Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tungempata mtu kama mahrez,tungetisha sana..sema ndo hivo kaenda man.city
Sidhani kama tunamhitaji mhrez ujio wa fred ni faida kubwa kwa pogba coz fred anashambulia na anakaba pia afu anapiga pasi za mwisho hatari sana uwepo wake utafanya pogba acheze free role zaidi tunahitaji tu beki wa kati 1 na w pembeni 1 labda na forwad mkali maana lukaku huwa tu simuelewi
 
Sidhani kama tunamhitaji mhrez ujio wa fred ni faida kubwa kwa pogba coz fred anashambulia na anakaba pia afu anapiga pasi za mwisho hatari sana uwepo wake utafanya pogba acheze free role zaidi tunahitaji tu beki wa kati 1 na w pembeni 1 labda na forwad mkali maana lukaku huwa tu simuelewi
Ila lukaku jaman ule mguu mmoja unamtesa sana.
Yaan nyuma yako yupo hazard na de bruine alafu unashindwa kufunga.lukaku ni mzigo
 
Alexis Sanchez atakosa mazoezi ya mwanzo ya Manchester United nchini Marekani baada ya kukosa viza ya kuingia nchini humo.
Mshambuliaji huyo wa Chile (29), alikubalia adhabu ya kifungo cha miezi 16 jela mwezi Februari kwa kosa la kukwepa kodi nchini Hispania.
Kwa mujibu wa sheria ya Marekani, mtu yoyote anayepatikana na hatia ya kukwepa kodi hawezi kupata viza ya kuingia nchi hiyo.
 
Jose Mourinho ametoa wiki tatu tu za mapumziko kwa wachezaji wake waliotoka kwenye fainali za Kombe la Dunia 2018 huko Russia na baada ya hapo warudi mzigoni huko Manchester United haraka.

Wachezaji saba wa Man United wamehusika kwenye mechi za Kombe la Dunia 2018 za wikiendi ya mwisho kabisa, ambayo ni juzi Jumamosi na jana Jumapili, lakini Kocha Mourinho amewataka warudi Old Trafford hadi kufikia Agosti 6.

Kuna mpango wa kuwaanzishia benchi wachezaji hao katika mechi yao ya kwanza ya Ligi Kuu England, Man United itakayomenyana na Leicester City, Agosti 10.

Jesse Lingard, Ashley Young, Marcus Rashford na Phil Jones waliokuwa kwenye kikosi cha England, wakati Romelu Lukaku na Marouane Fellaini walikuwa na kikosi cha Ubelgiji na Paul Pogba alikuwa kwenye kikosi cha Ufaransa ambapo wachezaji hao walikuwapo kwenye fainali za Kombe la Dunia 2018 iliyomalizika juzi
 
Man United itazindua ziara yake ya Marekani kwa mechi dhidi ya Club America mjini Phoenix, Ijumaa hii.

Baada ya hapo itakipiga na San Jose Earthquakes Jumapili kisha itafuatiwa na mechi dhidi ya vigogo AC Milan, Liverpool na Real Madrid.
 
Ila lukaku jaman ule mguu mmoja unamtesa sana.
Yaan nyuma yako yupo hazard na de bruine alafu unashindwa kufunga.lukaku ni mzigo
Lukaku ni mzigo? Acha masihara bana ligi imeisha msimu wa kwanza katupa goli 17 kombe la dunia ana goli nne na assist 2 mpe credit bana kwangu mm ni usajili bora wa striker.
 
Inasikitisha hawa jamaa bado wanachezea United
IMG_20180715_091224.jpg
 
OFFICIAL: Dejan Lovren has made the FIFA World Cup team of the tournament.
IMG_20180717_194103.jpg
 
  • Thanks
Reactions: cpt
Macheda + Martial +tRashford= The next big thing that never happened to become
 
Turudi nyumbani jamani pamenoga yale mambo ya vishoka (Russia )yamekwisha hongera kwa vijana wetu wote walio wakilisha timu mbalimbali za mataifa yao.
 
Back
Top Bottom