Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tetesi
Manchester City na Manchester United zote kwa pamoja zitapambana kujaribu kumsajili nyota wa Brazil Neymar iwapo ataamua kuondoka Paris St-Germain.

Kufuatia kocha wa Manchester Jose Mourinho kumshambulia kwa maneno mlinzi wa kushoto wa klabu hiyo Luke Shaw, kunaweka pia hatarini kumpata winga wa Real Madrid na raia wa Wales Gareth Bale. (mail)

Gareth Bale ataondoka Real Madrid na kujiunga na Manchester United wakati wa majira ya joto iwapo Zinedine Zidane atasalia kuiongoza miamba hiyo ya Bernabeu .(mirror)

Lakini mshambuliaji huyo wa Real Madrid, ameambiwa na meneja wa Wales na kiungo wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs kusalia katika La Liga kuliko kurudi Premier League. (express)

Mshambuliaji wa Manchester United Marcus Rashford, 20, ameibuka kuwa gumzo kwa klabu ya Real Madrid wakihitaji kumsajili majira ya joto. (Sport via Mail)

Vilabu vya Manchester City na Manchester United vinawania kumsajili mlinzi wa kati wa Ujerumani na Bayern Munich Jerome Boateng. (Sun)

Manchester United imetenga kitita cha Pauni milioni 40 kumshajili kiungo wa Bayern Munich na Brazil Douglas Costa, aliye kwa mkopo Juventus. (Mirror)
 
Manchester United inasema kwamba sababu ya mshambuliaji wa Chile Alexis Sanchez kupigwa picha akila pekee katika uwanja wa mazoezi ni kwamba alisalia nyuma ili kufanya mazoezi ya kupiga mikwaju. (Star on Sunday)
 
Tetesi

Manchester United iko tayari kumuuza kiungo wa Ufaransa ,25 Paul Pogba . Wachezaji inaowanyatia ni beki wa Real Madrid Raphael Varane, 24, na kiungo wa kati wa Ujerumani Toni Kroos, 28, beki wa Paris St-Germain na Brazil Marquinhos, 23, na kiungo wa kati wa Itali Marco Verratti, 25, pamoja na beki wa Juventus, 27, raia wa Brazil Alex Sandro. (Sunday Mirror)

Pogba na mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho hawazungumziani baada ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa kuwachwa nje na klabu yake mwezi uliopita (Sun on Sunday)

Mourinho hadhani kwamba ''uwezo wa wachezaji'' unaweza kumfuta kazi katika klabu ya Old Trafford. (Mail on Sunday)
 
Tetesi

Manchester United iko tayari kumuuza kiungo wa Ufaransa ,25 Paul Pogba . Wachezaji inaowanyatia ni beki wa Real Madrid Raphael Varane, 24, na kiungo wa kati wa Ujerumani Toni Kroos, 28, beki wa Paris St-Germain na Brazil Marquinhos, 23, na kiungo wa kati wa Itali Marco Verratti, 25, pamoja na beki wa Juventus, 27, raia wa Brazil Alex Sandro. (Sunday Mirror)

Pogba na mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho hawazungumziani baada ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa kuwachwa nje na klabu yake mwezi uliopita (Sun on Sunday)

Mourinho hadhani kwamba ''uwezo wa wachezaji'' unaweza kumfuta kazi katika klabu ya Old Trafford. (Mail on Sunday)
Mou huyu
 
SUPASTAA, Neymar ameripotiwa kuzungumza na wakala wake kuhusu ofa zinazoletwa kumhusu yeye ili ang’oke Paris Saint-Germain mwishoni mwa msimu huu.

Real Madrid imetajwa kwa muda sasa kuhitaji huduma yake, lakini, kwa sasa zimeibuka timu nyingine zinazohitaji saini ya Mbrazili hiyo, Manchester United na Manchester City. Hata hivyo, pesa ndiyo itakayoamua.

Hapa ndipo utakutana na ile methali ya mwenye kisu kikali ndiye atakayekula nyama. Man United wanataka kutumia vyanzo mbalimbali vya kipesa kunyakua huduma ya supastaa huyo anayeuguza majeraha ya mguu kwa sasa.

Kocha wa Man City, Pep Guardiola yupo tayari kuingia vitani kunasa saini ya mchezaji huyo na ametenga Pauni 300 milioni. PSG wenyewe wanaonekana wanachosubiri kwa sasa ni pesa tu. Kama watamuuza kwa Pauni 300 milioni, hapo watakuwa ameingiza faida kubwa sana, zaidi ya Pauni 100 milioni.

