Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

glazer inabidi mtuachie timu yetu inunuliwe na waarabu sasa....... rejea matusi ya PSG

sent from my iphone 7 nimeinunua SAPNA pale POSTA
 
Kuna kitu hamjui jamani msimlaumu RUTA ule uzi ni zaidi ya cocain ukiingia kule lazma uwe addicted mimi ni mmoja wa walioshinda addiction ya ule uzi kwahiyo itamchukua muda bwana RUTA kurudi huku😀
Ninichokizungumza nadhani hata kisu cha ngariba ni shahidi.
 
Nakubaliana na Maelezo ya Mourihno,Our Pre season imekuwa nzuri kwa timu safari hii,kiasi flan tumeona uwezo wa timu,wachezaji,we'r happy kwa kweli.

Nitajaribu kuchambua wachezaji wachache kutokana na muda kwenye hii Pre season.

Tuanze na waliosajiliwa:-

1.Lukaku,kama alivyotegemewa na wengi hakutuangusha,magoli mawili akizifunga timu kubwa tu duniani,shoot on goal 3 na off goal Zaidi ya mashuti 5 katika match zisizozidi tano,tunahitaji nini Zaidi kutoka kwake.

Moto utawaka EPL ikianza,jana katika match na Sampdoria pamoja kuwa hakufunga lakini alionesha kitu katika eneo la mbele akiwa peke yake.

Maoni yangu katika Ushambuliaji,tunahitaji kusajili mshambuliaji mmoja Zaidi kutokana na mashindano tutakayoshiriki na kadri tutakavyofanya vizuri,ili kuwe na rotation nzuri kwa washambuliaji wetu.

Katika 10,Lukaku nampa 8 katika hii Pre season.

2.Leondorf,nimemuona katika match chache za hii Pre season, mwanzoni alikuwa na mapungufu kutokana na ugeni katika kikosi na kucheza katika timu yenye jina na mashabiki wengi Duniani,lakini ameendelea kuimarika kadri muda unavyoenda,Lendorf ni mzuri kwa kuzuia mipira ya Juu,tuendelee kumuamini na tutegemee mabadiliko makubwa kutoka kwake,itapendeza Zaidi kama akicheza na Baily,nampa 6 kati ya 10.

3.Matic,match yake ya jana ndio ilikuwa ya kwanza akiwa na uzi wa Man United,kama ilivyokawaida yake amepiga mpira Mwingi sana katika dimba la chini eneo la kiungo,ameonesha kitu,ameonesha uwahi mpya kwenye timu katika ya Washambuliaji,viungo washambuliaji na mabeki, sasa timu imepata holding midfield wa uhakika,hii inawapa uhuru Viungo wa Ushambuliaji kushambulia Zaidi na hata mabeki wa pembeni kupanda kusaidia kushambulia,tunahitaji nini Zaidi Zaidi ya kutuwezesha kutwaa makombe,Chelsea wametupa Zawadi tuliyostahili.

Kwa match moja tu aliyocheza nampa 8/10.

Kwa wachezaji waliopo kwa Uchache! !

1. Martial, akitoka kwenye matatizo ya kifamilia/kimahusiano,msimu mbaya wa mwaka jana,Martial ameonesha mabadiliko makubwa katika hii Pre season na akiendelea hivi hamna haja ya kusajili winger,assist mbili na tamu za magoli,Dribble za uhakika,uwezo wa kuwakata mabeki Zaidi ya wanne kwa kujiamini tena katika match na timu kubwa kama Man City,Madrid,Barcelona.
Sina shaka na Martial kinachohitajika kwa sasa ni kuamini wa tu na Kocha na kupewa majukumu kamili ya winger moja tupate raha kutoka Katika kipaji hichi,kwangu nampa 8/10.

2. Rashford,Patners hip anayojabu kuitengeneza Mou ni ya utatu pale mbele,Rashford,Lukaku na Mikhityran,nimeshamuelezea Lukaku,kwa kifupi,Rashford ameendelea kuonyesha uwezo wake katika eneo la Ushambuliaji,katika hii Pre season naweza sema amejihakikisha kuwa mshambuliaji wa pili baada ya Lukaku,mabadiliko makubwa katika umilikaji wa mpira,uwezo wa kufunga na pasi za uhakika zinanifanya nimpe 8/10 huyu mtoto kutoka pale Mfenesini Zanzibar.

3. Mikhityran, bado kuna kitu nasubiri kukiona kutoka kwa huyu Fundi wa mpira,naona bado ana vingi Zaidi ya hivi anavyotuonesha,uwezo wa kufunga,kupanga mashambulizi na kumiliki mpira humfanya Mou kutojutia kumsajili,huyu jamaa ni Fundi haswaa huwa namfananisha na Hazard,tutegemee makubwa Zaidi kutoka kwake,kuna kipindi huwa najiuliza kwa nini Mou hana mpango wa kusajili mshambuliaji mwingine?jibu ni kwa sababu ya uwepo wa Mikhityran,Mikh ana uwezo wa kucheza namba zote katika eneo la Ushambuliaji,7,8,9,10 na 11.

Kwa sasa anasogea kutoka eneo la kiungo mshambuliaji na kwenda eneo la Ushambuliaji kamili akiwa sasa na Rashford na Lukaku,tumeona akicheza hivi katika hii Pre season.

