Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Screenshot_2017-08-10-08-19-01.png
 
Wachezaji wetu sijui wamekuwaje, ukiangalia kikosi alichochukua nacho ubingwa Ferguson mara ya mwisho na hiki alichonacho Mou hiki cha mou kina wachezaji wanaoonekana wazuri zaidi..

Ona kitu kama hiki.. Sijui ni hawaonani au ni nini View attachment 562023
Pogba hapo alizingua sana asee alitaka kufanya kama martial ila akashindwa hadi kutolewa mpira.
 
Hayo ni masihara zaidi. Hivi mbona Mourinho anabadili utamaduni wa Man U wa 'hakuna mchezaji Mkubwa kuliko klabu'? Zlatan alikuwa hivyo kule PSG, sasa naona hilo linataka kuja kwetu. Klabu ishatangaza kumuacha lakini inampa option ya kusaini tena au kuondoka manake nini, kwa kipi alichonacho yule mzee? Kiukweli naamini Ibra wa Jana c Ibra wa Leo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unakumbuka vizuri vipengele vya mkataba wake kwani!!!!?
Kama ndio usingesema hayo
 
Borussia Dortmund reject Barcelona bid for Dembele

5 minutes ago / autty

Borussia Dortmund have confirmed that they have rejected an offer from Barcelona for Ousmane Dembele.

"Borussia Dortmund has held talks with the Catalan football club FC Barcelona regarding the possible transfer of the BVB player Ousmane Dembele to FC Barcelona," a statement read.

"During this meeting, the representatives of FC Barcelona submitted a bid which did not correspond to the player's extraordinary footballing and other status and not to the present economic market situation of the European transfer market. BVB therefore rejected this offer.

"As there is no other offer from FC Barcelona to date, there is currently no transfer of the player to FC Barcelona and this is not currently likely."
 
faida kubwa ya jamiiforums ni kwamba kila member ana uhuru wa kutoa mawazo yake bila ya kubughudhiwa ila nimesikitishwa na baadhi ya mawazo ya wachangiaji.
Inasikitisha kuona baadhi ya wadau wa manchester united kumdharau mourinho na kufika mtu kusema mourinho ni mwalimu mbovu na hafai kuwepo manchester.
Tunasahau ya kwamba ni mourinho ndiye aliyeileta fc Porto kwenye ramani ya soka la ulaya na aliifunga manchester united kwenye robo final mwaka 2004.
Tunasahau ya kwamba ni mourinho ndiye aliyeipa mafanikio makubwa Chelsea na kuipa utambulisho kwenye soka la ushindani duniani.
Tunasahau ya kwamba ni mourinho ndiye aliyerudisha soka la ushindani nchini italy na kuipa mafanikio Inter Milan iliyoundwa na wachezaji wa kawaida kama cambiasso,lucio,stankovic n.k
Ni mourinho huyu huyu tena ndiye aliyekwenda kuondoa utawala wa wasio shindika wa guardiola isala nchini hispania na haya mafanikio ya ancelloti na zidane ni msingi uliojengwa na mourinho. Kumtukana mourinho kwa sababu anampenda Lingard ni makosa makubwa kwa mtazamo wangu kwa sababu lingard hakupandishwa timu kubwa na mourinho ila yeye alimkuta tu.
Wakati moyes anarithi nafasi ya big boss aliamua kumtoa lingard kwa mkopo na baada ya kufanya vizuri van gaal aliamua kumrudisha kwenye kikosi na nakumbuka mechi ya kwanza ya ligi dhidi ya swansea lingard alianza kikosi cha kwanza(3 -5-2)na bahati mbaya aliumia na akakaa nje kipindi kirefu.
Msimu wa pili wa van gaal aliwauza van persie,dimaria,kagawa,rafael n.k lakini alishindwa kumuuza lingard na aliendelea kumpa nafasi lakini hatukulalamika.
Kwanini awe mourinho wa kulaumiwa?
Siamini kama tumefungwa kwa sababu ya lingard ila naamini tulifungwa kwa sababu tulishindwa kumdhibiti Isco alacron ambaye ndiye mchezaji bora wa real madrid kwa miezi sita amekuwa kwenye ubora.
Kama mourinho aliweza kusikia kilio changu na akafanikiwa kutafuta dawa ya eden hazard basi naamini jose mourinho ataitafuta dawa ya kutibu ugonjwa hatari wa Isco.
Kama mourinho aliweza kutafuta dawa ya kutibu ugonjwa hatari wa xavi na iniesta na mimi naamini jose atafanikiwa kutafuta chanjo ya kutibu ugonjwa hatari wa Isco mwanadamu aliyewafanya juventus kipindi cha pili waonekane kama walikunywa togwa kwenye final ya uefa.
Kwa mpira niliouona jana kipindi cha pili mimi ningependelea kwenye ligi kuu tunapocheza na timu kama west ham tusitumie viungo watatu kwa sababu kasi yetu inakuwa ni ndogo sana na pia huwa hatutengenezi nafasi nyingi.
Kati ya pogba au herrera kwa mtazamo wangu mechi ya ligi kuu mmoja wapo anapaswa akae benchi ili mbele tuweke utatu mtakatifu (mkhitaryan +mata+martial) utakaomuwezesha lukaku kufunga mabao 3 na nitafurahi kama mourinho atakuwa na mawazo kama yangu.
Nitoe shukrani zangu za dhati kwa uongozi mzima wa chelsea kwa kukubali kupokea million 40 kwa ajili ya mauzo ya Matic ila kwenye kipengele cha mauzo walishindwa kuweka kipengele cha kutaka tuwalipe kila mechi atakayocheza matic na hili ni kosa kubwa sana kwa sababu matic ana uwezo wa kucheza hadi miaka 40 bila ya kuchoka.
Pia nimkumbushe muafrika mwenzangu ngolo kante ajiandae kisaikolojia kurudisha ile tunzo ya mchezaji bora wa ligi kuu na wala hapaswi kuipeleka FA ila anatakiwa amkabidhi fundi Mkhitryan kabla ya jumamosi hata kama ligi haijaanza, njia pekee ya kumzuia mkhitaryan asibebe tunzo msimu huu ni kumkata mguu wake.
Mimi naamini kwa timu yetu ilivyo hata kama tutakuwa kundi moja na timu kama real madrid, munich na psg basi sisi tutatokea nafasi ya pili na nafsi ya kwanza watajuwana wenyewe kwa sababu tuna mwalim anayejua kuzitumia mechi mbili za home and away na ndio maana msimu uliopita niliamini timu ilihitaji zaidi kombe la europa kuliko nafasi ya nne japo mashabiki wengi waliamini bado ni mapema.
majirani zetu wenye kelele waanze kujiandaa kisaikolojia kabla ya jumamosi haijafika.
chelsea,arsenal,liverpool hawa wote ni majirani zetu na si wapinzani kama wanavyojidai kwa sababu thamani ya manchester united unaweza kuzinunua timu mbili unazozipenda kati ya chelsea,man city,liverpool na arsenal

