Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

109e54ac7bbfe515feed411981b5efb2.jpg
Ongera Man u mwendo wa dozii....

Kidogo tu kilichoonekana...



...... Walichokikosa Everton ni Romero Lukaku wao tu kumalizia kazi nzuri ya kikundi cha viungo( Davies, Sirgudson, Gana na Shneiderlin). Bado Wayne Rooney mchezo huu ulimhitaji kucheza kama second streker zaidi kutokana na aina yake ya uchezaji.

Baada ya ule mguu wa Valencia kwenda moja kwa moja ndani ya nyavu za Jordan Pickford. Na kabla ya Everton kuutawala mchezo eneo la kiungo katika mchezo huu. Romero Lukaku alishindwa kuweka mipira miwili ya wazi kwenye nyavu za Jordan Pickford. Pamoja na ubora wa Lukaku kwa hivi sasa lakini bado anatatizo la kuzitumia vizuri nafasi zote zinazopatikana, na katika mchezo huu nafasi mbili za wazi akibaki yeye na kipa alishindwa kuzitumia.

Kipindi cha kwanza mchezo ulikuwa chini ya ulinzi wa Manchester United, Nemanja Matic na Marouane Fellaini waliwafanya viungo wa Everton kukubali kuwa wageni pale OT. Maumbile ya viungo hawa wawili wa Manchester united yalifanikiwa kuwatisha viungo wa Everton na kumfanya Rooney kushuka chini na kuongeza nguvu katika eneo la kiungo.

Baada ya kuanza kwa kipindi cha pili hapo ndipo Ilikuja Everton mpya tofauti na ile ya first half. Half time team talk iliwasaidia sana vijana wa Ronald Koeman.... Idrissa Gana, Tom Davies, Morgan shneiderlin na Glyf Sirgudson pamoja na ongezeko la Wayne Rooney katika eneo hilo la kiungo, kuiliwafanya Manchester united kupoteana katikati mwa uwanja na kuukabidhi mcheo wote kwa Everton. Kama sio umahiri wa Davide De Gea basi hesabu za Everton zingekuwa bora katika wakati ule wa umiliki wa mchezo. Pengine pia ni pamoja na kupungua kwa umakini wa Nahodha wa zamani wa mashetani wekundu hao Wayne Rooney, ndiko kuliko sababisha kushindwa kwake kupeleka mipira miwili ya wazi mbele ya de gea.

Baada ya Ronald Koeman kuona amefanikiwa kuufanya mchezo kuwa mgumu, na sasa akaamua kuingiza watu wa kufunguka ili kusawazisha goli. Kumtoa Wayne Rooney mtu aliyekuwa ameongeza wingi wa watu katika eneo la kiungo ilikuwa ni nafuu kwa united. Lakini pia kumtoa Idrissa Gana pamoja na Tom Davies wanadamu ambao waliwafanya viungo wa Manchester united kupoteza mipira muda mwingi na kuwaingiza Kelvin mirales, Calvert Lewin na Sandro Ramirez watu ambao wanakwenda na plan mpya ya kufunguka kutoka katika mpango kazi wa awali wa kulizima eneo la kiungo lote.
Bado tunatakiwa kumuombe Mtalii wa Tanzania Ronald Koeman kuendelea kuishi pale ili Msimu ujao aje tena katika utalii.
Huu ndio ule Msimu wa kuvuna ulichopandaa....
 
Kuna match alikosa penalt, sasa naona atakuwa kaingia woga.
Hakukosa bhana ila refa alikosea mana kipa aliwahi kutoka katika mstari kabla ya kipyenga kupulizwa,Ila uzuri wa kocha wetu hatabirki we angalia hata sub alizofanya hakuna hata shabik1 aliyetarajia mana kwenye maziwa ye katia Nazi ya bakhresa na kwenye Alma's katia vioo
 
Manchester United-Kings of Late Goals

manchester-united-premier-league-anthony-martial-romelu-lukaku-goals-stat_4103697.jpg


To put that statistic into context, Manchester City are the only other Premier League team to score more than nine goals in total so far this season. Defending champions Chelsea have scored eight, Arsenal and Tottenham each have seven. In other words, United have been more deadly in 15 minutes than many of their rivals have been in 90.
 
