fuentte
JF-Expert Member
- Jul 30, 2015
- 3,472
- 10,049
Bado hatujaanza kuwa na mvuto sokoni tu!Anderson ni kujisumbua tu maana keshasema anataka mancity.
Bado hatujaanza kuwa na mvuto sokoni tu!Anderson ni kujisumbua tu maana keshasema anataka mancity.
Shida sio mvuto, kama unakumbuka alichosema amorim kwamba tunatakiwa kusajili mchezaji anayependa kuchezea Mun fc. Hivyo sijui kwa hiki kipindi cha Carrick hawa glineos kama wataendelea na hii falsafa.Bado hatujaanza kuwa na mvuto sokoni tu!
Jamaa alitufumbua macho kwa kauli yake hii, maana tulikuwa tunalazimisha upendo matokeo yake wachezaji wanakimbia kama wamefungwa mawe miguuni. Lakini bado nina hofu sana kama kutakuwa na mwendelezo kwenye hili, tujipe muda.Shida sio mvuto, kama unakumbuka alichosema amorim kwamba tunatakiwa kusajili mchezaji anayependa kuchezea Mun fc. Hivyo sijui kwa hiki kipindi cha Carrick hawa glineos kama wataendelea na hii falsafa.
Yule jamaa ana jicho la usajili banaIla jamani amorin kuna kitu amekifanya, hata Carrick ameivusha timu kutokana na kuundo wa amorin.
Kwanza kuwaondoa wavivu na kuleta wapiganaji. Carrick anapaswa ajue anatembelea muundo wa amorin..kosa lake amorin kungangania mfumo mmoja
Fabrizio anasema zipo club nyingine, zilizotuma maombi atalanta. Lakini Ederson, alikuwa keshasema anaitaka Manchester United, ndio maana hili dili limenda fasta.Mbona hatukupata upinzani mkubwa kwenye hii sajili ya Ederson?
Zilikuwepo Pinzani maana Atl Madrid walikuwa washaanza kusema nae na ndipo Baada ya kusikia Man U wanahitaji huduma yake nazani alikuwa anapataka Dogo akatia msimamo haendi Popote zaidi ya Man u yani ni kama Mbeumo alivyowachana mapema, sema utofauti ni kuwa Timu nyingine zikishaskia mtu anataka upande furahi zinamsikuliza zinaachana nae tofauti na Man U wazee wa kung'ang'ana na Demu asowapenda (Anderson) De Jong pia kama unakumbuka na ndio maana hujaona Competition kwenye kumchukua.Mbona hatukupata upinzani mkubwa kwenye hii sajili ya Ederson?
Nadhani hili linawezekana kabisa hasa ukizingatia kwa sasa ni kama Newcastle United inatawanyika sana. Hata yule Tonali na Guimares wanafikika kwa sasa. Howes naye ni kama amefikia mwisho wa project yake mkuu, Hivyo vijana wengi wataondoka pale St James Park.
Hivi kwa sasa Dorgu tuna muweka nafasi gani na tunamthaminisha vipi ubora wake? Nataka nijue kama ilikuwa transfer ya kuimarisha kikosi kipindi kile cha mpito au anakuwa sehemu ya mipango ya muda mrefu ya timu? Je, anafit kama starter?
Mie hua najua dorgu ni left wing back, pia naona ni sehemu, ya mipango ya mda mrefu ya timu. Kwakua msimu ujao tupo hadi UEFA, na rotation ni muhimu sababu ya mechi nyingi.Hivi kwa sasa Dorgu tuna muweka nafasi gani na tunamthaminisha vipi ubora wake? Nataka nijue kama ilikuwa transfer ya kuimarisha kikosi kipindi kile cha mpito au anakuwa sehemu ya mipango ya muda mrefu ya timu? Je, anafit kama starter?
Mkuu ni kweli unachosema ijapokua howes kajitahidi mno. Na baada ya anthony Gordon kwenda Barcelona Newcastle watatusumbua sana kama tukitaka kumchukua tonali na lewis hall.Nadhani hili linawezekana kabisa hasa ukizingatia kwa sasa ni kama Newcastle United inatawanyika sana. Hata yule Tonali na Guimares wanafikika kwa sasa. Howes naye ni kama amefikia mwisho wa project yake mkuu, Hivyo vijana wengi wataondoka pale St James Park.
Dogo anawasha moto sana kulingana na Mechi nilizofanikiwa kumuona anatufaa mNooo na sizani kama anao uwezo wa kukataa maana anakaa kwao huyo wazazi wakisema anafuata.
Dorgu ni mchezaje aliyechukuliwa kwa mpango wa muda mrefu, na inavyosemekana Carrick alipofika alimchagua moja kwa moja Dorgu awe stater Winga ya kushoto dhidi ya Mateus Japo Mateus alikunja na ndipo wakaambiwa wapambanie namba na ndio maana unapaona upande wao Pa moto sana.Hivi kwa sasa Dorgu tuna muweka nafasi gani na tunamthaminisha vipi ubora wake? Nataka nijue kama ilikuwa transfer ya kuimarisha kikosi kipindi kile cha mpito au anakuwa sehemu ya mipango ya muda mrefu ya timu? Je, anafit kama starter?
Tukiachana na Luke kuna huyu Dalot nae hibi kweli anakutana na Krava au Vini si tumekwenda na maji, hawa watu wawili Impact yao ni ndogo sana ukilinganisha na wanachopata pale united walitakiwa kuondoka misimu mi 3 iliyopita 🤕.Mie hua najua dorgu ni left wing back, pia naona ni sehemu, ya mipango ya mda mrefu ya timu. Kwakua msimu ujao tupo hadi UEFA, na rotation ni muhimu sababu ya mechi nyingi.
Hapa nikuomba injury zisiwe nyingi kwa wachezaji, ngoja tuone Carrick atakavyopanga kikosi. Lakini kikubwa ni beki wa kushoto. Ebu fikiria tupangwe na Barcelona au bayern afu Luke shaw amakabe yamal na olisse, hapa kutakua na red card ya mapema sana.
Mkuu unachosema ni ukweli kabisa tumalizane na middlefilders kwanza, tupate beki moja ya kushoto na beki ya kulia. Hapa tunaitaji wachezaji angalau wasiopungua 5.Tukiachana na Luke kuna huyu Dalot nae hibi kweli anakutana na Krava au Vini si tumekwenda na maji, hawa watu wawili Impact yao ni ndogo sana ukilinganisha na wanachopata pale united walitakiwa kuondoka misimu mi 3 iliyopita 🤕.