Mkuu agiza kinywaji nakuja kulipa.
 
Umeanza vizur ukamalizia na pumba.. matic n kiungo mzito sana.... kama hujui... yupo slow.. na anachoka haraka especially second half... team ikiwa inashambuliwa matic huwa anapotea.. kama ulimfuatilia vizur Chelsea ngolo kante aliteseka sana pind akicheza na matic.. I stand to be corrected...

Sent using Jamii Forums mobile app

Labda ni uko Chelsea lakini juzi alionyesha ni kwanini alisajiliwa. Alionyesha uwezo wa hali ya juu wa kuzuia na kupeleka mashambulizi kwa mda wa dakika 97 bila ya kuchoka.
Uyu ndie Matic ninaemfahamu tokea january 2014, uyo wa kwako sijui ni wa wapi?
 
Matic n kiungo mzito ndiyo..... mfuatilie vizur mkuuu.. huwez compare mtu kama bakayoko na matic... yoko yupo faster sema nahis injuries sana

Sent using Jamii Forums mobile app

Nina hakika ujawai kuangalia zaidi ya mechi 4 ambazo Bakayoko amecheza.

Conte: "Bakayoko is a good signing for us. He's young. My idea was to give him the right time to adapt in this league behind Matic."
 
Labda ni uko Chelsea lakini juzi alionyesha ni kwanini alisajiliwa. Alionyesha uwezo wa hali ya juu wa kuzuia na kupeleka mashambulizi kwa mda wa dakika 97 bila ya kuchoka.
Uyu ndie Matic ninaemfahamu tokea january 2014, uyo wa kwako sijui ni wa wapi?
Kaka unatoa vp judgment kwa game moja ya juzi tu....?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nina hakika ujawai kuangalia zaidi ya mechi 4 ambazo Bakayoko amecheza.

Conte: "Bakayoko is a good signing for us. He's young. My idea was to give him the right time to adapt in this league behind Matic."
Wakati mwingine nikukaa kimya tu kubishana na Shabiki wa Chelsea..wengi wao wameanza juzi kutazama kandanda.


Conte mwenyewe anakili wamefanya makosa makubwa kumuacha matic.
 
Back
Top Bottom