Chief-Mkwawa
Platinum Member
- May 25, 2011
- 32,226
- 44,223
1. msimu wa kwanza wa mourinho Herrera ameonesha kiwango kikubwa kupata kutokea toka aanze kucheza mpira.Swali langu linarudi palepale Mou analalamika usajili je mpaka sasa tokea amekuja united amesajili wachezaji wangapi?? Kati yao wangapi wanaperform sawasawa na walikotoka? Pogba amekuja akiwa WC player micki, na wengine hawa wote wameshindwa kufanya vizuri shida ni nini?.
Kama alinunua wachezaji wazuri lakini wameflop na amekuta kina Martial Rashford wakiwa vizuri wote now wameflop wakija hao wengine tuna uhakika gani kama wataperform vizuri au ndo mauza uza yataendelea.
Kuna timu ndogo tu pale EPL zinapiga mpira mzuri kuliko sisi na hawana World class players.
Hitimisho Mou ndo tatizo pale period.
Mfano wake ni huyo perisic, yupo pia forsberg wa sweden/RB leipzig, vazquez madrid, di maria etc. Wapo japo ni wachache compare na zamani.Mkuu Katika Modern Football kwani Bado Upo Mpira huu Wa Winger Kibendera?
Mbona sasahivi Mawinga wote Ni Mafoward ambao unawakutia Wanafunga Magoli mengi Kuliko Mastriker!!
Winger Wa Kina Beckam umeshapotea Mkuu.
Wachezaji 12 wapo mapumziko, man u ina wachezaji gani tena waliobakia kubadili kikosi kizima kipindi cha pili?JOSE MOURINHO ana matatizo ya kisaikolojia na yamepanda stage, kwa washabiki wanaojua mpira hawatabishana kuwa Mou ni Muoga kupindukia alf uoga wake kwenuye timu kubwa kama United haufai.. Jinsi alivyojitetea baada ya mechi ya Liver na hata kikosi alichopanga asubuh ile na Madrid yote ni uoga. Kwa timu kama Manchester kupanga kikosi full cha wachezaj walioko alf unafanya sub tatu tu kama fainali vile, kina Sanchez anao kila siku kwann wacheze dk 90 wakati kuna madogo wanaoweza wakacheza tu kupima uwezo wao, huo ni uoga wa matokeo kitu ambacho kita mcost kweny kutengeneza timu.
1. msimu wa kwanza wa mourinho Herrera ameonesha kiwango kikubwa kupata kutokea toka aanze kucheza mpira.
2. Lukaku hajawahi cheza kwa mafanikio kama ya msimu uliopita
3. Ukitoa majeruhi Bailly anacheza vizuri sana na kiwango chake kinakua
4. DE Gea amechukua tuzo ya golden gloves (sina uhakika kama aliwahi)
5. Ibrahimovic hakuwahi kuchukua ubingwa wa ulaya kaupatia Man u hata kama ni Europa.
6. Valencia anakuwa regarded kama moja ya beki namba mbili bora duniani kwa sasa.
7. Rashford amefunga goli 7 msimu uliopita za ligi, ndio goli nyingi zaidi kufunga kwenye msimu toka aanze kucheza soka (nipe proof kwamba ameflop)
8. Martial katupia goli 10 hajafikisha zile 12 za msimu wa kwanza alipokuja ila there is no way mchezaji wa pembeni mwenye goli 10 akawa flop kama sijakosea leroy sane kamzidi goli 1 tu martial, na ukumbuke martial hajacheza mechi zote alikuwa akipokezana na rashford na sanchez
Wachezaji waliosajiliwa na mourinho kama Pogba, Bailly, ibrahimovic, Mkhitariyan, matic, lukaku etc wote wameperform vizuri sana with exception of lindelof ambae naamini ni star wetu wa baadae
Kuna mashabiki wanachosha mkuuWachezaji 12 wapo mapumziko, man u ina wachezaji gani tena waliobakia kubadili kikosi kizima kipindi cha pili?
wapo wengi mkuu Cuardado, Zaha, Willian, Lemar wapo wengi sana watu wanasahau kuwa kuna plans nyingi za kumaliza game kutoka na aina ya mechi husikaMfano wake ni huyo perisic, yupo pia forsberg wa sweden/RB leipzig, vazquez madrid, di maria etc. Wapo japo ni wachache compare na zamani.
