Nimeangalia match kati yetu na Real Madrid na nimeona chambuzi nzuri humu na Mkuu@ubarnGentleman umeongea vema hasa ulipowazungumzia Lingard,Matial na Matta.
Kwa kifupi, tumecheza na kufungwa na timu bora kwa sasa ulimwenguni, Madrid wamekamilika kila idara.
Sababu kubwa ya kufungwa kwetu ni timu kukosa uzoefu, Kikosi chetu ndio tunakiunda kufikia ubora wa Madrid, wachezaji wetu wanahitaji kucheza pamoja kwa misimu mitatu au zaidi kuwa na ubora wa 99's
Kulikuwa na mapungufu makubwa Sana kwenye eneo la Beki yetu pengo la Baily na Rojo lilionekana dhahiri kabisa, nilionesha wasiwasi wangu katika eneo hili mapema.
Lakini kama wengi wetu tulivyotegemea tumeona kuimarika kwa eneo la kiungo, Matic ameongeza kitu katika eneo la kiungo, Chelsea nadhani sasa wanajutia juu ya maamuzi yao. Jamaa amepiga mpira mwingi mno basi tu kazi yake imeshindwa kunogeshwa na Pogba
Kazi nzuri kwa Matic, De gea, Fellain, Lukaku,Rashford,Herera na Valecia wameonesha kitu even Darmian
Lakini nasikitishwa na uwezo wa Pogba bado kuna shida kama tutaendelea kuipanga timu kwa kumuangalia Pogba, pamoja na gharama ya fedha alizonunuliwa Pogba anatakiwa kudhihirisha ubora na uwezo wake ndani ya Man U kama anataka kuwa mfalme wa Oldtraford, bado ana deni kwa mashabiki wa Man united.
Kwa kiasi kikubwa kufungwa kwetu kulitokana na poor performnce kutoka kwake, alishindwa kudrive timu katika eneo la mbele, akawapa kazi kubwa akina Herera, Lingard, Mikh na Lukaku.
Sasa nakubaliana na wengi humu kuna umuhimu wa kusajiliwa kwa Winger @Perisic kwa ajili ya kudrive timu
Ama tuanze kuwaamini Martial na Matta katika wingi ya kushoto na kulia.
Ni rahisi kocha kuipata first eleven kwa Madrid lakini ni ngumu kwa sasa kupata first eleven kwa urahisi kwa Man United, hasa eneo la kiungo kama Pogba hatobadlika.
Tunahitaji Match zaidi ya 10 - 15 kujua kikosi chetu cha kwanza.
Tuone mabadiliko ya kikosi chetu leo tukicheza na West ham.
Sent using
Jamii Forums mobile app