Kusikia hivyo, kocha wa Man United, Jose Mourinho naye ameingia vitani kumsajili Neymar na anaamini atamnasa. Mourinho anamhitaji pia Marco Asensio kwenye kikosi chake msimu ujao. Mourinho anaamini katika matumizi ya pesa.

Ripoti zinadai ukiweka pesa kando, Mourinho anataka kumtumia pia Paul Pogba kumnasa Neymar.

Kilichopo ni, Pogba anaweza kupelekwa PSG pamoja na pesa ili Neymar atue Old Trafford.

Ripoti za ndani kabisa kutoka Old Trafford zinadai wadhamini wa timu hiyo, Chevrolet ndiyo watakaofanya mchakato mzima wa kuhakikisha Neymar anazipiga chini Real Madrid na Man City na kutua Man United.

Taarifa zaidi zinadai kwa timu hizo zilizotajwa hapo, Man United pekee ndiyo wenye jeuri ya kumlipa mshahara atakaoutaka Neymar. Kwa sasa Mbrazili huyo anakunja pesa ndefu huko PSG, Pauni 775,477 kwa wiki ukijumlisha bonasi zote. Mshahara pekee haupungui Pauni 600,000 kwa wiki.

Kwa hesabu hizo, si Man City wala Real Madrid wanaonekana kuwa uwezo wa kumudu mshahara wa wiki wa staa huyo zaidi ya Man United tu, ambao kulipa mkwanja mrefu kama mshahara wa wiki si tatizo kwao kama kwa sasa tu wanamlipa Alexis Sanchez zaidi ya Pauni 500,000 kwa wiki.

Kitu kingine Man United wana uhakika, wadhamini wao Chevrolet wanaweza kuweka mkwanja mrefu, huku dili likionekana kukaa vizuri Adidas pia wanaweza kulifurahia kama ilivyofanya kwa staa Pogba, wakati alipotua kwa pesa nyingi Old Trafford.

Man United inalenga kujiboresha zaidi sokoni kuvutia dili za kibiashara, hivyo kuwa na wachezaji mastaa kutawafanya nembo yao kuendelea kutikisa Ulaya na duniani kwa jumla.

Chevrolet ndiyo wadhamini wakuu wa Man United wanaotokea kwenye jezi zao, huku Adidas pia wakimwaga mkwanja mrefu kwenye kikosi hicho chenye maskani yake Old Trafford. Mourinho alishawahi kumwambia Neymar anamtaka aende Man United ambako atakwenda kumfanya kuwa staa mkubwa na nembo ya timu hiyo kama ilivyo kwa mastaa wenzake Lionel Messi ni Barcelona wakati Cristiano Ronaldo ni Real Madrid.
 
SUPASTAA, Neymar ameripotiwa kuzungumza na wakala wake kuhusu ofa zinazoletwa kumhusu yeye ili ang’oke Paris Saint-Germain mwishoni mwa msimu huu.

Real Madrid imetajwa kwa muda sasa kuhitaji huduma yake, lakini, kwa sasa zimeibuka timu nyingine zinazohitaji saini ya Mbrazili hiyo, Manchester United na Manchester City. Hata hivyo, pesa ndiyo itakayoamua.

Hapa ndipo utakutana na ile methali ya mwenye kisu kikali ndiye atakayekula nyama. Man United wanataka kutumia vyanzo mbalimbali vya kipesa kunyakua huduma ya supastaa huyo anayeuguza majeraha ya mguu kwa sasa.

Kocha wa Man City, Pep Guardiola yupo tayari kuingia vitani kunasa saini ya mchezaji huyo na ametenga Pauni 300 milioni. PSG wenyewe wanaonekana wanachosubiri kwa sasa ni pesa tu. Kama watamuuza kwa Pauni 300 milioni, hapo watakuwa ameingiza faida kubwa sana, zaidi ya Pauni 100 milioni.

Kusikia hivyo, kocha wa Man United, Jose Mourinho naye ameingia vitani kumsajili Neymar na anaamini atamnasa. Mourinho anamhitaji pia Marco Asensio kwenye kikosi chake msimu ujao. Mourinho anaamini katika matumizi ya pesa.

Ripoti zinadai ukiweka pesa kando, Mourinho anataka kumtumia pia Paul Pogba kumnasa Neymar.

Kilichopo ni, Pogba anaweza kupelekwa PSG pamoja na pesa ili Neymar atue Old Trafford.

Ripoti za ndani kabisa kutoka Old Trafford zinadai wadhamini wa timu hiyo, Chevrolet ndiyo watakaofanya mchakato mzima wa kuhakikisha Neymar anazipiga chini Real Madrid na Man City na kutua Man United.

