Huu ubishi wa nani ni nani hata siuelewi
Kiufupi wanaosema Jose sio kocha, wanakosea na tena wanakosea sana. Kusema Jose sio kocha, ni kumtukana SAF, Pep, Wenger, Ancelot & co. maana wakati Jose anabeba 20+ trophies nao walikuwa wanapambana naye. Ina maana walishindwa na mtu ambaye sio kocha.
Kusema kwamba Jose ni kocha wa kizamani pia ni kosa kubwa. Kocha wa kizamani gani ambaye amechukua Europa 2016/2017 na Carling Cup? Embu nikumbusheni makocha wa kisasa Klop, Sari, Ancelot, Emery wamechukua kombe mara ya mwisho lini?
Jose ana uwezo mkubwa, lakini ni kocha wa misimu 2, ame prove hivyo sio akiwa United tu. Tatizo kubwa linalomsumbua José ni namna ya ku handle watu wake, MAN MANAGEMENT.
PIA
Kusema Ole hana uwezo ni kumkosea heshima huyu jamaa. Wakati anakabidhiwa Molde huko Norway ilikuwa haijawahi kuchukua kombe la ligi kuu, yeye ameawapatia makombe 2. Sasa ameiacha ikiwa nafasi ya 2 au 3 kama sijasahau.
Cardiff kwa OGS was a failure. Tatizo alitaka acheze mpira ambao kwa mujibu wa wachezaji alionao (kiwango chao) ilikuwa ni kama kutumia vitani mbinu za wenye bunduki wakati una mishale. Vita ya namna hiyo lazima ushindwe vibaya. Alikiri kwamba alifanya makosa.
Kuhusu kuanguka/kufeli, SAF mwenyewe miaka ya mwanzoni akiwa United aliboronga sana. Ukweli ni kwamba kila mtu anafeli duniani, ila tunatofautiana reaction yetu baada ya kufeli.
Ukiacha rejea ya miaka ya nyuma, Ole ameonesha uwezo tangu aingie United, mechi 12 kashinda 10, 1 ka draw na 1 kapigwa si jambo dogo. Hivyo ameonesha uwezo.
Mwisho, Ole hajateuliwa kuwa kocha wa United, bado ni option tu. Option nyingine kuna akina Pochetino n.k
Na kutumia matokeo ya PSG dhidi ya United kama kigezo cha kumpima OGS ni kiburi cha Mashabiki wa United ambao wanaamini wana wachezaji bora kama wa PSG. Itatuchukua si chini ya 400+ million pound kufika kikosi cha PSG cha sasa.
Mei ndio utakuwa muda mzuri ku judge Ole kama anafaa kuwa kocha wa United au laa. So far anafanya kazi nzuri sana.
Sent using
Jamii Forums mobile app