Mkuu umeandika kweli tupu, kama ningekuwa mou Rooney angecheza nafasi ya ibra na kwasababu naamini Rooney ni mtu wa kulazimisha na pia ningemlazimisha asizunguke uwanja mzima.. Rooney anatabia ya kuzunguka uwanjani muda wote akikaba na kutafuta mipira,sasa hii inamchosha na kumfanya asiwepo kwenye nafasi yake!
Kinachonifanya nisimkubali ibra japo ametusaidia sana ni vile hana uwezo wa kupambana na mabeki akikabwa kidogo anaachia mpira na wala haangaiki kuutafuta.. Rooney ni mpambanaji na hakubali kushindwa kizembe.
Hili la bastian me hata mou simuelewi maana alimpanga na akaonesha mpira wa maana sijui kwanini hampangi tena!
Timu nzima inamtegemea Zlatan afunge,sijui ni mou amewaambia ni lazima afunge ibra?