Mkuu ni kweli Mou amesajili wachezaji hao ulio wataja. Unapo sema anasajili wachezaji halafu anaishia kuwaweka benchi naona hauko sahihi. Katika wachezaji wote alio wasajili hapo ni Linderlof ndio alisubiri benchi na Lee grant maana inajulikana amekuja kama kipa namba tatu. Msimu wa kwanza alimsajili Baily,Mikh,Pogba na IBRA. IBRA alikuja kwa short term plan. Mikh ligi ndio imemshinda (sio kitu cha ajabu) . Msimu wa pili kaongeza Linderlof,Matic, Lukaku January akaja Sanchez kwa swap. Ila tuangalie timu aliyo ikuta ilikuwa ina hitaji additions au Reformation? Kwa upande wangu naona sehemu kubwa ya wachezaji walio kuwepo hawastahili kucheza man utd. Kwa hiyo ilibidi timu isukwe upya.
Nikizungumzia kwa upande wa bodi: kwa nini mtazamo wangu ni kwamba bodi haijampa sapoti?
Wakati Mou anapewa timu kuna vitu walikubaliana. La kwanza ilikuwa ni kuirudisha timu UEFA. Hilo amelifanya. Tangu Fergie astaafu kwa Mara ya kwanza timu imeweza kushiriki michuano ya uefa Mara mbili mfululizo.
La pili ilikuwa ni kuhakikisha timu kuanzia msimu wa pili inakuwa mshindani kwenye Ligi na hilo naweza kusema hajafanikiwa ila kwa sababu man cty alikuwa na msimu mzuri zaidi.
Point yangu ni nini?
Kama bodi wangekuwa wanataka kocha wa kutengeneza timu na mpira wa pasi basi hawakuwa na haja ya kumfukuza LVG. Kwa Van Gaal tulikuwa tuna posses hadi 80% lakini on target mbili. Kwa kumfukuza LVG ina maana bodi iliona timu inahitaji makombe na sio kujenga timu ya watoto au mpira wa pasi. Kama unataka makombe basi mtu sahihi ni Mou na ndio maana akapewa timu. Sasa ili Mou afanye hiyo kazi inabidi na yeye atimiziwe mahitaji yake.
Sasa tuseme kwamba Mou alikosea kusajili hao wachezaji na amegindua kuwa alikosea na bodi inagoma kutoa hela sababu alikosea kusajili hii itakuwa hasara kwa Man utd au Mourinho? Kama bodi inaona Mou hafai kwa sababu anachezea hela kwa nini wasimtoe mapema ili timu apewe MTU ambaye wana imani naye(kumbuka Mou kasini mkataba mpya January tu hapo)?
Pia tuangalie targets alizo kuwa anazitaka Mou ni kweli nafasi zao zina mapungufu au ndio alitaka kujaza watu? (LB,RW,CB)
Sent using
Jamii Forums mobile app