lonewolf ranger
JF-Expert Member
- Feb 22, 2013
- 476
- 149
Sometime we can b champs
GGMU
GGMU
Ikawa usiku ikawa mchana hatimae maneno yako part 1 yakatimia tusubiri part 2 sasa, hureeee!!!!!City jtatu wanafungwa na sisi tutawatuliza
Tarehe 18 huna chako darajani!
Hahahahahahahahaaaaaaaa tutakomaa na nyinyi hadi kieleweke. Hapo uswahiba pembeni, utatusamehe tu.
kitwala wala usijali Mkuu! Huu uswahiba hauzuii kurushiana tambo za hapa na pale ndio kwanza story zinanoga!
Nyie mkija darajani ni halali yetu lazima tuwapige kwasababu mchezo wenu na Wa Arsenal ni michezo ambayo itatuhakikishia kuchukua kombe hivyo basi tutaipa umuhimu mkubwa sn kuhahikisha hatupotezi kitu ambacho tunaweza!
Nyie malizaneni kwanza na City hivi karibuni then niwaalike wote ktk Uzi wetu kule turushiane tambo!
Tutarushiana hapa hapa, safari hii jambia linakuhusu .....lol
Lile jambia mmefanikisha kulipitisha kwa Spurs, LFC, Aston Villa na tarehe 12 mnatakiwa kulinoa kweli vinginevyo mtashindwa kumchinja Man City.
Hachomoki ,anaanzaje kuchomoka kwa kikosi kile? Kazi anayo....... Aiseee kama hizo 3 tumevuka salama hata za mbele yetu tutavuka salama, nikikumbuka humu mlivyokuwa mnatutisha na ratiba kwamba ni Ngumu kwetu nacheeeka sana, kweli Mungu si Athumani tumechomoa na tutachomoa tena na tena.........
Hahahaha!! Sasa kama unafunga na kikosi kiko atleast si mbaya kwanini usiwe na confidence, tena unazurura hadi kwa majirani kifua mbele, au na nyie hamjioni mlivyo na kelele mnasumbua ile mbaya.
Sikatai kiukweli utakuwa mchezo mgumu sana kwetu na tukiangalia historia wana record nzuri juu yetu lakini pamoja na yote game hiyo tunachomoa labda LVG avuruge kwenye kupanga karata zake
Aiseee RVP hapana aiseeee tunamshuru kwa kazi nzuri aliyotufanyia muda wote na abarikiwe, ila kwa mechi hizi kubwa zilizobaki naomba LVG asimpange kabisaa,avumilie tu hilo benchi aiseee!!!!
RvP bado yuko vzr sn sema Ashley Young na Mata wamekua wanafanya vzr sn hivi karibuni. Kwahiyo hawa wanaweza wakapangwa!
Msiwe na hofu mna kila sababu ya kufanya vzr huo mchezo mkizingatia mtakua OT sehemu yenu ya kujidai na kuchinjia watu!
Duh! Ila mimi maombi yangu kwenye hizi mechi kubwa asipangwe.Van persie aneungana na wenzake kwenye mazoezi
Kimahesabu tukimbutua Shitty jumapili atabaki akifukuza point 4, hivyo tutabaki tukimpigia mahesabu Gunners ambaye anajifanya gari lake kaweka petrol ya kutosha. Hebu jumapili njoo haraka ili mawazo yetu yahamie tarehe 18 april.
Duh! Ila mimi maombi yangu kwenye hizi mechi kubwa asipangwe.
Halafu gazeti la Daily Mirror limesema kwamba LVG yupo tayari kumuuza RVP na kumleta Cavan wa PSG. Kamchina kamegoma kuweka link, wadau mnalizungumziaje hili? Je Cavan ni chaguo sahihi kwetu?
Cc Nzi DonDonald kitwala RRONDO mfarisayo na #MUFC fans wote.
Cavan ni mchakalikaji mzuri sana uwanjani ila siyo goal scorer wa kuogopwa sana ktk dunia ya leo.
Akitua OT siyo vibaya ataongeza kachumbali na kuwafanya mabeki wa timu pinzani wasipande.