Hahahaha mkuu Daud1990 hamuelewi kabisa jose
Rashford na Martial sio winga wa asili na wote wanacheza upande wa kushoto tunahitaji winger wa kulia, kama unaangalia mpira.
Mchezo wa rashford na martial ni akipata mpira anaingia ndani wachezaji hawa wanaitwa wing forward,
Tunaohitaji sisi ni winger wa kizamani design ya beckham ama giggs ama valencia etc ambao wakipata mpira wanatia majaro, tuna mtu kama Pogba, Lukaku, smalling, Fellaini etc wote ni magiant wanahitaji sana cross ila hatuna mtu wa pembeni wa kuzileta.
Ndio kama mdau alivyosema hapo juu mpira sio kukariri, sawa full backs wanapanda je wakiwekewa mawinger wenye mbio watapanda kama inavyotakiwa? Fullback kazi yako kumkaba ronaldo utakuwa wewe unacheza karibu na goli lako mda wote.Hiyo kazi inafanywa na fullbacks,kwa mpira wa sasa mkuu.
Mkuu sioni ni kitu gani Wachezaji wa Man City wanawazidi wa United, zaidi ya mbinu bora za Guardiola.Ukimtoa sanchez na de gea pengine na matic waliobakia wote ni vijana ambao wanahitaji kushikwa akili watulie.
Hebu tuangalie
MADRID~ experience ya modric na kroos katikati, una ramos nyuma na benzema na ronaldo mbele(kabla hajaenda juve) hapo bado kuna marcelo pia. Wote ni wachezaji ambao ni winners wana makombe kibao wanajua wawin vipi mechi.
MAN CITY~ wana silva na fernandinho kati wana Aguero na nyuma yupo kompany bila kumsahau de bruyne japo si sana, wote hawa ni viongozi wanaotuliza timu
BARCELONA~ kuna Pique, Bosquet, Messi, Jordi Alba na Iniesta kabla hajastaafu wote hawa uelewa wao wa club na uongozi wao kwa wachezaji wengine utamfananisha na nani?
JUVENTUS~ huku ndio usiseme kina Chielini, Buffon kabla hajaondoka, Higuain, marchisio, Matuidi etc wote wanajua nini maana ya kuchezea juve.
Sisi Angalau Pogba baada ya kuwin world cup anaweza kuwa matured msimu huu na kutusaidia ila wachezaji wetu wengi wana potential ila bado kuwa viongozi wa timu na kuwa na experience ya kuua mechi. Mtu kama martial, Rashford, shaw, pogba, Lingard, lukaku, wote wana utoto mwingi sana huwezi fananisha na hizo club hapo juu.
Mourinho amefanya kazi kubwa sana na hio timu na point 81 sio mchezo Leicester amechukua ubingwa na hizo point, its just Man city amefanya vizuri sana, ila sisi pia tumefanya vizuri, na naamini tuna kocha sahihi
Mimi mwenyewe wakati mwingine napata hisia hizo, msimu huu huenda ukawa wa neema kwetu.Fred hawezi kumuweka bench Pogba. Nafikiri Pereira na Fred ndiyo watakuwa wanabadilishana nafasi. I wish Pogba aongeze umakini kulenga goli.
Halafu nafikiri tofauti na wengine, MUFC itakuwa moto sana msimu huu. Ubingwa upo hakuna sababu ya kuwa wanyonge.
Ukimtoa walker wana mendy na danilo. Utamfananisha young na mendy?Mkuu sioni ni kitu gani Wachezaji wa Man City wanawazidi wa United, zaidi ya mbinu bora za Guardiola.
Nimeuliza Man City ukimtoa Walker wana beki gani wa kueleweka? Company utamlinganisha na Baily?
Man City wana beki mbovu sana kuilinganisha na United.
