Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Cheki hapa ratiba iliyobaki kwa kila timu na wanavyotabiriwa namna watakavyomaliza msimu kwa pointi watakazovuna.

MAN UNITED

Msimamo: Nafasi ya Pili

Pointi : 65

Mechi: 30

Ratiba mechi zilizobaki

Man City v Man United

Man United v West Brom

Bournemouth v Man United

Man United v Arsenal

Brighton v Man United

Man United v Watford

West Ham v Man United

Hii ilikuwa kabla ya mechi ya jana Jumamosi huko Old Trafford, Manchester United ilipotarajia kumenyana na Swansea City. Ukiondoa mechi ya ugenini kwa Manchester City, ratiba ya Man United inaonekana kuwa nyepesi kwa kiasi fulani na kwamba kuna uhakika mkubwa wa kuendelea kuishikilia nafasi yao hiyo hadi mwisho wa msimu. Kwa mechi hizo za Man United, matarajio wanaweza kushinda si chini ya mechi saba na hivyo kuwa sawa. Kama mambo yatakwenda kama yalivyotarajiwa, Man United inaweza kumaliza ligi ikiwa na pointi 82.
 
IMG_20180402_153529_614.JPG
 
Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho anaamini haiwezekani kukimbizana na Manchester City msimu huu katika mbio za ubingwa Ligi Kuu.
City ililaza Everton 3-1 Jumamosi, hiyo ina maana wanahitaji ushindi katika mechi moja tu ili wajitangazie ubingwa kwa mara ya kwanza tangu msimu wa 2013-2014 iwapo watafanikiwa kuifunga Man United kwenye Uwanjani Etihad wikiendi ijayo.
Man United ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 68 baada ya kucheza mechi 31. Wakiwa wameachwa nyuma kwa pointi 16 na City.

Katika ligi nyingine, tungekuwa bado tunapigania taji," alisema Mourinho.
United wamo mbioni kumaliza ligi wakiwa na alama za juu zaidi Ligi Kuu tangu msimu walioshinda ligi 2012-13 wakiwa na Sir Alex Ferguson msimu wake wa mwisho.
Misimu iliyofuata,walimaliza nafasi ya saba, nne, tano na sita.
Baada ya kuondolewa Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya 16 bora na Sevilla, na kisha kutuhumiwa kwa kucheza mchezo usio wa kuvutia, Mourinho amekosolewa sana msimu wake wa pili akiwa kocha wa Man United.

Mreno huyo anatetea sana matokeo ya klabu hiyo, na mapema mwezi huu alitoa hotuba ya dakika 12.
Kabla yao kushinda 2-0 nyumbani dhidi ya Swansea Jumamosi, Mourinho alitumia ujumbe wake kwenye ratiba ya mechi kusisitiza tena kwamba United ni "klabu iliyo kwenye mpito".
Baadaye, alitaja rekodi yao ligi na pia kwamba wanacheza nusu fainali Kombe la FA dhidi ya Tottenham kama ishara kwamba wameimarika msimu huu.

Msimu uliopita, tulishinda vikombe lakini tukamaliza nafasi ya sita katika ligi," alisema Mourinho ambaye alishinda Kombe la Ligi na Europa Ligi msimu uliopita.
"Tunataka kumaliza wa pili msimu huu na tuna alama 10 zaidi ya msimu uliopita, tumefunga mabao mengi, tumefungwa mabao machache, lakini kuna klabu ambayo imeifanya kuwa vigumu sana kuwakimbiza.
"Tumekuwa na msimu mzuri na bado tunacheza Kombe la FA. Tutapigania nafasi yetu huko."
 
Wadau hivi tunalakujifunza kwenye game ya city v liverpool kuelekea game yetu ya kutunza heshimu hiyo j1 au mou kama kawaida ni mzee haambiliki?
Najua wengi wetu watakuja na madai kuwa hatuna wachezaji wa kaliba ya akina OX kuweza kufanya walichofanya liverpool,kwangu hiyo bado sio sababu toshelezi. Mou angalau arudishe imani ya mashabiki wake kuhusu msimu wa 2018/2019 kwa kushinda hii game the easy way,tofauti na hapo tujiandae kugombea top 4 tena.
 
Wadau hivi tunalakujifunza kwenye game ya city v liverpool kuelekea game yetu ya kutunza heshimu hiyo j1 au mou kama kawaida ni mzee haambiliki?
Najua wengi wetu watakuja na madai kuwa hatuna wachezaji wa kaliba ya akina OX kuweza kufanya walichofanya liverpool,kwangu hiyo bado sio sababu toshelezi. Mou angalau arudishe imani ya mashabiki wake kuhusu msimu wa 2018/2019 kwa kushinda hii game the easy way,tofauti na hapo tujiandae kugombea top 4 tena.
Tukifungwa hio mechi nitabaki na mechi moja tu ya kuangalia msimu huu au mbili zote za FA kama tutapita. Maana sitaangalia tena mechi ya man u.
 
