Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tetesi
MAN UTD WANAMTAKA KINDA WA WHITECAPS


Manchester United wamemwalika kinda wa Vancouver Whitecaps Alphonso Davies kufanya majaribio Januari kwa mujibu wa CTV Edmonton .
Kinda huyo wa miaka 17 ambaye amekuwa mchezaji mdogo zaidi kuichezea timu ya taifa ya Canada majira ya joto, anasubiri kupata kibali kutoka kwenye klabu yake kutua United.
 
Tetesi
ROMERO ANAFIKIRIA KUONDOKA MAN UTD


Sergio Romero anafikiria kuondoka Manchester United dirisha la uhamisho wa Januari kabla ya kuanza kwa Kombe la Dunia majira ya joto, kwa mujibu wa Daily Mail .
Romero ameendelea kuwa mlinda mlango chaguo la kwanza kwa Argentina, licha ya kucheza kama kipa nambari mbili United nyuma ya David de Gea.
 
Tetesi
MAN UTD BADO WANAMTAKA PERISIC


Manchester United bado wanaitamani huduma ya Ivan Perisic baada ya kumkosa winga huyo wa Inter uhamisho wa majira ya joto, kwa mujibu wa The Sun .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Croatia alisaini mkataba mpya kubaki Italia, lakini mchakato huo ulifanyika kutunza thamani yake ila anaweza kupatikana Januari kwa dau la £45 milioni.
 
Tetesi
UTD YATENGA £95M KUMPATA NYOTA WA LAZIO


Manchester United wanataka kuvunja rekodi yao ya usajili kwa kuinasa saini ya nyota wa Lazio Sergej Milinkovic-Savic kwa dau la £95m, kwa mujibu wa The Express .
Kiungo huyo yumo kwenye rada za miamba wa Serie A Juventus, lakini Jose Mourinho amemfanya kuwa shabaha kuu kwa bodi ya Old Trafford.
 
Tetesi
MAN UTD YATENGA DAU KUMSAJILI ASENSIO


Manchester United itafanya mchakato kumsajili kiungo wa Real Madrid Marco Asensio dirisha la uhamisho la Januari baada ya kuachana na mpango wa kumsajili Gareth Bale, kwa mujibu wa Don Balon .
Mashetani Wekundu wanajiamini watafanikiwa kumsajili mchezaji huyo wa miaka 21 kwani ameshindwa kupata nafasi ya kudumu Santiago Bernabeu.
 
Tetesi
MAN UTD KUMUUZA SHAW & DARMIAN


Manchester United wapo tayari kusikiliza ofa kuwauza mabeki wao Luke Shaw na Matteo Darmian, kwa mujibu wa The Daily Record .
Shaw ambaye amesumbuliwa na majeraha amepewa nafasi kujiunga na klabu nyingi za Uingereza wakati Muitaliano Darmian hatakiwi kwenye kikosi cha Jose Mourinho.
United wanataka kutunisha mfuko wao ili kuwasajili beki wa kushoto Alex Sandro na Danny Rose majira ya baridi.
 
Tetesi
MAN UTD WANATAKA KUMSAJILI ALEX SANDRO


Jose Mourinho amemfanya Alex Sandro wa Juventus kuwa shabaha nambari moja kutua Manchester United kucheza nafasi ya beki wa kushoto kwa mujibu wa Daily Record .
 
City ndo bingwa wa epl ilo halipingiki ila tunafurahi kulikua na kauli kua hatujawahi fungwa uwanja wetu mara cc ndo tutamsimamisha huyu mtu mara sisi ndo tunagombea nae ubingwa hahahaaa jana mtt kalale kwa jilani na "fyatu" vyake

Hapo kuna utoafaut wa mashabik wa timu ndogo na kubwa nyie tayar mshasanda sisi hatujazoea kukata tamaa kama nyie mashabik wa vitimu vidigo bingwa hutangazwa may sio december Mpira ni bahat shukran ziende kwa striker wangu lukaku tu ila wale mliokuwa mkiwataja hawakuonekana pale.
 
Mourihno anakosa nn mpaka anakua na approach mbovu hv dhidi ya timu kubwa?
Alikuwa na kikosi finyu jana, Wachezaji wanne muhimu hawakuwa uwanjani, City ni timu nzuri lazima ucheze nayo kwa tahadhari, kufungwa ni matokeo na mpira ni mchezo wa makosa, ukiangalia jana tulicheza vizuri zaidi ila bahati haikuwa yetu.

City hawakucheza mpira wao, uliona dakika 10 za mwisho City ndio walicheza mpira wao.

All in All tunapokutana na timu kubwa kuna aina flan ya Wachezaji tunawakosa kuufanya Mfumo wetu kucheza, Hatuna winger wa uhakika zaidi ya Martial, timu haina mbadala wa Pogba.

