Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

38916115_10156867172158598_7135098288306388992_n.jpg

Fred conceded more fouls (3) in the opening 55 minutes than any other Man Utd or Leicester player.

Not a dream debut so far.
 

Mou ana miujiza ya ajabu,tusishangae game ijayo Shaw akawa bench.😀
 
Na kitu kinachoniboa mimi,ingekuwa Martial ndo kacheza hivi leo,basi angekaa benchi kwa mechi tano zijazo..narudia tena kusema sanchez usajili wake tulikurupuka tu..ni bora tungetafuta mtu wa kucheza winga ya kulia ambaye angeongeza nguvu ya ushambuliaji..

Martial sio kwamba nampenda sana,no,,sioni sababu ya sanchez kumweka benchi..

Rashford sijui anaelekea wapi huyu dogo..yasije yakawa yale ya welback

Bailly na lindelof wanaweza kutengeneza patnership nzuri,,kocha inabidi aendelee kuwapa nafasi

Perreira ni kama usajili mpya..trio yao yeye pamoja na pogba na fred ilikuwa nzuri sana...wamefanya mechi iwe na tempo ila sasa tatizo likaja kwenye washambuliaji wetu(rashford,sanchez,mata),,wote hawa walikuwa ovyo..

Nakubaliana na wewe.
 
Mourinho on Andreas Perreira.


He played a deep role in United's midfield three with Fred and Paul Pogba ahead of him and Mourinho was impressed with what he saw.

“I don’t want to go without bringing a message about Pereira, " Mourinho explained. "He was on the bench as a right winger at Valencia and came to Old Trafford as a number 6 and played phenomenally.”
 
HUKO England kumenoga, ni amshaamsha tu. Ile mikikimikiki ya Ligi Kuu England imerudi rasmi, usiku wa jana Ijumaa kulikuwa na mechi moja, lakini uhondo kamili unaanza leo Jumamosi na kuendelea kesho Jumapili.

Jana Manchester United ilikuwa na shughuli pevu huko Old Trafford ilipoikaribisha Leicester City na hiyo ilikuwa mechi ya kufungua pazia la Ligi Kuu England, ambapo kila kocha anajaribu kusaka njia za kuubeba ubingwa ambao msimu uliopita ulinyakuliwa na Manchester City ya Pep Guardiola.

Utamu wa ligi hiyo kwa timu za Top Six kwa msimu huu ni kwamba kutakuwa na makocha wawili wageni, Unai Emery huko Arsenal na Maurizio Sarri huko Chelsea.

Makocha hao wanakuja kuwapa changamoto wenyeji wao, Guardiola wa Man City, Jose Mourinho wa Man United, Jurgen Klopp wa Liverpool na Mauricio Pochettino wa Tottenham Hotspur.

Mchakamchaka wa msimu huu utashuhudia pia mastaa wa kigeni kibao wakitua kwenye Ligi Kuu England kuongeza uhondo utakaofanya utamu wa michuano hiyo pengine kuzidi misimu uliopita.

Mechi ya kwanza itakayofanyika mchana wa leo Jumamosi, Newcastle United inayonolewa na Rafa Benitez itakuwa nyumbani kuikaribisha Spurs, mechi inayotazamwa itakuwa ngumu kwelikweli kabla ya Bournemouth kumaliza ubishi na Cardiff City, Fulham ikiwa na mastaa wapya kibao wakishuka uwanjani kucheza na Crystal Palace, Watford ikicheza na Brighton na Wolves itakuwa na kasheshe mbele ya Everton. Kocha Sarri ataanzia shughuli ya Ligi Kuu England ugenini wakati atakapoifuata Huddersfield.

Lakini yote hiyo ni tisa, kumi bana ni vipute vya hiyo kesho Jumapili. Huko Emirates kutakuwa na kasheshe zito, wakati Emery na chama lake la Arsenal watakapowakaribisha mabingwa watetezi Man City.

