Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

24294053_10155326817382746_5913608992196301565_n.jpg
 
Arsenal si timu ya kutosha, Nog acheze tu kawaida. Jaime maana aache kuimarisha defense.
 
Zlatan Ibrahimovic ameonyesha dalili njema ya kupona majeraha na kwa mujibu wa habari huenda akarejea dimbani Manchester United dhidi ya Arsenal
Straika wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic amepania kurejea dimbani Desemba 2 katika mechi dhidi ya Arsenal Ligi Kuu Uingereza.
Mkongwe huyo, 36, amekuwa nje ya dimba tangu Aprili akiwa anasumbuliwa na majeraha ya ligamenti, ambayo ilitarajiwa atakuwa nje mwaka wote huu.
Ibrahimovic ameonyesha maendeleo mazuri miezi ya hivi karibuni, pia maendeleo ya afya yake yameishawishi Man United kumpatia mkataba mpya hadi majira ya joto msimu ujao.
Kwa mujibu wa The Mirror, mchezaji huyo wa zamani wa kimataifa wa Sweden amerejea sasa kwenye uzima wake na ataanza mazoezi mwezi ujao.
Habari zinadai kuwa Jose Mourinho anatamani kuwa na supastaa huyo kwenye kikosi chake, mechi ratiba ikiwa inaendelea kuchanganya kwa mechi za Ligi na Ulaya.
 
Matokeo ya mechi yatategeme jinsi Manchester United wanavyocheza katika mechi hii ya Emirates
Jose Mourinho amekuwa na tabia ya kupaki basi kwenye mechi kubwa za ugenini, jambo linaloashiria mechi hii inaweza kuishia sare.
Licha ya hilo, ni vigumu kuona jinsi mechi hii itakavyomalizika bila magoli.
Moja ya mahasimu wakuu wa Ligi ya Uingereza watakwaana Jumamosi Arsenal watakapoikaribisha Manchester United katika uwanja wa Emirates.
Manchester United walishinda 4-2 dhidi ya Watford Jumanne usiku. Timu ya Mourinho wakienda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 3-0 shukrani kwa Anthony Martial na mabao mawili kutoka kwa Ashley Young.
Mabao ya kipindi cha pili kutoka kwa Troy Deeney na Abdoulaye Doucoure yaliipatia United utisho kabla ya Jesse Lingard kufunga goli la nne.
Arsenal wameshinda mechi saba Ligi Kuu Uingereza katika uwanja wao wa nyumbani msimu huu (kama walivyofanya Manchester United).
United wamepoteza mechi tatu kati ya tano za mwisho kwenye michuano yote ugenini.
Mbinu ya Mourinho kucheza kwa kujihami kumeifanya United kuondoka bila goli mechi za ugenini Liverpool na Chelsea.
Arsenal hawajaruhusu goli katika mechi zote sita ambazo Laurent Koscielny, Shkodran Mustafi na Nacho Monreal walianza kwa pamoja kwenye safu ya mabeki.
 
Manchester United habari za timu vs Arsenal

Marouane Fellaini yu shakani baada ya kupata majeraha ya goti. Kukosekana kwa Mbelgiji huyo kutaifanya United isiwe thabiti sana eneo la kiungo cha kati.
Nemanja Matic alilazimika kutoka kwa sababu ya majeraha ya misuli katikati ya wiki, lakini anaweza kuwa mchezoni. Michael Carrick hatakuwepo, wakati Paul Pogba amemaliza mechi yake ya pili mfululizo dakika 90 kwa mafanikio makubwa.
Mourinho alidokeza kuwa Anthony Martial anaweza kuwa na uchovu kutokana na kucheza mechi mfululizo.
Phil Jones atakuwa nje, wakati Eric Bailly akitarajiwa kurejea baada ya kusumbuliwa na majeraha ya paja.
 
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kuwa hatarajii kama Jose Mourinho atatumia mbinu za kujihami Man United watakaposafiri kwenda Emirates
Mashetani Wekundu wameshindwa kuifunga timu yoyote katika sita kuu kwenye mechi ya ugenini chini ya Mourinho katika matukio saba tangu achukue mikoba kuinoa timu hiyo mwaka jana, akiambulia sare tatu na kupoteza nne.
United pia wamefanikiwa kuweka kimiani goli moja katika mechi waliyofungwa 2-1 na Tottenham Hotspur miezi sita iliyopita - na walikosolwa hivi karibuni kwa mbinu walizotumia kwenye sare isiyo ya magoli dhidi ya Liverpool katika uwanja wa Anfield.
Wenger anaamini kuwa wageni wake watajaribu kutafuta mbinu kuongeza mashambulizi na kukaba pia katika mechi yao ya Jumamosi jioni, hata hivyo, aliwaambia waandishi: "Sitarajii jambo jipya [kiulinzi]. Man United ni timu imara na natarajia tutaweza kuyakabili matatizo watakayotusababishia.
"Watashambulia pia. Hawatakaba tu. Ni mechi baina ya Arsenal na Man United nyumbani kwetu. Nahitaji tu kujidhatiti na kuandaa vema timu yangu, na kuipa timu yangu nafasi nzuri kushinda mechi hiyo. Man United wanafanya vizuri kwa sasa, tunafanya vizuri pia kwa sasa, kwa hiyo inaonekana itakuwa mechi yenye mvuto."
Wenger, ambaye atamkosa mchezaji wake ghali zaidi Alexandre Lacazette dhidi ya United, amefanikiwa kukipandisha kikosi chake nafasi ya nne kufuatia ushindi wa mechi tatu mfululizo.
 
Mourinho leo akiingia na mambo yake ya kiogaoga Arsenal lazima watatutoa kamasi

Degea
Lindelof. Smalling. Rojo
Vncia,matic,pogba,young
Lingard Lukaku Martial

Kama matic hatokuwa fit herrera atamreplace.

Inabidi tuingie uwanjani kutafuta ushindi,sio kutafuta kutokufungwa, halafu tunakuja kuruhusu goli dakika za mwisho..
 
Back
Top Bottom