" Niliwashauri wawasajili Mbappe na G.Jesus " - Giggs.
Winga wa zamani wa Manchester United Ryan Giggs amesema kwamba aliiambia klabu kuwasajili Kylian Mbappe na Gabriel Jesus mwaka mmoja kabla ya kuibuka kwenye ramani ya ulimwengu wa soka.
Giggs ambaye aliwahi kuwa kocha msaidizi wa Manchester United chini ya Utawala wa Louis van Gaal kuanzia 2014-2016 amekiri kwamba alitofautiana na mdachi huyo kuhusu Sera ya usajili ndani ya klabu.
Giggs amekiri kwamba aliwaskauti wachezaji hao wawili Mbappe na Jesus chini ya utawala wa Van Gaal na kuishauri klabu kuwasajili vijana hao kabla hawajawa nyota wakubwa Duniani.
Mbappe,19 alijiunga na PSG kwa mkopo kutoka Monaco mwezi Agosti kukiwa na kipengele cha kufanya uhamisho huo kuwa wa kudumu kwa dau la Pauni Milioni 166 majira yajayo ya kiangazi baada ya kuonyesha kiwango bora sana msimu uliopita.
Huku , Jesus mwenye umri wa miaka 20 tayari ameshafunga magoli 15 kwa mahasimu wa United, Manchester City tangu aliphamia hapo mwezi januari kutoka Palmeiras kwa dau la Pauni Milioni 27.
" Nilimuangalia Gabriel Jesus akicheza miaka mitatu iliyopita . Nilimuangalia Mbappe kwa mwaka mzima . Nilikuwa nawaangalia nikiwa na skauti na ilikuwa wazi kabisa kuhusu vipaji vyao." Amesema Giggs kwenye mahojiano na The Times.
" Ilikuwa kama kusema, ' nenda wachukueni'. Ingeweza kuwa Pauni Milioni 5 au zaidi kidogo tu , wanunue halafu warudisheni kwa mkopo - na hapo ndio idara ya usajili ilitakuwa kufanya kazi nzuri."
United walifanya usajili mkubwa pindi Van Gaal alipokuwa madarakani , usajili wa wachezaji Angel Di Maria, Memphis Depay, Anthony Martial, Morgan Schneiderlin na Radamel Falcao.
Licha ya usajili mkubwa wa klabu , Giggs alihisi kwamba wachezaji waliosajili walikuwa hawana utambulisho wa mchezaji wa Man United - sababu ambayo ilileta kombe moja ndani ya miaka miwili ya utawala wa Van Gaal.
" Najua mchezaji wa Manchester United anavyoonekana ." Ameongeza Giggs.
" Kumekuwa na wachezaji wengi walioingia ndani ya United ambao hawana sifa ya kuwa mchezaji wa Man United na pia wachezaji ambao walikuwa na sifa ya Man United kuruhusiwa kuondoka."
" Naongea kuhusu Rafael [Da Silva], Danny [Welbeck], na Jonny Evans wachezaji ambao wana damu ya Man United , wanaocheza mpaka filimbi ya mwisho ."
" Ilikuwa ngumu kwasababu Louis alikuwa na mitazamo yake mwenyewe na unalazimika kuheshimu hilo lakini ni kweli
tuliwahi kuwa na mahojiano kuhusu baadhi ya wachezaji. Alinielewa kwasababu niliwahi kucheza na hao wachezaji , lakini hawakuwa chaguo lake."
" Baadhi yao kama Welbeck alikuwa anataka kucheza mara kwa mara , Jonny alikuwa na majeraha kadhaa muda ule , kwahiyo ulikuwa unaweza kuelewa kwa hilo - lakini idara ya usajili chini ya Van Gaal haikufanya kazi nzuri sana kwa daraja la sifa ya United."