Mechi hiyo inatarajia kuwa na ufundi mkubwa, huku Arsenal ikiingia uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kuchapwa Tatu Bila katika mechi ya mwisho ya ligi ilipocheza uwanjani Emirates dhidi ya vijana hao wa Guardiola.

Lakini mechi hiyo ya baadaye, itatanguliwa na mechi mbili matata, wakati Liverpool itakapokuwa Anfield kuikaribisha West Ham United, ambayo imefanya usajili mkubwa sana kwenye dirisha lililofungwa juzi Alhamisi.

Mechi nyingine itakayopigwa kesho ni ile ya Southampton itakapocheza na Burnely. Macho ya mashabiki baada ya kuona ile shughuli ya Man United usiku wa jana, sasa watasubiri kuona kipi kitafanywa na Chelsea, Tottenham, Man City na Arsenal kwenye mechi zao. Mambo ni moto!
 
Dondoo muhimu ufunguzi EPL

Beki wa Leicester City, Daniel Amartey amekuwa mchezaji wa kwanza kwenye Ligi Kuu ya England msimu huu, kusababisha penalti iliyozaa bao la kwanza, lakini pia amekuwa wa kwanza kupewa kadi ya njano katika mchezo wa kwanza msimu huu. Dakika 51. Man United vs Leicester City

Kiungo mpya wa Manchester City, Fred, amekuwa mchezaji wa pili kupewa kadi ya njano kwenye mchezo wa ufunguzi wa Ligi Kuu ya England. Dakika 55. Man United vs Leicester City

Beki wa Man United, Luke Shaw amekuwa mchezaji wa pili kufunga bao kwenye mechi ya ufunguzi wa msimu mpya wa Ligi Kuu ya England. Dakika 82. Man United vs Leicester City.
 
Kiungo wa Manchester United, Paul Pogba ameweka rekodi katika Ligi Kuu ya England kwa kupachika bao la kwanza la msimu mpya wa ligi hiyo.

Pia, Man United imekuwa timu ya kwanza msimu huu kupata penalti tena ya mapema (dakika tatu) kwenye mchezo dhidi ya Leicester City kwenye dimba la Old Trafford mjini Manchester.

Beki wa Leicester City, Daniel Amartey aliunawa mpira kwenye eneo la hatari na mkwaju wa penalti wa Pogba ulimshinda kipa Kasper Schmeichel na kuipa Man United bao la kuongoza.

Katika mchezo huo wa ufunguzi, Kocha Jose Mourinho amemfanya Pogba kuwa nahodha wa Man United. Licha ya kupata bao la mapema, kwenye mchezo huo Leicester City ilionekana kuwa moto na kutengeneza nafasi za mashambulizi pamoja na kumiliki sehemu kubwa ya mchezo. Hata hivyo, mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika, Man United ilikuwa mbele kwa bao 1-0.
 
Na kitu kinachoniboa mimi,ingekuwa Martial ndo kacheza hivi leo,basi angekaa benchi kwa mechi tano zijazo..narudia tena kusema sanchez usajili wake tulikurupuka tu..ni bora tungetafuta mtu wa kucheza winga ya kulia ambaye angeongeza nguvu ya ushambuliaji..

Martial sio kwamba nampenda sana,no,,sioni sababu ya sanchez kumweka benchi..

Rashford sijui anaelekea wapi huyu dogo..yasije yakawa yale ya welback

Bailly na lindelof wanaweza kutengeneza patnership nzuri,,kocha inabidi aendelee kuwapa nafasi

Perreira ni kama usajili mpya..trio yao yeye pamoja na pogba na fred ilikuwa nzuri sana...wamefanya mechi iwe na tempo ila sasa tatizo likaja kwenye washambuliaji wetu(rashford,sanchez,mata),,wote hawa walikuwa ovyo..
Kiongozi uko right 100%
 
Back
Top Bottom