Camilo Cienfuegos
JF-Expert Member
- Apr 23, 2015
- 19,226
- 68,242
Nilichojifunza mechi ya leo dhidi ya Arsenal.
David De Gea kwasasa ndio kipa bora barani Ulaya sio tena EPL.
Toni Valencia anazidi kutakata licha ya umri kuendelea kusonga mbele, jamaa alistahili kitambaa cha unahodha, anaongoza kwa mfano.
Ashley Young ni kama amezaliwa upya. Kwasasa ni mtu muhimu katika safu ya ulinzi ya United.
Lingard licha ya kutokukubalika na mashabiki wengi wa United, ni mchezaji anayejua kutimiza vyema majukumu anayopewa na kocha.
Marcos Rojo awapo mzima, basi timu nayo inakuwa salama hasa kwenye mipira ya juu.
Na mwisho kabisa, Man United bado yupo kwenye mbio za Ubingwa, anakimbiza mwizi kimya kimya.
TUKUTANE Mwezi MAY!!!!
David De Gea kwasasa ndio kipa bora barani Ulaya sio tena EPL.
Toni Valencia anazidi kutakata licha ya umri kuendelea kusonga mbele, jamaa alistahili kitambaa cha unahodha, anaongoza kwa mfano.
Ashley Young ni kama amezaliwa upya. Kwasasa ni mtu muhimu katika safu ya ulinzi ya United.
Lingard licha ya kutokukubalika na mashabiki wengi wa United, ni mchezaji anayejua kutimiza vyema majukumu anayopewa na kocha.
Marcos Rojo awapo mzima, basi timu nayo inakuwa salama hasa kwenye mipira ya juu.
Na mwisho kabisa, Man United bado yupo kwenye mbio za Ubingwa, anakimbiza mwizi kimya kimya.
TUKUTANE Mwezi MAY!!!!

na tunapunga upepo pale juu. Niwatakie sare njema maana sijaona kikosi cha kuichapa aseno hapo.