Baada ya kuitenda miujiza sehemu tofauti duniani. Messi alitoka Camp Nou akafika mji wa Madrid. Watu wengi walijaa uwanja wa Santiago Bernabeu kumlaki mfalme huyo wa soka... Atoaye ubatizo wa moto.
Natazama kulikuwa na mchezaji wa Real Madrid aitwayeCR7..Naye amepata upofu wa kushindwa kuziona nyavu za timu pinzani. Aliposikia Messi anapita alipaza sauti.. Mesiiiiiii, mesiiiiiii mfalme nihurumie...Nataka kuona Ili nianze kufunga tena.
Messi alipomuona moyo wake ukaingiwa na huruma. Akamfuata, akamwambia..Maadam umekiri mimi ndiye mfalme wako. Nakuamuru uone tena sawa sawa na imani yako. Baada ya kuona, Cr7 akamwambia Messi, nitakufuata popote utakapokwenda.
Messi akamjibu, nenda kwenye ofisi ya Frolentino perezz. Akupe nauli Urudi Ureno, ukapate kusimulia miujiza aliyokutendea LIONEL MESSI LAPULGA