Kwangu nampatia 9/10.

Stay tuned sehemu ya pili..tukianza na eneo la Viungo. (Pogba,Pereira,Matta na Herera)



Sent Using Sumsung S6 Edge
Bwanaa tumalizie shughuliiiiiii tule vtu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mata hajawahi shindwa mfumo wa kocha yeyote duniani. Hapa raia wengi hawamzungumziii kabisa ila Mata anapokuwa uwanjani moyo wangu huwa unatulia sana na matokeo huwa yanabadilika muda wowote. Jamaa anapass za akili $190bn. So msimu huu jamaa akimtumia vema mbele ya Kong Lukaku ni balaaaaa. Martial dah yule dogooo,sema mapenzi tuu ila kijana mpira anaujua.
 
Mata hajawahi shindwa mfumo wa kocha yeyote duniani. Hapa raia wengi hawamzungumziii kabisa ila Mata anapokuwa uwanjani moyo wangu huwa unatulia sana na matokeo huwa yanabadilika muda wowote. Jamaa anapass za akili $190bn. So msimu huu jamaa akimtumia vema mbele ya Kong Lukaku ni balaaaaa. Martial dah yule dogooo,sema mapenzi tuu ila kijana mpira anaujua.
Kweli kabisa mkuu..umeongea facts..ila mou hao wote uliowataja naona msimu huu hawatakuwa kwenye first eleven yake..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Personally sioni kama kuna haja ya kusajili left wing kwa sasa yani sioni kabisa!! Uwepo martial/rashfod/miky unatosha kabisa!! martial jana kaonyesha kiwango sana jaman!!


Kuna Haja Mkuu Martial Na Rashford Bado Wadogo Sana Wanahitaj Kupewa Changamoto Na Kujifunza Perisic Ni Muhimu Sana Watu Wanapiga Kelele Umri Wake Pale Hatakiwi Tena Mtu Chini Ya Miaka 28 Ili Wakina Martial Wasije Kupotea
 
Kuna Haja Mkuu Martial Na Rashford Bado Wadogo Sana Wanahitaj Kupewa Changamoto Na Kujifunza Perisic Ni Muhimu Sana Watu Wanapiga Kelele Umri Wake Pale Hatakiwi Tena Mtu Chini Ya Miaka 28 Ili Wakina Martial Wasije Kupotea

Lakini si akina miky wapo??

Uko sahihi mkuu ila kusema ni wadogo bado unakosea maana akina messi ...ronaldo...rooney... hata rashford mwaka jana walipewa nafasi na tukaona ujuzi wao!!

Bado sioni haja ya jamaa, maana tuna kiungo tayari kaja, beki yupo, na tuna lukaku!! nadhani tuache kwanza!! kama wakizingua ndio tuangalie dirisha lijalo!!
 
Kuna Haja Mkuu Martial Na Rashford Bado Wadogo Sana Wanahitaj Kupewa Changamoto Na Kujifunza Perisic Ni Muhimu Sana Watu Wanapiga Kelele Umri Wake Pale Hatakiwi Tena Mtu Chini Ya Miaka 28 Ili Wakina Martial Wasije Kupotea

Hapana kijana. Martial ni mtu mzima tena sana tuu kwenye soka. Katoka Monaco na goal kama 18 hivi. Kaja Man U akiwa bado hajazoea ligi kapga magoli kama 18 tena. Msimu ulioisha japohakuwa chaguo sana kapiga 4. Martial huwa haogopi beki ni kama Rashford tuu. Anavocheza ni kama De Lima anaifata beki ilipo. Anageuza kwa namna yoyote. Perisic umri mkubwa hafu chenga yake moja. Martial akipewa game mfululizo lazima akuue tuu. Ni kama Rashford on target 3 goal 1. Yaan pale hatutakiwi kutafta winger ingine. Wako wengi sana. Martial na Rashford big match zote pale EPL waliuua. Lingard yuko pale. Ndomaana Mou kaamua kulizika na usajili wa watatu kwanza. Martial uku Rashford kule Lukaku uko Miki/Mata hapo waraiiiiiii ni ushindii tuuu.
 
9b6d1dee88d6e88f9318b76f2dfb1303.jpg

Tumemaliza vizuri.
Hivi EPL inaanza lini wakuu?
[HASHTAG]#GGMU[/HASHTAG]

Sent using Jamii Forums mobile app
naona mood iko juu.
 
Yaah! uhali gani bibie?cute b tunae humu ila weye ulijichimbia sana umekuwa adimu humu.
nipo aiseee, kwasas sionekani sana ila nipo ligi ikianza ndiyo nitakuwepo zaidi. afadhali cute b karudi mana nae akifichwa anafichwa haswaaa.

mrembo mwingine shabiki damu wa Man Utd nae kapotea, sijui anamsaidia Mou kwenye mambo ya usajili.
 
nipo aiseee, kwasas sionekani sana ila nipo ligi ikianza ndiyo nitakuwepo zaidi. afadhali cute b karudi mana nae akifichwa anafichwa haswaaa.

mrembo mwingine shabiki damu wa Man Utd nae kapotea, sijui anamsaidia Mou kwenye mambo ya usajili.
Yule kweli kitambo itabidi atafutwe aje tujumuike msimu utakuwa mzuri sana kwetu huu
 
Back
Top Bottom