Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Tonali anaenda spurs,scott bado haieleweki man u wanachungulia pochi, baleba amedrop man u, hawawezi kubet, yule dogo wa moroko, na ile mido madrid ndo karata ya mwisho ya utd otherwise wasahau kushindania ubingwa wa epl.
Tonali ameshaenda spurs tayari, united hawakua seriously kumchukua. Tchouamen wasahau kabisa hata huyo bouaddi nae wasahau unafikiri madrid na lile hawataki hizo £100m.
 
United naona wameandaa kiwango Fulani cha pesa kwaajili ya wachezaji Fulani, there is no way united ingetoa kiasi kile cha pesa Kwa Fernandez then mchezaji alisema timu itakayo kuwa na dau kubwa basi ndo atakwenda hiyo hiyo hapo united ndo wakakimbia kabisa maana mchezaji hajui anataka kucheza timu gani...Naona wako na Falsafa ya kuwa mchezaji utake kucheza timu yetu Kwanza halafu mambo ya pesa ndio yanafuata na sio kuweka fees kama kipaumbele, nowadays soko limeharibika Sana...
 
NtYga fuentte Mr Mike ze-dudu mateus Fernandes to Tottenham, here we go pound £85m waliyokua wanaitaka westham, with no adds on. pia mchezaji kulipwa pound £250k kwa wiki na pesa nyingine ya usajili pamoja na wakala wake. Sina mengi ila uongozi wa manunited, wanazingua sana. Leo siku nzima walikua wanafanya contact kwa mchezaji na wakala wake, ili iweje sasa. Nakama walikua hawataki,kutoa hiyo hela si wangemwacha tu.

Hapa ndio nimejua Ruben amorim, alikua sahihi kuhusu wamiliki wa united. Mchezaji hana msimamo, yeye anasema ataenda popote iwe man united au Tottenham. Na bado uongozi unaendelea kumshawishi, ni bora wangemtema kitambo tukaepusha hii dharau. Kama lengo ni baleba si wangesema tu. Dah ijapokua mateus Fernandes hana hiyo thamani lakini haikustahili tumpoteze kwa Tottenham ambaye alikua anaenda kushuka daraja.
Bora hata ingekua club nyingine kama psg au real Madrid.

NtYga fuentte Mr Mike ze-dudu mateus Fernandes to Tottenham, here we go pound £85m waliyokua wanaitaka westham, with no adds on. pia mchezaji kulipwa pound £250k kwa wiki na pesa nyingine ya usajili pamoja na wakala wake. Sina mengi ila uongozi wa manunited, wanazingua sana. Leo siku nzima walikua wanafanya contact kwa mchezaji na wakala wake, ili iweje sasa. Nakama walikua hawataki,kutoa hiyo hela si wangemwacha tu.

Hapa ndio nimejua Ruben amorim, alikua sahihi kuhusu wamiliki wa united. Mchezaji hana msimamo, yeye anasema ataenda popote iwe man united au Tottenham. Na bado uongozi unaendelea kumshawishi, ni bora wangemtema kitambo tukaepusha hii dharau. Kama lengo ni baleba si wangesema tu. Dah ijapokua mateus Fernandes hana hiyo thamani lakini haikustahili tumpoteze kwa Tottenham ambaye alikua anaenda kushuka daraja.
Bora hata ingekua club nyingine kama psg au real Madrid.
Kwa EPL, tuliwahitaji sana wachezaji wa pale pale katika ujenzi wa Msingi imara wa timu hasa idara ya Kiungo..

Tayari tumekosea..sijui Mpango ni upi..

Niliwaona
Tanguy Ndombele
Timeoe Bakayoko
Thomas Lema
Wakiwa Monaco, wa moto sanaa..

Mmoja akaenda Spurs
Wa pili Chelsea na
Wa mwisho Atletico..

Hawakuwahi kuwa wale wa Monaco Tena..

Benardo na Fabinho ni Exceptionals, Walienda timu ambazo zimeshakomaa, walimu Bora pia..

Hivyo, tulipaswa tusajili watu wa pale pale..

Na sasa Spurs wanamchukua na Tonali..

Wanataka kufanya nini Hawa Jamaa?
 
Ugarte ameumia
Casemiro ameondoka

Tumebaki na Mainoo + Bruno

Wamiliki wameshindwa kutoa 85 kwa Tonali ama Matheus, sasa watasajili nani?

Alex Scott jamaa wanataka 90
Tchoumeni 75 - 80
Baleba upepo ulishakata

Baadae Carrick aungushiwe zigo la lawama, tushukuru msimu jana Amorim alikua na ushawawishi kwa wachezaji tukawapata akina Cunha, Sesko, Mbeumo
Mimi si mtabili😂😂😂
Ila kuwakosa hao jamaa wawili tayari gari imeyumba sana..

