Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu King faisal kuanzia Edesron, Santos na hata huyu Kone ni panic buys kama ilivyo kawaida yetu. Hakuna mfuatiliaji yeyote wa EPL alikuwa haoni gap la Man Utd kwenye kiungo ila inaonekana hatukufanya maandalizi ya machaguo yanayoendana na uhitaji pamoja na gharama.

Msimu wake uliofuata Amorin aliainisha targets zake na akazipata cheaply na kwa wakati sahihi. Ila sasa naona kama tumerudi kwenye defaulty ya ile Man Utd ya akina OLE ya kuletewa yeyote anayepatikana.

Maana yake wanamfanyie Kone scouting kwenye hizi game za WC tena akiwa amezungukwa na world class players wa ufaransa
Ni kweli unachosema mkuu.
 
Surprise Surprise MF....... 🚐

Screenshot_20260713-144430 (1).jpg
 
Surprise Surprise MF....... 🚐

View attachment 3628117
Ile sababu kwamba tunasajili wachezaji wanaoipenda timu pamoja na kuangalia thamani halisi ya soko inaonekana ni utapeli mtupu. Huyu dogo katoka Leicester kaenda Villa lakini sikuona interest toka klabu nyingine kubwa zaidi ya Utd leo hii baada ya kukosa targets zake.

We are officially a mid table team kama usajili wa Tielemans toka Villa unatufurahisha hivi.
 
Daaah! mkuu upo chap yaani nataka niilete hii habar nakuta umeiweka. Safi san hii kazi nzuri ineos wapo serious. Huyu mwamba atatupa magoli mengi sana nadhani ni moja ya udajili bora sana utd wanafanya. Huyu ni mtu wa kazi kweli kweli.
Mkuu christeve88 kwani Tielemans na Santos wanakaribiana uwezo na Baleba, Wharton, Anderson au hata Tchounamen?
Binafsi naona usajili huu kama tunakimbizana na muda zaidi
 
Mkuu christeve88 kwani Tielemans na Santos wanakaribiana uwezo na Baleba, Wharton, Anderson au hata Tchounamen?
Binafsi naona usajili huu kama tunakimbizana na muda zaidi
Mkuu frankly speaking kwa uchezaji wa utd Tielemans atatufaa sana nadhani kuliko hata hao uliowataja. Huyu bwana ni very aggressive hasa anapolikaribia goli na anauwezo wa kukupa goli kadhaa nje ya majukumu yake uwanjani. Ni mtu mwenye maamuzi sahihi wakati sahihi namaanisha anaweza kukupa suprise nyingi uwanjani na kukupa magoli aina ya Lampard, Scholes au Gerad. Wachezaji kama hawa ni muhimu sana hasa pale njia za kupata magoli zinapokuwa zimefungwa. Huyu mwamba atatufaa.

Mimi sifurahi sana wachezaji wa bei ghali au wanaopambwa sana kuja utd, asilimia kubwa ya watu kama hao walifeli. Mfano Pogba, Falcao, Lukaku, De Maria, Anthony na wengine wengi. Watu kama kina Bruno, Mbuemo na Cuhna hawakuj kwa mbwembwe lakin ona dhughuli zao.
 
Surprise Surprise MF....... 🚐

View attachment 3628117
NtYga hapa sio kina fabrizio na ornstein tu, hadi ma content creator. Pia wameshitushwa kwa jinsi ineos, walivyofanya haraka na upesi kukamilisha dili hili. Bila kuwa na tetesi zozote, mie naona huu ni usajili mzuri sana. Maana Youri tielemans anao uzoefu na EPL, ijapokua hana jina kubwa, kama akina Eliot Anderson,sandro tonali na mateus Fernandes. Lakini jamaa anajua sana.
 
Daaah! mkuu upo chap yaani nataka niilete hii habar nakuta umeiweka. Safi san hii kazi nzuri ineos wapo serious. Huyu mwamba atatupa magoli mengi sana nadhani ni moja ya udajili bora sana utd wanafanya. Huyu ni mtu wa kazi kweli kweli.
Kweli kabisa mkuu mie nimeanza kuwaelewa ineos kwamba wanafocus sana na future ya united.
 
Ile sababu kwamba tunasajili wachezaji wanaoipenda timu pamoja na kuangalia thamani halisi ya soko inaonekana ni utapeli mtupu. Huyu dogo katoka Leicester kaenda Villa lakini sikuona interest toka klabu nyingine kubwa zaidi ya Utd leo hii baada ya kukosa targets zake.