Wadau hivi tunalakujifunza kwenye game ya city v liverpool kuelekea game yetu ya kutunza heshimu hiyo j1 au mou kama kawaida ni mzee haambiliki?
Najua wengi wetu watakuja na madai kuwa hatuna wachezaji wa kaliba ya akina OX kuweza kufanya walichofanya liverpool,kwangu hiyo bado sio sababu toshelezi. Mou angalau arudishe imani ya mashabiki wake kuhusu msimu wa 2018/2019 kwa kushinda hii game the easy way,tofauti na hapo tujiandae kugombea top 4 tena.
Hahahaaa Mau ni jiwe kama bwana yule....
 
Wadau hivi tunalakujifunza kwenye game ya city v liverpool kuelekea game yetu ya kutunza heshimu hiyo j1 au mou kama kawaida ni mzee haambiliki?
Najua wengi wetu watakuja na madai kuwa hatuna wachezaji wa kaliba ya akina OX kuweza kufanya walichofanya liverpool,kwangu hiyo bado sio sababu toshelezi. Mou angalau arudishe imani ya mashabiki wake kuhusu msimu wa 2018/2019 kwa kushinda hii game the easy way,tofauti na hapo tujiandae kugombea top 4 tena.
Man city kapigwa na livapuli mara mbili tena goli kuanzia tatu lakini livapuli kashindwa kumfunga mourinho msimu huu zaidi ya kubiringwa biringwa na Rashford huku salah akiwekwa mfukoni na Ashley fvcking young, kwann asipewe credit?

Mnataka tuende kichwa kichwa kama kipara alivoenda kichwa kichwa kwa liva na akalia? Mourinho ni mastermind yupo tayari apange mabeki wote as long as hiyo ndio itakua njia pekee ya kumzuia city, and for this am supporting my manager as long as we won't lose.
 
Man city kapigwa na livapuli mara mbili tena goli kuanzia tatu lakini livapuli kashindwa kumfunga mourinho msimu huu zaidi ya kubiringwa biringwa na Rashford huku salah akiwekwa mfukoni na Ashley fvcking young, kwann asipewe credit?

Mnataka tuende kichwa kichwa kama kipara alivoenda kichwa kichwa kwa liva na akalia? Mourinho ni mastermind yupo tayari apange mabeki wote as long as hiyo ndio itakua njia pekee ya kumzuia city, and for this am supporting my manager as long as we won't lose.

As long as we wont lose,fine. Lakini kwanini tactics za mou zitufanye tuwe underdogs kwa city? Point yangu ni kwamba je,tuko tayari kushindana msimu ujao kwa mbinu hizo hizo maana hii game itatupa mwanga kama kweli game ya kwanza tulikusudia kudroo au kutafuta point 3. Man U inakila kitu hivyo tujengewe timu ya kutafuta point 3 kila game na si kuchagua game za kushambulia.
Imagine tunakwaana na city uefa knockout stage,tutaazimia kutafuta droo pia?
 
As long as we wont lose,fine. Lakini kwanini tactics za mou zitufanye tuwe underdogs kwa city? Point yangu ni kwamba je,tuko tayari kushindana msimu ujao kwa mbinu hizo hizo maana hii game itatupa mwanga kama kweli game ya kwanza tulikusudia kudroo au kutafuta point 3. Man U inakila kitu hivyo tujengewe timu ya kutafuta point 3 kila game na si kuchagua game za kushambulia.
Imagine tunakwaana na city uefa knockout stage,tutaazimia kutafuta droo pia?
Miaka ya hivi karibuni United imekua ni underdog kwa city, sio kipindi cha mourinho tu, van gaal, moyes hata Ferguson mwenyewe huku mwishoni city alikua akimsumbua sana.

Mbinu za mourinho ni kukupa makombe kama unataka entertainment basi WWE is better for you. Mechi hata bado haijachezwa watu mshaanza kulalamika sababu ya walichofanya livapuli jana, what the fvck??????????

Mourinho hajawahi fungwa home and away na kocha mmoja and am sure haitatokea kwa msimu huu.
 
Sasa faida ya utajiri wa club yetu na uwekezaji wa milioni una maana gani kama tunakubali kuwa wanyonge kwa the citizens? Chini ya fergie hata kama walikuwa wanatusumbua lakini mpira ulikuwa unachezeka na ndio maana kulikuwa na thrills za ushindi wa magoli ya mwishoni mwishoni,rooney,owen na rvp kama unakumbuka.
 
Back
Top Bottom