Lukaku alizomewa sana jana,Amenifurahisha alivyoanza kushangilia kabla yay goli (penati ya Martial).
Mashabiki walikuwa sahihi.

Lukaku anakosa nafasi nyingi sana mwanzoni mwa mchezo, kabla ya ku-assist na kufunga goli.

Leo nilikuwa namsikiliza Jose mourinho.Anasema hivi

" timu ilipoteza nafasi nyingi mwanzoni, baada ya kipindi cha kwanza nilitegemea kutoka sare ya 1-1 na everton"

"Lakini kipindi cha pili timu ilibadilika na mimi nikaona tunaweza kushinda 2" .

"Goli la 3 na la 4 ni magoli ya bahati, sikutegemea magoli hayo na kwangu sio ya msingi sana. Yale mawili yaishatosha"

Hahaaa! Jose bhanaa..
 
Mashabiki walikuwa sahihi.

Lukaku anakosa nafasi nyingi sana mwanzoni mwa mchezo, kabla ya ku-assist na kufunga goli.

Leo nilikuwa namsikiliza Jose mourinho.Anasema hivi

" timu ilipoteza nafasi nyingi mwanzoni, baada ya kipindi cha kwanza nilitegemea kutoka sare ya 1-1 na everton"

"Lakini kipindi cha pili timu ilibadilika na mimi nikaona tunaweza kushinda 2" .

"Goli la 3 na la 4 ni magoli ya bahati, sikutegemea magoli hayo na kwangu sio ya msingi sana. Yale mawili yaishatosha"

Hahaaa! Jose bhanaa..
Sure pamoja na kwamba alizngua nimemsifu kwa kujiposition sehem zenye bahati.
 
Pamoja na ushindi wa jana...binafsi bado sijaelewa Mourinho alitumia upeo upi kumuingiza Lingard ahead of Martial na baadae kumpatia Martial dakika 6 tu za kumalizia mchezo...ndio, Martial alibahatika kupata goli,lakini je ilikua sawa kumpatia nafasi finyu kiasi kile ukizingatia uwezo wake?
 
Pamoja na ushindi wa jana...binafsi bado sijaelewa Mourinho alitumia upeo upi kumuingiza Lingard ahead of Martial na baadae kumpatia Martial dakika 6 tu za kumalizia mchezo...ndio, Martial alibahatika kupata goli,lakini je ilikua sawa kumpatia nafasi finyu kiasi kile ukizingatia uwezo wake?

Martial ni mchezaji mzur lakin bado hajaipata fom yake vizur anaweza kuanza akazingua balaa sisi tunahangaika upande wa mshumbuliaj wa kushoto rashford ni nutural striker sina lawama nae anajitahidi sana.
 
Pamoja na ushindi wa jana...binafsi bado sijaelewa Mourinho alitumia upeo upi kumuingiza Lingard ahead of Martial na baadae kumpatia Martial dakika 6 tu za kumalizia mchezo...ndio, Martial alibahatika kupata goli,lakini je ilikua sawa kumpatia nafasi finyu kiasi kile ukizingatia uwezo wake?
Mashabiki wengi walikuwa hawamwelewi Mourinho kwa nini anampanga Fellaini leo wamekaa kimya wanamsifia Fellaini huenda kuna siku utaelewa na kumsifia kocha kumchezesha Lingard.Martial ana kipaji sana lakini ndio mchezaji mwenye workrate ndogo sana pale United

Last season sikumuelewa kwa nini Mourinho alikuwa anampiga benchi Mikhitaryan lakini kwa sasa namwelewa hata akiwa hayuko kwenye form anapambana kuanzia dakika ya kwanza hadi ya mwisho. Kila mchezaji ana strength & weakness zake na kuna faida kubwa ya kuwa na wachezaji wenye uchezaji wa aina tofauti
 
Back
Top Bottom