Tumeishi misimu minne ya kuwaombea njaa Arsenal.. mwisho wa siku wamebeba ubingwa😂

Maumivu ni makali sana kwa kweli
 
Hii club itatuua kwa msongo wa mawazo siku moja mkuu King faisal .
Man Utd inataka kuonekana kuwa ni klabu kubwa ila inataka kusajili kwa gharama za klabu ndogo. Ni sawa na mwanamke aliyekuwa na mvuto mbele ya wanaume ila baada ya muda kwenda bado anataka kutambulika kwa sifa zake za awali badala ya kuukubali ukweli na kubadilika kuendana na mazingira halisi.

Kwa sasa wachezaji hawaangalii legacy ya klabu ila mustakabali wa maisha yao. Sikatai kwamba jamaa wanataka kununua wachezaji kwa thamani yao halisi sokoni ila tukubali kuwa lazima tutumie pesa zaidi ili kurudisha ushindani uwanjani na mambo ya mvuto yatafuata mbele ya safari. Tuchague target zetu kwa usahihi ila suala la kumwaga pesa kwenye soko la usajili halikwepeki kwa sasa.
Ukweli katika maisha, chochote kizuri huwa kina gharama zake..hakuna namna ya kupata mchezaji mzuri kwa pesa za kibahili.. haiwezekani...awe kinda ama aliye komaa,, mchezaji mzuri unampata kwa pesa nzuri..

INEOS hii itikadi Yao itawafukuzisha kazi watu wengi sanaa,,

By the way, Berrada yeye sio kama Mawaziri wakuu wa UK?😂 Fasta tu wao Wana achia kiti..
Miaka hiyo ya redio nimemsikia sana Tony Blair, Kisha nani nani Gordon na baadae Cameroon..baada ya hapo ni miezi tu mtu anaachia kiti
 
Kama eneo la kiungo limeonyesha uhitaji wa wazi kabisa lakini bado tunajibana kutoa hela, beki wa pembeni si ndio itatakiwa tumuombee Dalot apandishe kiwango msimu ujao!
Sina Maarifa mengi katika Soka, ila Nina amini Msingi wa timu imara na Bora yeyote unaanzia kwenye Kiungo..

Kama hapa wataleta mzaha(ambao tayari wameufanya) basi tutangoja sana..

Nimeishuudia Chelsea ya kwanza ya Jose Mourinho..(Lampard, Essien, Ballack, Obi, Makelele) wengine wamenitoka, hii timu hata ile Barcelona ya Deco, Gaucho na Eto'o wakipata shida mno..

Kuna Arsenal ya Mzee Wenger, miaka flani Alexander Song alichanganya, Fabregas, Ramsey, Wilshare, Nasri, walikuwa moto sana..

Vipi Barcelona ya Sergio, Xavi na Iniesta?😂😂umefanya tuichukie sio tu Barcelona, Bali Jimbo Zina la Catalonia..

Pep Guadiola, timu zake zote huwa anaimarisha Kiungo na ubunifu kutokea pembeni..

Sasa sisi tunaleta mzaha?
Tujipe muda tuone itakuwaje hiyo September
 
Ndio najua Bournemouth wamesema hawamuzi lakini ikitokea ofa nzuri kuanzia £80m plus wanaweza kumuuza hata huyo tonali bila £100m humpati. Hata Tchouamen amsahau maana hawezi kushusha mshahara na pia Madrid watataka pesa kubwa zaidi ikitokea France 🇫🇷 kabeba world cup.
Tchouamen, huyu ni design ya wapambanaji anaowapenda kocha mzalendo The Special One..😁😁
Ataruhusu aondoke? Labda tu iwe iliamuliwa baada ya tukio la kugombana na Fede
 
United naona wameandaa kiwango Fulani cha pesa kwaajili ya wachezaji Fulani, there is no way united ingetoa kiasi kile cha pesa Kwa Fernandez then mchezaji alisema timu itakayo kuwa na dau kubwa basi ndo atakwenda hiyo hiyo hapo united ndo wakakimbia kabisa maana mchezaji hajui anataka kucheza timu gani...Naona wako na Falsafa ya kuwa mchezaji utake kucheza timu yetu Kwanza halafu mambo ya pesa ndio yanafuata na sio kuweka fees kama kipaumbele, nowadays soko limeharibika Sana...
Unachosema ni uKweli kabisa, mchezaji kashuka daraja akiwa na Southampton na westham. Haoneshi msima wa kuja united bado hajaitwa kombe la dunia kuichezea ureno kwanini utoe £85m. Hivyo kupitia kwa omar berrada ngoja tuone kama hii falsafa yao ya usajili itaisaidia united.
 
