View attachment 3625439
Ningeshangaa sana kama ningemuona Tchouamen katua OT baada ya kukubari Paycut kwenye mshahara wake hivi kweli unawezaje kujifikilia hata kwa Dakika mbili umpunguzie mshahara Tchouamen anayepokea 210k kwa wiki huku tunae mchezaji fara tu kama Mason Mount anachukua £250k per week hata kama ni wewe ungeweza?..? Kwa ushawishi gani tuliokuwa nao Man u?..? kwa Kombe gani kubwa tulilobeba Recently?..? ety ni Target yetu sema shida ni moja kataki kupunguza mshahara wake yani kwa mafanikio yapi tulopata mpaka Bwana mdogo atoke zake Real Madrid aje kutua Man u ambapo huko atokako kila mechi anacheza hawa INEOS mtakuja kuniambia tu wako na shida sana yani hata kama ange Demand wage ya £245k wangetoa tu.
Sasa hivi wameleta Andrey Santos dogo tokea Benchi bila aibu wanamleta kwa Pauni £50m na muda huo kuna mtu kama Bruno G anathamani ya £65m -£60m hivi hizi ni akili kweli?..?
Na kuna interview moja nimeiona Boss mwembamba Jimmy akiporomosha nondo akidai kuwa Toka astaafu Ferguson kumekuwa na matumizi mabaya sana kwenye usajiri na kuliletwa watu ambao hata hawakufaa kuchezea Man united mfano Fred lakini naona Andrey huenda nae akawa Fred ajae,mie nachoka ndugu yenu na hii Timu.