia ya dhati ya kutafuta mwanadamu atakayemuingilia kimawazo kwenye mission zake za usajili kwa msimu huu.

kwenye dirisha hili la usajili hata kama leo hii klabu itamchagua michael zorc wa dortmund awe DOF basi hatokuwa na uwezo wa kufanya kazi kwa ufasaha zaidi kwa sasa, ina maana stering atabaki kuwa comando ed woodward a.ka.a usiyempenda ndiye aliyependeza harusini.

acha tuendelee kuchezea tetesi mpaka tunyooke then ndio tutaletewa wachezaji wawili kila baada ya mwezi, baadae atachukua likizo ya kwenda Australia kimapumziko utadhani amemuua simba mnyama.
hivi darren fletcher atakabidhiwa madaraka lini?

hizi tetesi za Moussa Dembele wa lyon sizielewi jamani, nadhani tunaukumbuka moto wa lacazzete pale lyon lakini alipokuja england alikuwa ni zaidi ya mwehu.
wajuzi wa soka naomba munisaidie juu ya uwezo wa huyu jamaa.

tutafanya makosa makubwa sana endapo tutamuondoa romelu lukaku then tukamsajili huyu jamaa ashirikiane na mjinga rashford.
tutafanya la maana sana endapo tutamsajili huyu jamaa huku tukiendelea kumbakisha romelu lukaku.

bila ya kusahau mpaka muda huu bayern munich wameshatumia takribani paundi millioni 100 kwa ajili ya wachezaji wawili tu.
Bayern si wamemchukua na Pavard bure, full back wa timu ya taifa ya Ufaransa

Sisi bado tupo kwenye tetesi, wakati sisi ndio tupo kwenye desperate situation kuliko wao
 
Bayern si wamemchukua na Pavard bure, full back wa timu ya taifa ya Ufaransa

Sisi bado tupo kwenye tetesi, wakati sisi ndio tupo kwenye desperate situation kuliko wao
yes wamelipa paundi millioni 30 kwa usajili wa benjamin parvard.
tetesi zetu zimejaa vituko kama anavyosema Daud1990
tetesi za kumhitaji bruno fernandez zimeshazikwa
 
Kuielewa klabu ya Manchester united kwa sasa ni ngumu sana. Tulikuwa juu lakini unaona juhudi za makusudi kabisa kuturudisha chini. Tunasajili kama blackburn rovers,tunacheza kama aston villa lakini CEO anapiga porojo kama manara tu.

Natumaini zile kelele za 'treble' za citizens zitawafanya wenzetu wapate njia mbadala ya ku deal na Ed
 
Antonio ni Dreams come True,alikuwa anaipenda Man United sana,Inasemekana kipindi anapata taarifa ya kutakiwa na SAF (Sir Alex Ferguson) alisitisha Matibabu na kuondoka katika kambi ya Wigani.

Antonio namfananisha na Wimbo wa Daz baba ft Ngwair (R.I.P) -WIFE.

Daz baba Moja ya mashairi yake
"Long-time Namzia huyu sholi/

Ila sjawahi naye hata kupiga story/

Ila niliamini yeye ndiye atakaye nifaa/
Siku moja moja nimekaa maskini nashangaa/

Kupokea yake barua yeye anadai Mimi ndio namchengua/

Hata jibu sikujua nikamwambia mama moyo wangu wote chukua"

Antonio hakuamini kilichotokea kutua Old Trafford.
Hahahaha kuhusu lugha umenikumbusha kuhusu Tevez, alishindwa kabisa kujifunza lugha ya Malikia

Antonio huko nyuma akiwa Wigan na wakati anahamia United, niliijua hiyo story ya kushindwa kui master lugha ya kiingereza, lakini alivyokaa United na baadaye akakabidhiwa kitambaa cha unahodha sijui kama tatizo la lugha liliendelea (logic yangu, ni mchezaji anapewaje ukapteni kama hana uwezo/anawasiliana kwa tabu na wachezaji wenzake?)

Valencia aliwahi kusema alivyokuwa anacheza huko kwao Ecuador, kuna siku alikuwa home na Familia ya kwao wanaangaalia mechi moja pale Nou Camp, akawaambia ipo siku nitacheza hapo, basi Familia yake wakiwemo wazazi wake wakamcheka sana. Anakwambia miaka kadhaa mbele (alivyokuwa United, akaichezea United dhidi ya Barca pale Nou Camp). Hii story ilinifundisha jambo kubwa sana kwenye maisha yangu

Antonio ni fighter sana, lakini umri umemtupa mkono. Ngoja tusubiri mbadala wake kwenye usajili dirishi hili.
Kuhusu lugha ya Malikia mpaka nyakati hizi Antonio bado si mzuri sana ukilinganisha na Juan Mata na Herrera waliomukuta England.

Kuhusu Ucaptain wa Antonio na lugha ya mawasiliano kama kiongozi,

Kwa mabadiliko ya kisoka Nyakati hizi Ucaptain kama umeshushwa vigezo hapa ndiposa tunapata kuwaona akina Messi/Ronaldo ambao kwangu mimi sioni sifa kutoka kwao katika uongozi katika Timu,

UCaptain imekuwa kama aidha ukongwe wa Mchezaji ndani ya klabu Au Umaarufu/Nembo ya klabu/Bembelezo la Mchezaji kubaki ndani ya klabu kwa hiyo kwa namna hiyo mchezaji anaweza kupewa UCaptain hata kama anauwezo mdogo sana(Ububu pia) wa vigezo vya Ucaptain....Tofauti na captain ni Mtu muhamasishaji,Mwenye kukemea uzembe,kuunganisha Timu na kuongoza timu katika nyakati zote(Mfano great Captains ,Patrick Viera,Roy Keane).

Carlos Tevez hahaha Jamaa alikuwa fighter kuna jamaa yangu mmoja alikuwa anamkubali sana alivyoondoka Old Trafford Jamaa aliumia sana na kuwekwa benchi UEFA champions final 2009 Barc vs Man United. Huyu jamaa naye hakujisumbua na lugha ya Malikia mpaka anondoka Epl inasemekana hafahamu lugha.


Ramires Mdigo wa Brazil aliyekuwa akipendwa Chelsea huyu pia pamoja na kukaaa muda London haifahamu lugha.

Saizi Kun Aguero inasemekana lugha ndio haipandi kabisa,kipindi cha nyuma mchezaji mwenzake Zabaleta ndiye alikuwa mkalimani wake.

SIR ALEX aliwahi kusema lugha ni moja ya changamoto kubwa sana haswa kwa Wachezaji wa kigeni.

Klopp huwa anawisisitiza wachezaji wake watie bidii kujifunza lugha ya Malikia ili irahisishe kazi ya ukufunzi,

Watu wa Lugha ya Malikia wanapata fursa kwa kufunza lugha wachezaji wenye nia na uhitaji.
 
Back
Top Bottom