ukipitia comment zangu za zamani naamini utajifunza msimamo wangu juu ya jose mourinho, mimi naomba tumuache jose apumzike na familia yake muda huu, tunafanya makosa makubwa kumbebesha mzigo wa lawama special one kwa haya matokeo tunayoyapata kipindi hiki.
Alaf wachezaj kama Wilfred Bonny na Mangala hawakuwah kusajiliwa na Pep na ndo mana aliwapiga fagio wachezaj wabovu ambao walisajiliwa hovyo na meneja aliyepita.
maneno niliyoyaweka bold umerudi pale pale kwenye mjadala wetu wa mara kwa mara humu ndani, tofauti kubwa iliopo kati ya guardiola na makocha wanaofundisha timu yetu ni uhuru waliopewa wa kufanya mabadiliko chanya ya kimfumo na kiuchezaji.
hili limeshazungumzwa zaidi ya mara 100 humu ndani.
| Oleksandr Zinchenko | Claudio Bravo | Nolito | İlkay Gündoğan | Gabriel Jesus | Danilo | Ederson | Bernardo Silva |
| Kyle Walker | Benjamin Mendy | Aymeric Laporte | Riyad Mahrez | Douglas Luiz | marlos moreno | | |
wakati guardiola anapewa uhuru wa kusajili wachezaji hao niliowawaka kwenye table na wengineo wanaochezea reserve team ukija upande wetu hali ni tofauti.
| wilfred bony | dzeko | zabaleta, | clichy | sagna | joe hart, | samir nasri | demichelis | fernando, | yaya toure | kelechi iheanaco | jesus navas, | steven jovetic |
hawa wote amewaondoa kwa misimu miwili tu, ukija kwetu wachezaji wenye viwango vya zabaleta na wapumbavu wengineo wamejaa tele lakini wanapewa mikataba mipya.
wachezaji wanaozidi kiuwezo na edin dzeko wamejaa tele klabuni lakini ndio hao leo hii wanataka kupewa kandarasi ya paundi laki 3 kwa wiki.
guardiola alirithi squad iliohitaji mabadiliko madogo sana ukilinganisha na timu yetu na ushahidi wa hilo fuatilia ubora wa timu mbili hizi mnamo mwaka 2015/2016