Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

uchochezi
Daud1990 anakusalimia bwana radika anasema jose hana makosa.
baada ya real madrid kufungwa magoli 5 na barcelona walifanya maamuzi ya kumtimua kocha wao, nakumbuka kuna mdau mmoja aliandika humu ndani ya kwamba real madrid wamefanya maamuzi ya maana sana kumfukuza kocha wao na muda si mrefu watakuwa bora kuliko manchester united hii ya mourinho.
huwezi amini ukitoa mechi ya leo real madrid amezidiwa point 2 na barcelona, wakati wanamtimua kocha wao walikuwa na point 14 na jana wamefikisha point 29 japokuwa performance yao hairidhishi sana na hii inachangiwa zaidi na kuondoka gwiji wa mpira cristiano ronaldo, ina maana real madrid wamekusanya point 15 kwenye mechi takribani 7.

upande wetu tokea madrid wamtimue kocha wao sisi manchester united tumekusanya pointi 9 kwenye mechi 7, siku hiyo hiyo aliyofungwa real madrid magoli 5 upande wetu tunamfunga everton na kufikisha point 17 tukiwa nafasi ya 8 kwenye mechi 10.
View attachment 969945
TUNADHALILISHWA
Mkuu sijakuelewa hapo juu, unamaanisha Mimi namkubali Mou?


Kama ni hivyo umenikosea mnooooooo. Sijawahi na haitakuja either duniani au mbinguni nikamkubali kocha yoyote Mwenye mbinu za kiuchezaji kama Mou.



Mimi ni moja ya mashabiki tangu mwanzo tumekuwa na misimamo iliyo wazi kabisa kuwa Mourinho haiwezi kuipeleka hii team kule tunapopataka. Na sasa imekuwa.
 
Pogba hachezi kwa moyo mkuu, hapa Mou mnamuonea tu. Na Lukaku nae anahitaji kiungo kama Pogba na Pogba mwenyewe ndivyo kama unavyomuona
Duh we una moyo huyu co kocha hatufaiiiiiii au unataka mpka tushuke daraja
 
Mi nashukuru tu nilishajiandaa na matokeo yoyote yale so kwa yaliyotupata hata sishangai wala siumiiii
 
Kama kuna shabiki humu amefuatilia uchambuzi wa supersport baada ya game ya United na Liverpool ambao umefanywa na Giggs, Michael Owen na Robbie Fowler na bado anaendelea kumsapoti Mou, mtu huyo inabidi tumtafutie kitanda pale Milembe haraka iwezekanavyo.


Uchambuzi ule Kama kila shabiki angeuelewa Mou angekuwa anawekewa mabango.
 
Mkuu sijakuelewa hapo juu, unamaanisha Mimi namkubali Mou?


Kama ni hivyo umenikosea mnooooooo. Sijawahi na haitakuja either duniani au mbinguni nikamkubali kocha yoyote Mwenye mbinu za kiuchezaji kama Mou.



Mimi ni moja ya mashabiki tangu mwanzo tumekuwa na misimamo iliyo wazi kabisa kuwa Mourinho haiwezi kuipeleka hii team kule tunapopataka. Na sasa imekuwa.
mkuu naufahamu msimamo wako tokea miaka 3 iliopita, hahahahaaaaa umeninukuu vibaya.
hivi barua ya kuachishwa kazi yule mreno haijaandaliwa na karani wetu mpaka muda huu?
mechi 7 tunapata point 9.
aibu ya karne.
 
mkuu naufahamu msimamo wako tokea miaka 3 iliopita, hahahahaaaaa umeninukuu vibaya.
hivi barua ya kuachishwa kazi yule mreno haijaandaliwa na karani wetu mpaka muda huu?
mechi 7 tunapata point 9.
aibu ya karne.
Hahahaha barua imeshaandikwa mkuu , alieshika funguo za kabati lenye barua bado anagwaya gwaya
 
Hahahaha barua imeshaandikwa mkuu , alieshika funguo za kabati lenye barua bado anagwaya gwaya
hahahahahahahaaaaa kama ed woodward anadanganya financial statement basi atwambie, haiwezekani klabu mpaka muda huu inaendelea kufanya kazi na special one.
hivi tukichangishana kila mdau dola moja haitawezekana kumlipa mourinho hela yake ya fidia?
account ya FB ya manchester united ina wafuasi takribani millioni 60, ikiwa watachangia wadau million 40 kwa dola moja kila mtu uwezekano wa kununua mkataba wa mourinho upo.
hahahahahahahaaaaaa bila ya kusahau paul scholes peke yake atatoa dolla millioni 1.
mawazo ya mlevi yaliochanganyika na hasira.
 
Back
Top Bottom