Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mkuu NtYga kawapige nacho arsenal maana wanamuona Saka kama second to MESSI hivi, Na vile wamebeba ndoo huwezi kubishana nao bila mabandiko kama haya ukawashinda
Hakuna kitu sipendi kama kubishana na mtu asiye na Facts kuna muda mpaka walimdhihaki Bruno Fernandes kwa kumlinganisha na Odegard ety Odegard Kiungo mchambuko, Lakini Game ya Juzi nilikuwa na Mwana Arsenal akakili kutoka moyoni kwamba "Kusema kweli hii Game ilimhitaji Bruno Fernandes"
 
Ila jamani amorin kuna kitu amekifanya, hata Carrick ameivusha timu kutokana na kuundo wa amorin.

Kwanza kuwaondoa wavivu na kuleta wapiganaji. Carrick anapaswa ajue anatembelea muundo wa amorin..kosa lake amorin kungangania mfumo mmoja
Ilikuwa hivyo Pia kwa Thomas Tuchel kuchukua Ligi Ya Mabingwa Ulaya kupitia Sajiri za Lampard.
 
Kuna sajiri hapa zilihitajika kabisa "ILIMAN NIAYE waje wapiganie nafasi na Matheus Cunha" Pia huyu "MALICK DIOF huyu Dogo kazi yake Jamani mnaijua Dogo anamwaga maji mpaka kero, hawa wote watue kwa ajiri ya squad depth.

sema kuna kitu huwa nakiona United wachezaji weusi huwa hawapewi attention kwenye usajiri ndio maana hata Deal ya Baleba wanazunguka zunguka tu ila angekuwa Mzungu mwenzao mapema tu wangekuwa washafanya mazungumzo naweza sema huwa kuna Racism iliyojificha.
Screenshot_20260601-221140.jpg
 
Shida sio mvuto, kama unakumbuka alichosema amorim kwamba tunatakiwa kusajili mchezaji anayependa kuchezea Mun fc. Hivyo sijui kwa hiki kipindi cha Carrick hawa glineos kama wataendelea na hii falsafa.
Jamaa alitufumbua macho kwa kauli yake hii, maana tulikuwa tunalazimisha upendo matokeo yake wachezaji wanakimbia kama wamefungwa mawe miguuni. Lakini bado nina hofu sana kama kutakuwa na mwendelezo kwenye hili, tujipe muda.
 
Mbona hatukupata upinzani mkubwa kwenye hii sajili ya Ederson?
Zilikuwepo Pinzani maana Atl Madrid walikuwa washaanza kusema nae na ndipo Baada ya kusikia Man U wanahitaji huduma yake nazani alikuwa anapataka Dogo akatia msimamo haendi Popote zaidi ya Man u yani ni kama Mbeumo alivyowachana mapema, sema utofauti ni kuwa Timu nyingine zikishaskia mtu anataka upande furahi zinamsikuliza zinaachana nae tofauti na Man U wazee wa kung'ang'ana na Demu asowapenda (Anderson) De Jong pia kama unakumbuka na ndio maana hujaona Competition kwenye kumchukua.
 
NtYga fuentte huyu lewis hall inabidi tumchukue sijajua kama anataka kuja united.
Nadhani hili linawezekana kabisa hasa ukizingatia kwa sasa ni kama Newcastle United inatawanyika sana. Hata yule Tonali na Guimares wanafikika kwa sasa. Howes naye ni kama amefikia mwisho wa project yake mkuu, Hivyo vijana wengi wataondoka pale St James Park.
 
Hivi kwa sasa Dorgu tuna muweka nafasi gani na tunamthaminisha vipi ubora wake? Nataka nijue kama ilikuwa transfer ya kuimarisha kikosi kipindi kile cha mpito au anakuwa sehemu ya mipango ya muda mrefu ya timu? Je, anafit kama starter?
Mie hua najua dorgu ni left wing back, pia naona ni sehemu, ya mipango ya mda mrefu ya timu. Kwakua msimu ujao tupo hadi UEFA, na rotation ni muhimu sababu ya mechi nyingi.

Hapa nikuomba injury zisiwe nyingi kwa wachezaji, ngoja tuone Carrick atakavyopanga kikosi. Lakini kikubwa ni beki wa kushoto. Ebu fikiria tupangwe na Barcelona au bayern afu Luke shaw amakabe yamal na olisse, hapa kutakua na red card ya mapema sana.
 
Nadhani hili linawezekana kabisa hasa ukizingatia kwa sasa ni kama Newcastle United inatawanyika sana. Hata yule Tonali na Guimares wanafikika kwa sasa. Howes naye ni kama amefikia mwisho wa project yake mkuu, Hivyo vijana wengi wataondoka pale St James Park.
Mkuu ni kweli unachosema ijapokua howes kajitahidi mno. Na baada ya anthony Gordon kwenda Barcelona Newcastle watatusumbua sana kama tukitaka kumchukua tonali na lewis hall.
 
Back
Top Bottom