Jana nimeshuhudia soka tamu la kitabuni, soka la mipango sio la papatu. Mechi za Bilbao vs Arsenal, R. Madrid vs Marseill, Juventus vs Dortmund, PSV vs USG zilikuwa mechi Bora sana. Sikupata kuiona mechi ya Benfica vs Qarabag lakini kwa comeback waliyofanya Qarabag naamini nayo ilikua mechi Bora pia.
Jana nilitafakari sana kumbe Man utd tunakosa vitu vizuri usiposhiriki UEFA Kuna excitement Fulani kama shabiki unaikosa.
Kwa pira papatu la Amorim naona kabisa msimu ujao tutaendelea kukosa Uefa.
Mfumo wa kutegemea ma wing-back kama creative players wako wa kutengeneza magoli tutasubiri sana kwa mpira wa kisasa. Ndio maana msimu uliopita tulifunga magoli machache kuliko misimu yote. Huu mfumo una mafanikio sana katika ligi zisizo na ufundi mwingi na Kasi kama Serie A ya Italy, ndio maana ligi ya Italy inazalisha magoli machache kulinganisha na ligi zingine kubwa kutokana na timu nyingi kutumia huu mfumo. Ila kwa England, Spain na Ujerumani utapigika sana. Alonso mwenyewe kaenda Spain kaachana nao huu mfumo.
Siwapendi Arsenal ila kwa soka wanalopiga huwezi kuchoka kuwatazama, yule Zubimendi ni maestro haswa.
Nawakubali makocha wa kiispain, makocha wote wanaotamba sasa hivi ni wa spain kama Alonso, Guardiola, Arteta, Luis Enrique, Fuente wa timu ya taifa Spain. Namwona Xavi ni mtu sahihi wa kumpa hii timu nasi tufurahie soka tamu.
Viva United.