Wala uhitaji kuwa rocket scientist kuelewa kwamba dynamic football ndiyo staili na filosofi ya #ManUnited
Wachezaji wakicheza kwa uhuru kama leo, ushindi unapatikana kwa asilimia kubwa.
Mata yeye ni namba 10 bana, kumweka kwenye right wing ni kumwonea. Leo kaonyesha ni kivipi alivyo mmoja ya creative players with brains. Martial, Monaco inabidi waombe pesa zaidi.
Wazza is on fire, is it 7on 7 or 7 on 8?!? Naona mzee Bobby kiroho kinamdunda tu. Na naamini Wazza sasa anawaza rekodi ya Shearer.
Dogo CBJ, ananifurahisha sana. Anakimbia kama mzembe fulani, lakini shughuli yake baba, ni balaa. Inabidi Shaw akirudi akaze kweli, maana dogo anakipiga kwelikweli.
Wanasema ng'ombe hazeeki maini. Hivyo ndivyo ilivyo kwa pass master mwenyewe, Carrick. Jamaa akiwepo bana, forward passes ndizo zinatawala. Herrera anaweza kuziba pengo, lakini inabidi ajifunze zaidi kutoka kwa Carrick.
DDG Save leo alikuwa likizo kabisa.
Timu imecheza kitimu na kwa kujiamini sana leo. Hiyo ni muhimu ili tukienda darajani, Rent Boys viroho viwadunde.
Hivi hawa Leicester wapo serious kweli?! Loh! Maana wamemtoa nishai mtu mzima leo. Halafu nafikiri watakutana na United karibu na mwisho wa ligi. Yaweza kuwa decisive game kwa timu zote, huwezi jua.
#TutafikaTu