Pogba, Zlatan, Kurejea..!
Jose Mourinho amekaribisha mapumziko ya mechi za kimataifa na ameweka wazi wachezaji wawili wa Manchester United Paul Pogba na Zlatan Ibrahimovic wapo katika " nafasi nzuri "
Pogba na kiungo mwenzake Michael Carrick wamekuwa majeruhi tangu mwezi Septemba huku wachezaji majeruhi wa muda mrefu Ibrahimovic na Marcos Rojo bado hawajarejea dimbani.
Kikosi cha Mourinho kinaelekea mapumziko ya mechi za kimataifa baada ya kichapo cha 1-0 kutoka kwa Chelsea na kuwa nyuma ya pointi ya 8 dhidi ya vinara Manchester City , lakini kocha huyo ametoa taarifa chanya kuhusu wachezaji waliokuwa majeruhi.
" Tuna kundi la wachezaji ambao tuna matumaini kwamba watapona haraka iwezekanavyo."
"Lazima wafanye mazoezi kwa juhudi kila siku lakini sasa hivi wapo kwenye nafasi nzuri. Pogba, Ibrahimovic, Rojo, Fellaini."
" Wapo kwenye nafasi nzuri kwahiyo nafikiri kwamba tunaelekea katika hii sehemu ya msimu , kipindi cha Christmas na baada ya hapo tukiwa katika nafasi imara kwa maana ya kikosi."
Katika kipindi cha mwezi Desemba ambapo kuna na mechi nyingi za kucheza kocha wa United Mourinho ana matumaini kwamba wachezaji wake waliobaki ambao hawatokuwa katika mechi za kirafiki za mwezi huu watakuwa wamepata muda mzuri wa kupumzika.
" Wachezaji wengine wote wa kimataifa wameondoka na tumebakiwa na wengine wachache .. kama [Chris] Smalling na [Ander] Herrera na kiukweli wanastahili baada ya kucheza mechi nyingi wiki ya kupumzika ambayo nitawapa." Amesema Mourinho.