Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mourinho: “This weekend will be the first call for Dalot. He is ready now. He had an important injury, surgery, then a second injury in the national team when he was coming up. But now he has been training for two weeks and we think he is ready now.” #mufc [MEN]
 
Mimi ndiyo maana kuna muda sioni sababu ya kumlaumu mwalimu Huyu rashford one on one hajawahi kufunga
Mkuu alimfunga city 1-0 etihad kipindi anapandishwa timu ya wakubwa akaja kumfunga chelsea ile gem anakufa 2-0 old traford

Kilichompoteza rashford kumtoa center foward kuanza maisha ya kutokea pembeni hap rashford alipotea hasa ujio wa zlatan na lukaku uliathiri mwenendo wake mzima wa ukuaji kisoka van gaal alimsimamisha 9 rashford alikuwa moto
 
Ofcourse hatoonekana kuwa yupo serious na mpira, with his way of playing unafikiri yupo serious? He is not a guy who gets into a game to win, how can you take this guy as serious? afu aje ampige POGBA kiatu??? Duh!


Mwaka alomnunua Rio Ferdinand , total spending kwenye transfer market ni 32M, alipomnunua Veron na RVN 49.6M, kamnunua rooney for 25M hakununua mwengine (Usajili dirisha kuu). Hatukuweza ku compete na our European Rivals ambao kina Madrid, tumeshindwa kupata wachezaji kutokana na hela ya kununulia ama mshahara wa mchezaji.... Uhuru wa fedha alokuwa anao Fergie sio huu alokuwa nao Mou, Mou ana uhuru mkubwa sana, nasikia na January wana mpango wa kumtengea 100M azidi kupoteza hela mana tunazo nyingi siku izi.

Halafu Kumbuka, kipindi cha Glazers Klabu ilikuwa na deni, huku Glazers akitaka kuchota mahela. SAF na Gill walikuwa wanapita shida, kwa sababu Glazers trusted in Fergie, walijua huyu mtu ata ukimpa mbao achezeshe uwanjani atachukua ubingwa kwaio hawakuona umuhimu wa kurusha hela.
Kwa sasa hivi club inahitaji major surgery tofauti na zama za SAF. Kumbuka SAF ameacha kikosi chenye wachezaji bora lakini wanaozeeka kwa mkupuo na hiyo ni moja kati ya hoja zinazotajwa sana watu wanapoamua kumkosoa SAF.

Kwa hiyo kocha anayefuata ni lazima angepewa fedha ya kutosha ili kuirudisha timu kwenye hali yake. Sasa walichokosea United ni kuajiri makocha wenye falsafa tofauti tofauti, hivyo kuonekana kama wananunua wachezaji bila mpangilio. Na hapa ndio kilio cha kumuhitaji Director of Football kinapokuja.

Nasisitiza. SAF alitumia hela kwenye usajili, lakini alikiwa na advantage ya kuwa na Class of 1992 (Hawa walikuwa kama CORE YA TIMU) hivyo kuna wakati hakutumia fedha kwenye baadhi ya positions.

Mfano Barcelona, kizazi cha Xavier, Iniesta, Messi, Bosquet, Puyol, kikiisha nao watapata tabu sana unless wawe na succession plan nzuri.
 
Wachezaji wengi vijana wamekuja kipindi kibaya mno timu inataka matokeo kocha anataka matokeo tena kwa pressure mashabiki wamevurugwa hata christiano ronaldo angehangaika sana kukua kimpira kama angeanza sasa kipindi kile cha tulikuwa na majembe hata wakina ronaldo hawakuhangaika sana tulikuwa na watu wa kuficha madhaifu ya mwingine hata wasipofunga hao wakina ruud van walichukua nafasi pressure inakuwa ndogo saiv rashford anatolewa na macho balaa timu inatoka matokeo tunakazi ya kutafuta mchawi nani.
 
Nasisitiza. SAF alitumia hela kwenye usajili, lakini alikiwa na advantage ya kuwa na Class of 1992 (Hawa walikuwa kama CORE YA TIMU) hivyo kuna wakati hakutumia fedha kwenye baadhi ya positions.
Hao core, kawalea mwenyewe.... Na hii inaonesha kuwa Fergie alikuwa anafanyia kazi resources alizokuwa nazo.

