Nyie mnaomsupport morinyo tunawasubiri tu siku mtakuja kumtolea mapovu humu..morinho sio kocha..huo ndo ukweli
Kuna vitu watu mnapost bila hata kufikiria ipo hivi nikufafanulie kwa faida yako na wenzeko wanaofikiria kumpa kampani kocha ni kosa hupaswi kukosoa au kumpa sapot ajae kwamba tunataka mourinho asitoke hapana mpo wrong sababu za kumtoa kocha hazina mashiko hata akitoka bado kwetu fresh kwa kuwa sisi ni manchester united sio mourinho united tunafaham mourinho anasoka bovu tena sana halipo katika tamaduni zetu jiulize kwa nini alipewa timu? Ina maana walitegemea atakuwa pep au klopp? Kapita madrid alitolewa kwa soka lake
Hapa tunasapot timu sio kocha hata kama ukisema humpend kocha ipi nguvu yako ya kumfukuza? Unajitesa bure shangilia timu yako kocha tumefukuza makoch wawili nini tumeambulia?
Soma hilo bango lilikuwepo uwanjani kwa nini? Ni baada ya watu wenye akili kuona bodi inafanya mambo ya kipuuzi kumpa mtu timu ambae si muumini wa soka letu kisha unakuja kumdhalilisha ni kitu kibaya bodi ndio inatakiwa kuvunjiliwa mbali
Angalia arsenal na barcelona wanavyotulia kulinda utamaduni wa mpira wao safi sana zile bao 5 arsenal kashinda sio bahat mbaya hapana katembea na njia za mzee wenger hajapata shida ya mfumo
Siwezi kuichukia timu na kocha wakati wapo wajinga fulani wanafanya maamuzi ya kutesa mashabiki hebu tuone chanzo kwanza kabla ya kumfikia mourinho
Kabla ya mourinho kulikuwa na makocha wazur tu washambuliaji
Walijua van gaal wanamfukuza kwa nini walifanya maamuzi ya kumpa timu mkabaji?
Nilisoma habar za arsenal walivyohangiaka kutafuta kocha wa mfumo wao walimpa arsene wenger muda na yeye walimshirikisha kutafuta mtu wa soka lao hata ufukuzwaji wake ulikuwa na muda sio kama sisi
Manchester city toka ianzishwe na mwekezaj wake 2008 wapo kwenye utamaduni wa soka lao ila sisi tumekuwa watu wa kujaribujaribu tunafeli tunataka makocha watoke halafu wakitoka wanakurupuka tena kutafuta kocha kisha tunananasa sehem mbaya hatupigi hatua hapo
Mimi hata aje kocha gani nitamsuport kama mourinho tu siwezi kulialia na kuponda timu na kocha ila wakicheza vibaya ntasema wakicheza vizur ntasema ndio ushabik ulivyo
Sina mentality ya kumeza kitu kimoja hicho hicho kwamba et lazima kocha atoke what for?