Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United ikiwa ugenini katika dimba la Vicarage Road imefanikiwa kuichapa Watford 4-2 katika ushindi ambao awali ulionekana kuwa mgumu kwa United kabla ya kuanza kwa mchezo.
Magoli ya United yamefungwa na Ashley Young akiingia nyavuni mara mbili huku Antony Martial akipachika goli la tatu na Jesse Lingard.
Troy Deeney na Doucaure walindika magoli mawili ya Watford.
Meneja wa Manchester United José Mourinho amesema ushindi huo utaongezaotisha kwa timu yake.

Man United inasalia nafasi ya pili ikiwa na alama 32 ikiwa ni alama tano nyuma ya Man City ambayo pia ina mchezo mmoja mkononi.
 
Haaa haaa mkuu ya kweli ayooo
skysports-romelu-lukaku-manchester-united-watford_4169092.jpg

The Belgian is currently without a boot sponsor, and appeared to colour over the Nike tick on his all-black boots on Tuesday, something Mourinho jokingly referred to after the game.
 
mara nyingine tusiingilie maamuzi ya kocha,tuangalie tu outcomes
Mkuu Ferrenga....

Mechi ya soka ukiondoa wachezaji 11 field, inachezwa na watu wengi sana...!!! Kocha, Shabiki mpaka wale Wachezesha na Wacheza kamari..!! Laiti kama mechi ingekuwa inashia kwa Mipango ya kocha pekee then hakuna timu ambayo ingekuwa inashindwa..!!!

Mimi kuja na challenge ile ninatimiza nafasi yangu ya "uchezaji" kama Shabiki na mpenzi wa Utd na soka kwa ujumla..... so usiwaze mkuu..!! Halafu sijaingilia mipango ya kocha ile ni observations kulingana na nilivyokiona kikosi, sijamshikia bunduki Mou kwamba ampange Mata au Herrera kama nilivyokuwa nikitamani.

Ujue nini mkuu....
Watu tumetofautina.. mimi huwa ninatoa challenge au kujiamini/kutojiamini pale tu ninapokiona kikosi so kuongea kabla ya mechi ni kawaida yangu tofauti na yule anayesubiri timu imeshindwa/imepigwa au imevoyanga ndo anaanza kushangilia/kulia au kupovuka..!!

So tujitahidi kuishi kadiri ya differences kama hizo.
 
Tunaingia kwenye kipindi kigumu cha msimu na hii ilikuwa moja ya mechi ngumu lakini tungeweza kushinda magoli mengi kuliko mechi zote msimu huu

Lindelof ni mchezaji mzuri na yuko comfortable kwenye mfumo wa kuchezesha 3 CB


Kiwango cha Ashley Young kuna possibility kubwa ya Luke Shaw kuuzwa January kabla mkataba wake haujaisha
Young is 32....Luke hawezi kuuzwa kwa sababu 32 yrs old r/l back amepata form nzuri.
 
Una chuki binafsi kwa Lingard na mapenzi binafdi na Mata, hisia zikiingia huwezi kuangalia kitu kiuhalisia. Usiku mwema.
Yap mkuu Rrondo..

Katika yote hayo uliyonukuu wewe umeishia kuiona chuki yangu kwa Lingard..!! Ama kwa hakika kuweza kumetofautiana kati ya mtu na mtu..!!

Ukiisha kufikia hitimisho la namna hiyo hauwezi kuviona vitu ktk uhalisia wake.. mechi za nyuma za Lingard na Mata zinathibitisha kile nilichokishema mimi awali... Mimi nilidhani unakuja kunipinga kwa hoja kwamba labda timu imecheza hivi na vile tofauti na nilivosema... matokeo yake we umeishia kuiona chuki yangu kwa Lingard.!!

Ni kweli timu imecheza kwa kuvizia kama nilivosema awali vilevile ni kweli Young amecheza nyuma zaidi kulinganisha na kiungo Haya yote we hujayaona mkuu isipokuwa chuki yangu kwa Lingard..!! Hapa lazima nikiri kwa jana Lingard amecheza vizuri kulinganisha na mechi zilizopita... na nikisema hivi bado haiondoi ukweli kwamba Lingard hana au bado hajafikia kiwango cha kumuweka benchi Mata.!!

Kumeshakucha mkuu, uwe na siku njema
 
Yap mkuu Rrondo..

Katika yote hayo uliyonukuu wewe umeishia kuiona chuki yangu kwa Lingard..!! Ama kwa hakika kuweza kumetofautiana kati ya mtu na mtu..!!

Ukiisha kufikia hitimisho la namna hiyo hauwezi kuviona vitu ktk uhalisia wake.. mechi za nyuma za Lingard na Mata zinathibitisha kile nilichokishema mimi awali... Mimi nilidhani unakuja kunipinga kwa hoja kwamba labda timu imecheza hivi na vile tofauti na nilivosema... matokeo yake we umeishia kuiona chuki yangu kwa Lingard.!!