Mou resources alizokuwa nazo hazitendei haki na aki source nje nazo pia hazifanyishi kazi itakiwavyo. Unaponunua Goal Keeper ushajua kama umenunua mlinda goli kwa mikono, sasa ukimueka beki 2 akatoa penalty utamlaumu?

Mou asepe tu.... Tunahitaji kocha ambae ataipa identity MUFC
 
Hao core, kawalea mwenyewe.... Na hii inaonesha kuwa Fergie alikuwa anafanyia kazi resources alizokuwa nazo.

Mou resources alizokuwa nazo hazitendei haki na aki source nje nazo pia hazifanyishi kazi itakiwavyo. Unaponunua Goal Keeper ushajua kama umenunua mlinda goli kwa mikono, sasa ukimueka beki 2 akatoa penalty utamlaumu?

Mou asepe tu.... Tunahitaji kocha ambae ataipa identity MUFC
Hahahahhh....chilubiii...unakumbuka ulivyotamba mwaka jana??...ukamwagia misifa Mou...sahivi eti aondoke!!!! Hhhhhh...unachekesha kinyama...
 
Hao core, kawalea mwenyewe.... Na hii inaonesha kuwa Fergie alikuwa anafanyia kazi resources alizokuwa nazo.

Mou resources alizokuwa nazo hazitendei haki na aki source nje nazo pia hazifanyishi kazi itakiwavyo. Unaponunua Goal Keeper ushajua kama umenunua mlinda goli kwa mikono, sasa ukimueka beki 2 akatoa penalty utamlaumu?

Mou asepe tu.... Tunahitaji kocha ambae ataipa identity MUFC
Hii ni hoja nyingine sasa, hoja niliyoongelea ni kuhusu namna SAF alivyowezeshwa kibajeti. Hoja hapa ni kwamba SAF bajeti ilikuwa far superior kuliko washindani wake wengi Ulaya na Uingereza

Ni kweli Jose ana mapungufu kwenye kuendeleza vipaji kwani yeye anataka ready made players

Lakini pia huyo Pogba asingekuwa moja ya wachezaji tulionunua kama situation yake kipindi hicho ingekuwa managed vizuri
 
Hahahahhh....chilubiii...unakumbuka ulivyotamba mwaka jana??...ukamwagia misifa Mou...sahivi eti aondoke!!!! Hhhhhh...unachekesha kinyama...
AAAAAAA unazingua ankal.... sijamwagia Misifa..... sema nilikuwa namtetea kidogo.... ila saiv hana muelekeo, ana ile 3rd Season syndrome where as club anayo manage lazima alikoroge..... Nakubali nilimtetea kabla, kwa sababu tulitakiwa tumpe muda kama SAF alivosema alipoach madaraka, lau kama ningeona positive changes hadi sasa ningemtetea ila dah!!! jahazi linazama habari hana yeye anawaza treasures zake ataondoka nazo vipi. Nampenda MOU lkn naipenda MUFC zaidi... atuache tu saiv
 
Ofcourse hatoonekana kuwa yupo serious na mpira, with his way of playing unafikiri yupo serious? He is not a guy who gets into a game to win, how can you take this guy as serious? afu aje ampige POGBA kiatu??? Duh!


Mwaka alomnunua Rio Ferdinand , total spending kwenye transfer market ni 32M, alipomnunua Veron na RVN 49.6M, kamnunua rooney for 25M hakununua mwengine (Usajili dirisha kuu). Hatukuweza ku compete na our European Rivals ambao kina Madrid, tumeshindwa kupata wachezaji kutokana na hela ya kununulia ama mshahara wa mchezaji.... Uhuru wa fedha alokuwa anao Fergie sio huu alokuwa nao Mou, Mou ana uhuru mkubwa sana, nasikia na January wana mpango wa kumtengea 100M azidi kupoteza hela mana tunazo nyingi siku izi.

Halafu Kumbuka, kipindi cha Glazers Klabu ilikuwa na deni, huku Glazers akitaka kuchota mahela. SAF na Gill walikuwa wanapita shida, kwa sababu Glazers trusted in Fergie, walijua huyu mtu ata ukimpa mbao achezeshe uwanjani atachukua ubingwa kwaio hawakuona umuhimu wa kurusha hela.
Ki uhalisia Ferguson kumpiga Beckham ni hasira za kibinadamu tu. Japo Kwa Kuwa yeye ni Ferguson basi inaangaliwa Kwa utofauti.

