"HATA MAJIVU YA MWILI WA BILL SHANKLY YALIKUSANYIKA TENA"
Usiku mmoja wa saa 00.30 Usiku wa tarehe 29.09.1981 kwenye hospitali ya Broadgreen iliyopo Jiji la Liverpool ilitoka taarifa Baba wa klabu ya Liverpool FC amefariki dunia.
Siyo mwingine ni Bill Shankly.. Liverpool ni Bill Shankly na Shankly ni Liverpool FC. Ndani ya miaka 15 aliyofanya kazi Kama mkufunzi mkuu wa timu ya Liverpool FC aliitengenezea misingi migumu na imara ambayo hata sasaivi bado inaishi.
Ndani ya uwanja wa Anfield hairuhusiwi mechi yeyote kuanza mpaka walevi wao watakapomaliza sala yao takatifu ya wimbo wa "U Will Never Walk Alone ",Ndani ya Anflied Kuna jukwaa maalumu linaitwa "The Kop End" ambalo linanuka marashi ya majivu ya mwili wa marehemu Bill Shankly.
Yapo mengi Achana na uwepo wa kibao cha "THIS IS ANFIELD, Achana na uwepo wa kiwanja cha MELWOOD ambacho Shankly mwenyewe alikuwa anaamini hapo ndipo mahali maalumu kwa ajili ya "Askofu" mkuu kuandalia muongozo wa ibada.
Kwanini hata majivu ya Bill Shankly yalikusanyika tena?
Jibu ni Kiwango kitakatifu kilichooneshwa na Liverpool FC siku ya jumapili ya tarehe 16.12.2018 kwenye ardhi takatifu ya Anfield.
Niliingalia jinsi timu ya Manchester united ilivyonyanyasika chini ya mikono ya mjerumani Jurgen Klopp ,nikaangalia kwenye jukwaa flani la V.I.P nikaiona sura ya Sir Alex Ferguson imekuwa nyekundu huku akitingisha kichwa kwa ishara ya kusikitika .
Nikasafiri mpaka kwenye jukwaa wanaokaa watu maalumu waliokulia Liverpool FC na kukutana na sura ya Sir King Kenny Daglish Nikaona jinsi anavyotabasamu kwa furaha baada ya mechi kuisha.
Hiyo Ndiyo Liverpool FC ambayo marehemu Bill Shankly aliijenga na kuagiza siku akifa mwili wake uchomwe moto na majivu yake kusambazwa kwenye jukwaa la The Kop End, hiyo Ndiyo Liverpool ambayo Steven Gerrard ameagiza siku akifa mwili wake usipelekwe mortuary bali ukawekwe katikati ya kiwanja cha Anfield.
Siku zote kwenye maisha yake fundi Bill Shankly alikuwa anaamini ni laana kubwa Sana Liverpool FC kuwa chini ya Manchester United au Evarton na Ndiyo maana akaja na usemi usemao "In Liverpool city there only two best teams and those teams are Liverpool FC and Liverpool Reserves "
Anachofanya saivi Jurgen Klopp ni kurudi kwenye misingi ya Bill Shankly ambapo alikuwa akiamini katika mambo makuu mawili ambayo ni umuhimu wa mchezaji kufahamu kwanini kavaa jezi ya Liverpool FC na mchezaji anatakiwa kufahamu Melwood ni uwanja wa vita wa wajerumani.
Yapo mengi ya kuwasimulia wadogo zangu ambao hawaijui Liverpool FC zaidi ya kuijua kwenye makundi ya Whatsap na kwenye Odds za kubet, lakini ninachoamini siku ya Jumapili majivu ya mwili wa Bill Shankly yalikusanyika kwa furaha kutokana na mateso waliyopitia Manchester United kwa dakika 90.
Ni Nadra Sana kwa Mtukutu Kama Jose Morinho kwenda kwenye "Post Match Press Conference " na kukiri mbele ya vyombo vya habari kuwa alipitia mateso makubwa Sana kwenye ardhi ya adui.. Ila jumapili Morinho alikiri kupitia mateso makubwa sana na kukiri kuwa ilikuwa ni mechi ya mbingu na ardhi.
Kwa heshima ya jumapili naamini Billy Shankly kabakiza deni moja kwa Jurgen Kloop ambalo ni kuwapa Kombe Liverpool FC.
Hiyo Ndiyo Liverpool FC ambayo watoto wasioijua Liverpool FC wakawa wanakesha mitandaoni wakipiga porojo kuwa Napoli anaenda kuwatoa Liverpool FC kwenye UEFA Champion League , hiyo ndiyo Liverpool ambayo Pep Gurdiola anasema anapenda kusoma vitabu lakini kila akiiwaza anaacha kusoma kitabu, hiyo ndiyo Liverpool ambayo mwaka 1997 kuliwekwa Jukwaa la Bill Shankly nje ya jukwaa la the Kop End kuwakumbusha wachezaji shujaa huyo.
Wanaoweza kujua vizuri kuwa majivu ya Bill Shankly yalikusanyika tena Anfield kwa furaha ni Marehemu Bob Paisley, Joe Fagan na Renben Bennett.
Hiyo Ndiyo Liverpool ambayo iliamua kutoa misa takatifu kwa Manchester United na Kunikumbusha Liverpool ya akina Phil Neal, Alan Hansen na Ian Rush.
Kilichotokea Jumapili ni Liverpool FC kuipa Manchester United PENZI la Ghetto ambalo Kanye West anampa Kim Kardashian.. Kama Hujui Penzi la ghetto tafuta video ya Kanye West na Kim Kardashian wakiwa Ikulu ya Uganda kwa Yoweri Kaguta Museven.
Ashante Jurgen Kloop kwa kusababisha majivu ya Bill William Obe Shankly kukusanyika kwa Mara nyingine ndani ya ardhi tukufu ya Anfield

Montelo 10
Kapumzike Mourinho nenda Inter Milan ukamalizie ufalme wako ulioshindwa kusimama OT, najua team pinzani hazitamani kukutana na Liverpool kwa sasa duh noma sana