Imagine tungekuwa na Perisic yule wa Inter kama namba 7, afu Martial 11 kati kukawa na Lukaku na Rashford.

Ule ndio Mpira wa Man United hata tulipokuwa na Ferguson tatizo tulikosa Wachezaji muhimu.


Sikuumia kwa kuwa tuliitendea haki Match.
 
Unajenga timu mwaka wa ngapi huu?Guardiola kaja lini? Unanunua wachezaji kwa record ya dunia unaishia kupaki basi!!

Pep hakuikuta city mbovu wewe Kdb,silva,aguero,company,fernandinho,sterling hao wanamsaidia sana yeye kanunua bek tu
 
Mimi Kabla Ya Ligi Kuanza Kama Utafatilia Comments Zangu Kwenye Uzi Wetu Basi Nilisema Kwa Kigenge Tulichonacho Hatuna Safari...
Na ilipoanza Ligi tu Nikajua Wazi Kuwa Man City Ndiyo Wenye Timu Ya Ushindani na Kuchukua Ubingwa
....

Na Nikajua Wazi Kuwa Man United Wana Timu Bora Kuliko Man City Lakini Nikajua Wazi Kuwa Mourinho Ni Obstacle Ya Man United Kuchukua Ubingwa
...

Nimekupata mkuu
 
Si kweli, hata Mourunho anasema hivyo ili kupata huruma kutoka kwa kwa watu kama nyinyi. Hivi kwa jana tulifanya nini kikubwa kinachoweza fanya sema city walishinda kibahati? Possession yenyewe ilikua United 25% na City 75%. Tulipiga mashuti mangapi golini, na tulitengeneza nafasi ngapi za wazi kulinganisha na wao hadi tuseme jamaa walikuwa na bahati? Mourinho anafeli kwa uoga wake halafu anasingizia bahati. Bahati tulikuwa nayo sisi tulipowafunga arsenal.
babu fegi alikua na timu ya kawaida sana ila ilikua inapambana hatari ila kuna baadhi ya mechi tulibebwa na bahati na si soka la uwanjani....hao city rejea mechi zao 2 za nyuma na soton na westham ndio utajua nini nachokiongelea
 
2011/2012 review
United then went on an eight-match winning streak to open up an eight-point gap at the top, but two defeats, including one courtesy of a Vincent Kompany header, against City, and a 4-4 draw against Everton left their rivals ahead on goal difference going into the final match.

Unajua kilichotokea

City took on QPR, still not safe from relegation, while United faced mid-table Sunderland. Wayne Rooney's goal gave United the win they needed and Djibril Cisse and Jamie Mackie cancelled out Pablo Zabaleta's opener at the Etihad Stadium to leave United on the brink of a 13th Premier League title.

Then, against 10-man QPR following Joey Barton's dismissal, Dzeko levelled in the 92nd minute and, with virtually the last kick of the match, Aguero's cool finish made City champions. Fans streamed on to the pitch as a historic first Premier League triumph was confirmed.

Katika football kila kitu kinawezekana...kama huamini waulize wazee wa kubeti....
na hawa jamaa kwa bahati tu wamejaliwa kwa kweli
 
FB_IMG_1512972842279.jpg
 
2011/2012 review
United then went on an eight-match winning streak to open up an eight-point gap at the top, but two defeats, including one courtesy of a Vincent Kompany header, against City, and a 4-4 draw against Everton left their rivals ahead on goal difference going into the final match.

Unajua kilichotokea

City took on QPR, still not safe from relegation, while United faced mid-table Sunderland. Wayne Rooney's goal gave United the win they needed and Djibril Cisse and Jamie Mackie cancelled out Pablo Zabaleta's opener at the Etihad Stadium to leave United on the brink of a 13th Premier League title.

Then, against 10-man QPR following Joey Barton's dismissal, Dzeko levelled in the 92nd minute and, with virtually the last kick of the match, Aguero's cool finish made City champions. Fans streamed on to the pitch as a historic first Premier League triumph was confirmed.

Katika football kila kitu kinawezekana...kama huamini waulize wazee wa kubeti....
hii ngoma mpaka christmas tulikua tunaongoza sie ligi lakini kilichokuja kutokea sasa kwanin usiseme ni bahati ilichangia kwa 100%
 
Tetesi
MAN UTD BADO WANAMTAKA PERISIC


Manchester United bado wanaitamani huduma ya Ivan Perisic baada ya kumkosa winga huyo wa Inter uhamisho wa majira ya joto, kwa mujibu wa The Sun .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Croatia alisaini mkataba mpya kubaki Italia, lakini mchakato huo ulifanyika kutunza thamani yake ila anaweza kupatikana Januari kwa dau la £45 milioni.
kwangu ni bora aje dyabala kulko huyo perisic
 
Back
Top Bottom