Tukirudi Kwenye bajeti bado napingana na wewe Kuwa Ferguson alikuwa na bajeti ndogo. By that time timu ambayo ilikuwa inaweza kushindana na sisi Kwenye usajili wa hela kubwa duniani alikuwa ni Madrid tu. Kwa maana nyingine tulikuwa tuna uwezo wa Ku spend kuliko timu zote Kwenye Epl. Na ndio maana tuliwanyanyasa ndani. Ila Chelsea na Man cty walipoanza kutumia pesa tuliamza Ku struggle.

Hebu nikupe changamoto nyingine, kama

Bei ya Maguire saizi unaambiwa ni zaidi ya 75, Ferdinand yule Kwa saizi ungempata Kwa sh ngap?

Rooney yule alisajiliwa Kwa 25 na soko la saizi Morata,Lukaku unawapata Kwa zaid ya 70. Rooney yule Kwa saizi angeuzwaje?? Maana yangu ni 25 ile ni ndogo kwa namba lakini ilikuwa ina thamani kuliko pengine 150 ya soko la saizi.
 
Ki uhalisia Ferguson kumpiga Beckham ni hasira za kibinadamu tu. Japo Kwa Kuwa yeye ni Ferguson basi inaangaliwa Kwa utofauti.

Tukirudi Kwenye bajeti bado napingana na wewe Kuwa Ferguson alikuwa na bajeti ndogo. By that time timu ambayo ilikuwa inaweza kushindana na sisi Kwenye usajili wa hela kubwa duniani alikuwa ni Madrid tu. Kwa maana nyingine tulikuwa tuna uwezo wa Ku spend kuliko timu zote Kwenye Epl. Na ndio maana tuliwanyanyasa ndani. Ila Chelsea na Man cty walipoanza kutumia pesa tuliamza Ku struggle.

Hebu nikupe changamoto nyingine, kama

Bei ya Maguire saizi unaambiwa ni zaidi ya 75, Ferdinand yule Kwa saizi ungempata Kwa sh ngap?

Rooney yule alisajiliwa Kwa 25 na soko la saizi Morata,Lukaku unawapata Kwa zaid ya 70. Rooney yule Kwa saizi angeuzwaje?? Maana yangu ni 25 ile ni ndogo kwa namba lakini ilikuwa ina thamani kuliko pengine 150 ya soko la saizi.
Huu ndio ukweli
 
Hivi wakuu niwaulize swali, mnadhani Ferguson kukaa miaka 20+ na kuchukua ndoo za UEFA mbili ni mafanikio? Kwa maana nyingine ni kwanini tulikuwa tunatisha sana EPL lakini hatuwa hatari nje ya epl?
Ndio ni mafanikio

Kuna ma Meneja wenye heshima zao duniani watakufa na hawatachukua hilo kombe kamwe

Lakini kumbuka mafanikio yake hayatajwi kwa sababu ya UCL tu, yanaangaliwa makombe mengine kama EPL,Kombe la FA na Kombe la Ligi pamoja Club Bingwa Dunia

Lakini pia linaangaliwa suala la kukaa timu moja kwa miaka yote kwa mafanikio (consistence katika mafanikio maana bila consistence angefutwa kazi na asingedumu timu moja hivyo)

SAF might be the greatest manager ever
 
Ndio ni mafanikio

Kuna ma Meneja wenye heshima zao duniani watakufa na hawatachukua hilo kombe kamwe

Lakini kumbuka mafanikio yake hayatajwi kwa sababu ya UCL tu, yanaangaliwa makombe mengine kama EPL,Kombe la FA na Kombe la Ligi pamoja Club Bingwa Dunia

Lakini pia linaangaliwa suala la kukaa timu moja kwa miaka yote kwa mafanikio (consistence katika mafanikio maana bila consistence angefutwa kazi na asingedumu timu moja hivyo)

SAF might be the greatest manager ever

Huoni kama alikuwa na consistency ndani ya Ligi pekee na Kwenye michuano ya nje Mara nyingi tulikuwa underdogs?
Mimi nadhani ni sahihi kusema yeye ni kocha bora wa muda wote Kwenye EPL ila sio duniani.,(mawazo yangu)
 
Huoni kama alikuwa na consistency ndani ya Ligi pekee na Kwenye michuano ya nje Mara nyingi tulikuwa underdogs?
Mimi nadhani ni sahihi kusema yeye ni kocha bora wa muda wote Kwenye EPL ila sio duniani.,(mawazo yangu)
No mkuu, ni kweli hakuwa mbabe UCL (Madrid ndio amenyanyasa zaidi kwenye hayo mashindano) lakini pia hakuwa mnyonge

