Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,382
- 10,951
Rooney best perfomance yake imekwisha hata lile goli ni kama kashfa kwake tu...rvp na chicharito lazma tuwamiss tu
Baada ya game ya jana nimeona ManUnited tunahitaji sana striker namba 9,Rooney ameshasahau kabisa kucheza striker.Kwenye defence tumecheza vizuri hasa (Romero,Darmian na Smalling) tunahitaji sana striker kuliko beki (Rojo,Blind) wanaweza kucheza na Smalling tuombee tusipate majeruhi.Kwa sasa bila striker ningependa kila game Herrera aanze sababu huyu ni kiungo anayefunga magoli,Ashley Young aanze benchi
Umeona vyema mkuu.
Ila usidharau umuhimu wa kupata na beki mzuri ili tuwe safe side zaidi.
Tuna michuano mingi msimu huu, we can't afford kuwa na majeruhi, itatugharimu.
Kila michuano tuliopo ni muhimu zaidi.
Striker na CB ni muhimu sana sana.
Tuongeze striker mwingine na tuanze kumtumia Chicharito.
Rooney amezoea misimu iliyopita alivyokuwa anacheza nafasi nyingi.
Wakuu, mmenena vyema kabisa.
Rooney kazoea sana kucheza dimba lote. Sasa akiwa hivyo, hawezi kumudu namba 9.
Pia LvG naona bado anataka kurudia makosa ya kupanga wachezaji kwenye nafasi zisizo zao kiufundi. Mimi sijui kwanini Depay ameletwa halafu anapangwa pale kati! Kwa kuja kwake, Young inabidi awe squad player sasa. Depay akipige pembeni kule, halafu Herrera awe kama AM mwenye kupeleka mipira kwa striker, Mata anakuwa huru kucheza kwenye wings na kumsaidia AM wakati wowote. Mata na Herrera wanakuwa nyuma ya Rooney, huku Morgan/Blind na Carrick/Bastian wakiwapa support ya kutoa mipira nyuma na kusukuma mbele.
Naamini ukiwa na viungo design ya Mata na Herrera, unaweka striker mmoja tu mbele pale. Anaanza Rooney na Chicharito anaingia kama sub saa zingine, wakibadilishana na madogo Wilson na Lingard kwenye mechi zenye uelekeo wa ushindi.
Herrera atakuwa akibadilishana na Fellaini/Perreira, huku Mata akibadilishana na Januzaj/Valencia, Januzaj naye anaweza kuwa huru, lakini siyo Valencia. Depay atabadilishana na Young.
Beki Rojo na Smalling wanakaa kama CBs, wakibadilishana CB mpya na Jones, huku Darmian akiwa RB na Shaw kama LB, madogo Blackett na McNair wakiwa kama subs za RB na LB.
Mimi naona kama hitaji kubwa kwa sasa ni CB mzoefu mmoja wa kuongoza timu hapo kwenye backline. Striker anahitajika ndiyo, lakini kwa mfumo huo niliousema hapo juu, ukiwa na Mata na Herrera nyuma ya Rooney/Chicharito au wale madogo, naamini hakutakuwa na shida sana.
Hivyo formation ambayo ningependa itumike ni 4-5-1 yaani:
Backline
CBs: Rojo/CB mpya, Smalling/Jones
LB: Shaw/Blackett
RB: Darmian/McNair
Midfield
CMs: Morgan/Blind na Carrick/Bastian
AM: Herrera/Fellaini/Perreira
Wingers: Depay/Young na Mata/Valencia/Januzaj.
Forward
Striker: Rooney/Chicharito/Wilson/Lingard
Haya ni mawazo yangu kama mpenzi wa #ManUnited ila kocha naye ana ya kwake kama mtu anayewaona wachezaji mazoezini, na kupanga timu.
Ila naamini mambo yatakuwa siyo mabaya msimu huu.