We are officially a mid table team kama usajili wa Tielemans toka Villa unatufurahisha hivi.
fuentte unachosema ni sawa Tielemans, hana jina kubwa lakini sio sababu ya kusema, sio mchezaji mzuri. Kisa hakuna timu nyingine zilizotaka kumchukua, lakini ujue pia hizi sajili za sasa, zimekua pia za kipuuzi sana. Wachezaji wanauzwa kwa pesa kubwa sana, ambayo haiendani kabisa na uwezo wao(akiflop na kushindwa kudelivery hii hasara club mnaibeba wenyewe).Hili suala limetusumbua sana, hasa kipindi cha Ed Woodward. Pia sajili ni kamali, united imekosa target zake muhimu kulingana na falsafa mbalimbali wanazotumia ineos kama:
1:mchezaji kuwa na mapenzi kwa united
2:mchezaji kukubali mshahara isiyo mikubwa
3:mchezaji kuwa na msimamo wa kuja united. N.k

Kosa walilofanya ineos, ni kwenye target yao muhimu, ambayo ilikua ni mateus Fernandes. Kumbuka huyu kashuka daraja na club mbili, Southampton na westham. Hapa united walikua sawa kabisa, kukataa kutoa £85m na mshahara wa £250k kwa wiki. Lakini walichonikela sana, ni kuendelea kumfukuzia mchezaji huyu mda mrefu. wakati ukiacha mateus, kutokua na msimamo thabiti, wa kuja united pia haku meet falsafa wanazotumia ineos kusajili mchezaji. Real Madrid, iliwahi pia kumtaka Mateus Fernandes, chini ya meneja wao mpya Jose Mourinho.

Nafikiria sababu iliyowafanya wao kumpotezea, waliona mateus Fernandes hana thamani hiyo, wanayoitaka westham. Ndiyo tukabakia sisi pekee yetu, kwenye race. Akatokea Tottenham spurs, ambae almanusura nae ashuke daraja. Akatoa hiyo pesa na huo mshahara na hii ni panick buy waliokua wanaitaka westham. Kuhusu elliot Anderson yeye aliweka wazi kwenda Manchester city. Hivyo sioni kosa la united kutemana nae mapema sana. kuhusu Aurelian tchouamen alikua target ya muhimu sana ya united na ineos walikua tayari kutoa £77m hadi £80m. Lakini Madrid wakaamua kumbakisha bila kusahau tchouamen bado alikua na mapenzi ya kubakia Madrid napia asingekubali kushusha mshara kilahisi licha ya kuwa na miaka 26. Hivyo bado mie naona united wako sawa hofu niliyonayo ni kwa huyu andrey Santos maana Chelsea huwa wanatupiga sana.
 
Ile sababu kwamba tunasajili wachezaji wanaoipenda timu pamoja na kuangalia thamani halisi ya soko inaonekana ni utapeli mtupu. Huyu dogo katoka Leicester kaenda Villa lakini sikuona interest toka klabu nyingine kubwa zaidi ya Utd leo hii baada ya kukosa targets zake.

We are officially a mid table team kama usajili wa Tielemans toka Villa unatufurahisha hivi.
Bado sielewi kwanini Baleba hatui tofali choma yani sielewi kwanini.

They are out of options mzee inawabidi wajaze mapengo tu mwisho wa siku next window waseme pesa walitumia dirisha hili 😎.
 
King faisal fuente NtYga
Sio kwamba united hatukuwa na target no.
target ilikuw ni viungo watatu haswa EPL proven, mpaka sasa kama tutampata baleba au DM mwingine tutakuwa tumefanikiwa kweny kujenga au build up ya kiungo kama tulivyofanya msimu uliopita kweny attacking phase
United ya sasa imegundua kujenga team sio kutumia hela nying, kama ambavyo alifanya man city, Liverpool, arsenal, psg, barcelona etc wote hawa ukifatilia wakati wanajenga team hawakufanya sajili kubwa au kutoa mshahara mkubwa.

Watuletee baleba, na ikibidi walete na Summerville yule left winger hapo team itakuwa na balance na itakuwa umeongeza thamani ya kushindana uwanjani na timu yoyote katika mashindano yote.
 
Back
Top Bottom