Kwa EPL, tuliwahitaji sana wachezaji wa pale pale katika ujenzi wa Msingi imara wa timu hasa idara ya Kiungo..

Tayari tumekosea..sijui Mpango ni upi..

Niliwaona
Tanguy Ndombele
Timeoe Bakayoko
Thomas Lema
Wakiwa Monaco, wa moto sanaa..

Mmoja akaenda Spurs
Wa pili Chelsea na
Wa mwisho Atletico..

Hawakuwahi kuwa wale wa Monaco Tena..

Benardo na Fabinho ni Exceptionals, Walienda timu ambazo zimeshakomaa, walimu Bora pia..

Hivyo, tulipaswa tusajili watu wa pale pale..

Na sasa Spurs wanamchukua na Tonali..

Wanataka kufanya nini Hawa Jamaa?
Huenda wameona wawe seriously si unakumbuka kauli za Diego conte na mourhino kuhusu uongozi wa Tottenham hasa kipindi cha levy.
 
Huenda wameona wawe seriously si unakumbuka kauli za Diego conte na mourhino kuhusu uongozi wa Tottenham hasa kipindi cha levy.
Wamenishangaza sana Spurs..

Muuzaji kugeuka kuwa mnunuzi wa Bei mbaya..
Nawatakia Kheri..

Soko limeshaharibika sasa..sijui sasa tetesi zinaelekea wapi..
 
Tchouamen, huyu ni design ya wapambanaji anaowapenda kocha mzalendo The Special One..😁😁
Ataruhusu aondoke? Labda tu iwe iliamuliwa baada ya tukio la kugombana na Fede
Huenda hii ndiyo sababu mojawapo, lakini tujiulize France akibeba world cup madrid watamuuza je vipi likitokea battle la club nyingine kubwa Manchester United wataweza kushinda na kumchukua Tchouamen hapo bado mshahara wake na kwa kauli za omar berrada sizani kama watatoa £100m plus so bado giza ni nene sana kwa Manchester United.
 
Mateus kaniuma ila Tonali kaniuma zaidi...
Heartbreak kama hii nilishawahi ipata kwa Demu wa Kwanza kabisa nilimpata Form 3 akaniacha niko Form 4 karibu na NECTA naona maumivu yana shabihiana kabisa kudadeq 😂, nilikuwa nimemkasilikia Fernandes kabla sijamsamehe Tonali kaingilia kati hizi siku mbili naishi kwa Taaaaaaabu sana ndugu zangu tuombeeane uzima tu ila msimu ujao Man u bila kunituliza na kikombe chechote aisee..... watakuwa wamenyonga kabisa.
 
Heartbreak kama hii nilishawahi ipata kwa Demu wa Kwanza kabisa nilimpata Form 3 akaniacha niko Form 4 karibu na NECTA naona maumivu yana shabihiana kabisa kudadeq 😂, nilikuwa nimemkasilikia Fernandes kabla sijamsamehe Tonali kaingilia kati hizi siku mbili naishi kwa Taaaaaaabu sana ndugu zangu tuombeeane uzima tu ila msimu ujao Man u bila kunituliza na kikombe chechote aisee..... watakuwa wamenyonga kabisa.
Hii timu itakuja kutumaliza mapema kwa shinikizo la damu.
 
Kuna fan wa utd ametoa mawazo kwamba, ikiwa Mbeumo, Sesko na Cunha wanalipwa 150k-180k kwa wiki na wamepambana hadi timu imerudi champions league itakuaje Matheus na Tonali wagekuja na kulipwa 200k- 250k?

Hii ingeleta shida dressing room kama ilivokua kwa Pogba na Sanchez! Nimejaribu kumuelewa hoja yake.
 
Heartbreak kama hii nilishawahi ipata kwa Demu wa Kwanza kabisa nilimpata Form 3 akaniacha niko Form 4 karibu na NECTA naona maumivu yana shabihiana kabisa kudadeq 😂, nilikuwa nimemkasilikia Fernandes kabla sijamsamehe Tonali kaingilia kati hizi siku mbili naishi kwa Taaaaaaabu sana ndugu zangu tuombeeane uzima tu ila msimu ujao Man u bila kunituliza na kikombe chechote aisee..... watakuwa wamenyonga kabisa.
Pole sana Mkuu..lakini kitu kimoja Nina Imani nacho, Manchester United ipo karibu kurejea.. timu zote Zina Anza upya kujipanga
 
Naskia Kuna mchezaji wa Brazil kasajiliwa United lkn toka world cup ianze sjaona akipewa hata dkk 😆😆
inamaana tuliesajali anauwezo mdogo had anazidiwa na babu casemiro? Au guameres

Kazi ipo
 
Back
Top Bottom