Ole kwangu mm sio kocha bora na nadhani timu yetu itamshinda kama haiijamshinda bado.
Ole hana plan uwanjani hajui timu inacheza vipi watu wanacheza tu uwanjani ovyoovyo kama vile hawajawai kucheza pamoja. Hana tactic yoyote uwanjani jamaa anaonekana kabisa hana experience yoyote. Klop anatumia high press..na fast buildup kwenye kushambulia..pep anatumia constant pressure kwenye kukaba na high possiesion kwenye attack..nk nk nk. Ukija kwa kocha wetu ole haijulikani anacheza mfumo upi yupoyupo tu anategemea miujiza na vibe la wachezaji kushinda.
Pili jamaa yuko poor sana kuselect wachezaji wa kuanza mechi na nadhani ana ubaguzi flani kweye kuselect first eleven kuna kipind unaona kabisa lingard anazingua lakini kila siku utamuona ndani anacheza kila saa anamweka nje mtu kama lukaku amabae anainekana kabisa anapambana anapanga watu wasiojituma kina rashford(yaan huyu dogo kocha hawez kumkanya kabisa..dogo anajiona ronaldo sijui ni mchoyo balaa anataka kupiga kila saa anakaa na mpira mpaka anapoteza analalamika mno uwanajani kuna mda mpaka anazira mpira aisipopewa faulu. Kocha mzuri angeshamnyoosha dogo toka kitambo) kila siku tunaona tabia ni ileile haibadiliki ata
Tatu jamaa anazingua kwenye kuongeza mikataba ya wachezaji. Yaaani ni uingereza tu umemjaa waingereza wabovu wanapewa mikataba mizuri na kuongezewa mpunga na bado wapambanaji wakina herera wanaachwa kusepa kisa kuongezewa pesa tu kidogo.
Yaan anaonesha ubaguz wa wazi kabisa unamuongezea mshahara martial asiejituma herera akiomba kumuongezea pesa unagoma??? Daah
Nne jamaa kwenye sub ni mbovu sana yaan unaona timu inazingua toka mda tu yeye katulia tu anasubir sijui mpak dakika ya 70 au mpaka mpigwe goli ndo anajifanya kushtuka na kufanya sub zake mbovu fasta. Unakuta lukaku ndo kacheza vizuri anamtoa anamwacha rashford aliekuwa anacheza fyongo. Rashford kacheza fyongo sana na jamaa alikuwa hamtoi hata iweje naona juzi ndo kaanza kumpiga sub dogo
Mwisho jamaa anaonekana kabisa sio mkali kwa wachwzaji na kuna wwachezaji anawaogopa mfano pogba..jamaa anawez zingua mechi anapoteza pasi hakab nk ila atampiga sub fred anaecheza vizuri. Huu upendeleo wa wazi ndio unaopunguza morali ya timu.Tatizo la kuchukua nakocha wadogo ndio hili kocha hawez kumwambia chochote star wa timu unadhani ole anaweza kumkaripia pogba au martial wakabe?? Ndio maana timu letu linacheza kivivu tu
Hao kina mourinho pep na fergie ni wakali ndio maaana wanamafanikio na timu zao huyu kocha wetu mselamsela sidhan kama ataweza irudisha timu kuwa bingwa tena.