Sanchez,Pogba,Matic,De Gea,Lukaku ni Timu ipi duniani wanaanzia benchi? Hawa si hata Timu zao za Taifa still ni tegemeo?
Mourihno hana mbinu za kuipa makombe kwa sasa lawama anawatupia wachezaji.Kwa wachezaji walio United sioni Timu ya kuilinganisha kwa Uingereza.Van Gaal angepewa hii Timu angechukua ubingwa.
Sawa mkuu umenena vyema"MORINHO ANAKARIBIA KUISHI GHETTO MOJA NA DAZ BABA"
maisha yana mafumbo mengi sana. Kuna nyakati naamini msanii aliyewahi kutamba na kundi la Daz Nunda Ndugu Daz Baba kuna mda anajiuliza Maswali mengi pasipo majibu.
Nahisi kuna nyakati anasikiliza nyimbo zake alipokuwa na kundi lake halafu anasikiliza nyimbo zake binafsi Kama "elimu dunia" na "umbo namba 8" basi anatoa machozi ya kiume mwenyewe.
Naamini haamini kama nyimbo za msanii kama dogo Aslay zinagusu hata nusu ya ubora wa nyimbo zake.
Hayo ndiyo Maisha ya mateso ya nafsi anayopitia msanii Daz Baba anapokuwa ghetto kwake. Hawezi mwambie mtu zaidi ya kutoa machozi ya kiume.
Kwanini Daz Baba amkaribishe Morinho kwenye Maisha magumu ya ghetto?
Toka mwisho wa msimu wa 2017-2018 wa Epl, mropokaji Josee Morinho amekuwa hana furaha na Maisha ya ardhi ya Carrington.
Morinho amekuwa akiilaumu bodi ya usajili waziwazi mbele ya vyombo vya habari kitu ambacho siyo utamaduni wa Manchester United. Morinho amekuwa na migogoro ya Mara kwa Mara na wachezaji muhimu wa timu Kama Pogba, Fellaini na Athony Martial.
Achana na mifumo ya kuudhi anayotumia ambayo inawakera akina Eric Cantona, Paul Scholes, Giggs, Neville na mastaa kibao waliotamba united.
Siku chache zilizopita Christian Ronaldo aliweka wazi kuwa alishindwa kwenda united kwasababu hayupo tayari kucheza Kama beki wa pembeni kitu ambacho ni kijembe kwa Morinho kwa kutumia mfumo wa kuwatumia left and right wingers kama mabeki wa pembeni.
Yapo mengi sana ambayo naamini Maisha ya Morinho hayana furaha kwasasa pale united. Anachofanya ni kukaa Mahali mwenyewe na anapokumbuka mafanikio yake ya nyuma basi huanza kuhisi kama dunia imemtenga Kama ilivyomtenga Daz Baba.
Kwenye moyo wa Morinho amechukizwa na usajili wa Liverpool FC, amechukizwa na kutokupewa hela ya kusajili mastaa aliokuwa anawataka, na Bado anachukizwa na Uwepo wa Gurdiola kwenye nyasi za etihad.
Ni Shabiki pekee wa united anayeishi Namtumbo anaweza akachukulia poah matokea ya Pre-sisson pale marekani dhidi ya Liverpool lakini siyo kwa watu Kama akina Sir Alex Ferguson.
Sishangazwi Sana na tetesi za Zinedine Zidane Ndani ya Old Trafford. Naamini Morinho kwasasa hayupo sehemu salama kwenye vikao vya bodi ya Manchester United.
Ni Shabiki pekee wa Nkasi ambaye anafurahia matokeo ya united kushinda kwa wartford au Leicester City huku zaidi ya dk 75 anacheza Mfumo wa kuzuia.
Nyakati hazidanganyi kwasasa... Daz Baba yupo ghetto akikumbuka jinsi dunia ya viwanja vya shoo za Daz Nunda ilivyomtenga... Wakati Daz Baba yupo ghetto la Dar es salaam kuna mreno kiburi yupo ghetto la jiji la Manchester akiwa anawaza Mawazo Sawa na Daz Baba.
Karibu Epl uniondolee Mawazo ya wanasiasa.
[emoji767] KEY THE DON.