Ni kweli timu imecheza kwa kuvizia kama nilivosema awali vilevile ni kweli Young amecheza nyuma zaidi kulinganisha na kiungo Haya yote we hujayaona mkuu isipokuwa chuki yangu kwa Lingard..!! Hapa lazima nikiri kwa jana Lingard amecheza vizuri kulinganisha na mechi zilizopita... na nikisema hivi bado haiondoi ukweli kwamba Lingard hana au bado hajafikia kiwango cha kumuweka benchi Mata.!!

Kumeshakucha mkuu, uwe na siku njema
Sina haja ya kupoteza muda to state the obvious.Ni kipofu tu ndio hawezi kuona alichofanya Lingard au akiingia huwa anafanya nini.
 
Brilliant Lingard's magic moment

Jesse Lingard scores some special goals. This one, to stop Watford's remarkable fightback in its tracks, will make his 'best of' montages, along with those wonderful Wembley strikes against Crystal Palace and Leicester.

With the momentum all with Watford and the home fans roaring their team forward in the final minutes as they searched for a third goal in a row to salvage an unlikely point, United needed to hit back. And Lingard delivered a devastating blow.
 
Btw Lingard replaced Rashford not Mata....

Jose Mourinho made two changes from the side that beat Brighton on Saturday; Lingard came in for Rashford, and United opted for an extra defender as Rojo replaced Mata. There was just the one change for the hosts as Prodl replaced Britos in defence.
 
Manchester United imefunga mabao nne huku Ashley Young akiwafanikiwa kufunga mawili ndani ya dakika 6 dhidi ya Watford .
Ushindi huu, unakuwa ni ushindi wa tatu mfululizo kwa United kwenye Ligi Kuu, wamepunguza gepu la pointi 5 dhidi ya wapinzani wao wakubwa, Manchester City ambaye baadae atavaana na Southampton.
Vijana wa Jose Mourinho ndiyo walikuwa wakwanza kupata goli kupitia kwa Ashley Young kwa shuti kali la nje ya 18 ambalo lilimshinda mlinda mlango wa Watford Heurelho Gomes.
Baada ya dakika tano baadaye, Young aliwainua tena United kwa kufunga goli la pili kwa adhabu ndogo . Nafasi hiyo ilipatikana baada ya Abdoulaye Doucoure kumfanyia madhambi Paulo Pogba kwa kumvuta shati.

Martial alifanikiwa kufunga goli la tatu akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Mbelgiji, Romelu Lukaku, na goli hilo linamfanya Mfaransa huyo kufikisha mabao 8 kwa msimu huu idadi hiyo ikiwa sawa na ilealiyofunga kwa msimu mzima wa 2016/17.
Young chupu chupu afunge magoli matatu katika dakika 45 za kipindi cha kwanza kufuatia Adrian Mariappa kumfanyia madhambi Martial katika eneo lile lile iliyopatikana faulo ya kwanza iliyozalisha goli, lakini safari hii mpira alioupiga uliishia kugonga ukuta wa Watford.
Manchester United wangeenda mapumziko na magoli 4 kama siyo ubora wa mlinda mlango wa Watford Gomes. Baada ya kufanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa Lukaku kisha Lingard kwa wakati huo huo.
 
Kabla ya kuelekea kwenye mapumziko Richarlison aligongesha mwamba baada ya kuunganisha mpira wa krosi uliochongwa na Kiko Femina.
Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinatimia, United walikuwa mbele kwa magoli matatu kwa bila
Kipindi cha pili kilianza kwa Watford kufanya mabadiliko kwa kumuingiza mshambuliaji Troy Deeney ambaye alifanikiwa kufunga goli la kwanza la wenyeji kwa adhabu ya penati baada ya Marcos Rojo kumuangusha chini Roberto Pereyra kwenye eneo la hatari.
Dakika chache baada ya kupata goli la kwanza, Watford walipata tena goli la pili kupitia kwa Doucoure akimalizia mpira ambao ulishindwa kuokolewa vyema na walinzi wa United, wakati wenyeji hao wakiwa na matumaini ya kusawazisha, Lingard alizima ndoto yao kufuatia kufanya juhudi binafsi za kuwatoka walinzi wa Watford kisha kuweka mpira nyavunia.

Zlatan Ibrahimovic dakika za mwishoni kuchuka nafasi ya Lingard na kufanya kuwa mchezo wa 50 kwa Msedeni huyo ndani ya United.
Vikosi vilivyoanza Watford: Gomes (c); Mariappa, Prodl (Carrillo 58), Kabasele; Femenia, Cleverly, Doucoure, Hughes, Zeegelaar; Huges (Pereyra 58), Richarlison; Gray (Deeney 72). United: De Gea; Valencia (c), Lindelof, Smalling, Rojo, Young; Matic (Herrera 54), Pogba; Lingard (Ibrahimovic 88), Lukaku, Martial (Rashford 65).
 
Back
Top Bottom