Taarifa zaidi zinadai kwa timu hizo zilizotajwa hapo, Man United pekee ndiyo wenye jeuri ya kumlipa mshahara atakaoutaka Neymar. Kwa sasa Mbrazili huyo anakunja pesa ndefu huko PSG, Pauni 775,477 kwa wiki ukijumlisha bonasi zote. Mshahara pekee haupungui Pauni 600,000 kwa wiki.

Kwa hesabu hizo, si Man City wala Real Madrid wanaonekana kuwa uwezo wa kumudu mshahara wa wiki wa staa huyo zaidi ya Man United tu, ambao kulipa mkwanja mrefu kama mshahara wa wiki si tatizo kwao kama kwa sasa tu wanamlipa Alexis Sanchez zaidi ya Pauni 500,000 kwa wiki.

Kitu kingine Man United wana uhakika, wadhamini wao Chevrolet wanaweza kuweka mkwanja mrefu, huku dili likionekana kukaa vizuri Adidas pia wanaweza kulifurahia kama ilivyofanya kwa staa Pogba, wakati alipotua kwa pesa nyingi Old Trafford.

Man United inalenga kujiboresha zaidi sokoni kuvutia dili za kibiashara, hivyo kuwa na wachezaji mastaa kutawafanya nembo yao kuendelea kutikisa Ulaya na duniani kwa jumla.

Chevrolet ndiyo wadhamini wakuu wa Man United wanaotokea kwenye jezi zao, huku Adidas pia wakimwaga mkwanja mrefu kwenye kikosi hicho chenye maskani yake Old Trafford. Mourinho alishawahi kumwambia Neymar anamtaka aende Man United ambako atakwenda kumfanya kuwa staa mkubwa na nembo ya timu hiyo kama ilivyo kwa mastaa wenzake Lionel Messi ni Barcelona wakati Cristiano Ronaldo ni Real Madrid.
huyo neema nae mbona kama anakuzwa kichwa sana?
 
Hapo sasa kijana ashtuke hizo sifa zitammaliza mapema,ni bora kuwa na haters kama c ronaldo au messi ili kupambana kuwaonyesha haters wanakosea kuwaletea chuki kuliko kusifiwa kila siku kama neymar
huyo neema nae mbona kama anakuzwa kichwa sana?
 
Hivi ni kweli Mou kasema hamuhitaji pogba katika kikosi chake?
 
Jamani uzi wetu siku hizi hauendi kabisa,mjinga pep katufarakanisha tayari.
 
"The football I grew up playing is no longer there. Today, all players care about is their cars, their shoes with their names on, and their image. While for me, the only thing that counted was football. Nothing else."

- Miroslav Klose.


Alichosema klose kipo kwa wachezaji wetu wengi sana na ndio kinaturudisha nyuma.
 
Tetesi

Barcelona wanapanga kuwasilisha ombi la kutaka kumchukua beki wa Manchester United Luke Shaw mwisho wa msimu. Beki huyo wa kushoro wa miaka 22 kutoka England amekosolewa sana na meneja wa United Jose Mourinho wiki za karibuni. (Mirror)

Meneja wa Manchester United Mourinho ameandaa orodha ya wachezaji sita ambao anaamini wanaweza kujaza nafasi ya Michael Carrick anayeelekea kustaafu. Orodha hiyo inashirikisha nyota wa Bayern Munich kutoka Chile Arturo Vidal, 30, na Mwitaliano anayechezea Paris St-Germain Marco Verratti, 25. (Manchester Evening News)

United wataimarisha juhudi zao za kutaka kumnunua beki wa Celtic ambaye thamani yake inakadiriwa kuwa £25m Kieran Tierney mwisho wa msimu. Mourinho anataka sana beki huyo wa miaka 20 mzaliwa wa Manx, Scotland ajiunge na klabu hiyo na anatarajiwa kuwasilisha ofa karibuni. (Mirror)

Mchezaji nyota wa Brazil Ronaldinho amefichua wkamba alikuwa saa 48 karibu na kujiunga na United mwaka 2003 kujaza nafasi ya David Beckham aliyekuwa amehamia Real Madrid. Badala yake mchezaji huyo wa miaka 38 alijiunga na Barcelona pale Sandro Rosell alipoteuliwa rais wa klabu hiyo. (FourFourTwo)

Mabingwa wa Ufaransa Monaco ndiyo klabu ya karibuni zaidi kuonesha nia ya kumtaka kiungo wa kati wa Manchester United Marouane Fellaini. Mkataba wa mchezaji huyo wa miaka 30 kutoka Ubelgiji unamalizika mwisho wa msimu na anatarajiwa kuondoka Old Trafford. (Mail)
 
Back
Top Bottom