Kwa miaka aliyotumikia Man Utd pale, ametolewa hatua ya makundi mara 3, miaka iliyobaki ameingia 16 bora had I fainali

Pia nikukumbushe tu ameingia nusu fainali UCL mara 7. Mtu kama huyu kusema hakufanikiwa nje ya Uingereza ni kumkosea heshima mkuu
 
No mkuu, ni kweli hakuwa mbabe UCL (Madrid ndio amenyanyasa zaidi kwenye hayo mashindano) lakini pia hakuwa mnyonge

Kwa miaka aliyotumikia Man Utd pale, ametolewa hatua ya makundi mara 3, miaka iliyobaki ameingia 16 bora had I fainali

Pia nikukumbushe tu ameingia nusu fainali UCL mara 7. Mtu kama huyu kusema hakufanikiwa nje ya Uingereza ni kumkosea heshima mkuu
Mafanikio ya Ferguson ni makubwa sana kwenye EPL japo hata EUFA champions league alitamba sana japo hakubeba makombe mengi sana ukilinganisha hata na Zidane tu ila bado aliitawala UEFA kwa kiwango kikubwa sana.
 
AAAAAAA unazingua ankal.... sijamwagia Misifa..... sema nilikuwa namtetea kidogo.... ila saiv hana muelekeo, ana ile 3rd Season syndrome where as club anayo manage lazima alikoroge..... Nakubali nilimtetea kabla, kwa sababu tulitakiwa tumpe muda kama SAF alivosema alipoach madaraka, lau kama ningeona positive changes hadi sasa ningemtetea ila dah!!! jahazi linazama habari hana yeye anawaza treasures zake ataondoka nazo vipi. Nampenda MOU lkn naipenda MUFC zaidi... atuache tu saiv

Hhhhh...vumilieni tu...mbona ss tulivumilia miaka 10...naona mashabiki ndo mnapiga kelele ila bodi ipo kimya na bado inamuamini...nasikia wanataka wampe tena hela asajili dirisha likifika...kwa sasa itabidi mfungwe tu hamna namna...
 
No mkuu, ni kweli hakuwa mbabe UCL (Madrid ndio amenyanyasa zaidi kwenye hayo mashindano) lakini pia hakuwa mnyonge

Kwa miaka aliyotumikia Man Utd pale, ametolewa hatua ya makundi mara 3, miaka iliyobaki ameingia 16 bora had I fainali

Pia nikukumbushe tu ameingia nusu fainali UCL mara 7. Mtu kama huyu kusema hakufanikiwa nje ya Uingereza ni kumkosea heshima mkuu
Mkuu huoni Kuwa hiyo inaweza Kuwa ni uthibitisho Kuwa alishindwa kushindana na ma giant? (Maana Mara nyingi kuanzia robo fainali ndio Mchele na chuya vinaanza kujitenga)
 
Mkuu huoni Kuwa hiyo inaweza Kuwa ni uthibitisho Kuwa alishindwa kushindana na ma giant? (Maana Mara nyingi kuanzia robo fainali ndio Mchele na chuya vinaanza kujitenga)
Mkuu hata hatua ya makundi kuna ma giant, angalia kinachomkuta Liverpool na Monaco sasa hivi

Hapo hatujaongelea hatua ya mtoani

Halafu kumbuka kuna timu nyingi bora sasa kweli unategemea kila mwaka yeye tu ndio ataingiza timu nusu fainali? Mkuu kuingiza timu nusu fainali mara 7 kwani ni mara chache? Wenger maisha yake yote ameingiza timu nusu fainali mara 1 (ile aliyofika fainali kisha kutolewa na Barca)

Angalia hata makocha bora unaowafahamu kama Guardiola wameingia nusu fainali mara ngapi, utakuta ni chache tu. Mourinho naye ameingiza mara 7
 
Hhhhh...vumilieni tu...mbona ss tulivumilia miaka 10...naona mashabiki ndo mnapiga kelele ila bodi ipo kimya na bado inamuamini...nasikia wanataka wampe tena hela asajili dirisha likifika...kwa sasa itabidi mfungwe tu hamna namna...
Liverpool miaka 10? Mmesota zaidi ya miaka 24 kila siku maumivu tu
 
Back
Top Bottom