POVU LA ZLATAN IBRAHIMOVIC KWA MANCHESTER UNITED
Zlatan Ibrahimovic: "Kuna jambo moja lililonishangaza sana: kila mtu anadhani Manchester United ni klabu kubwa sana, mojawapo ya matajiri na yenye ushawishi mkubwa duniani. Nilipokuwa naitazama klabu hiyo kutoka nje, niliamini hivyo pia."
"Lakini nilipofika ndani, nilikuta ni taasisi yenye mawazo ya kitoto."
"Siku moja tulikuwa hotelini na timu kabla ya mechi. Nikahisi kiu, nikafungua friji ndogna nikanywa juisi ya matunda."
"Tulicheza mechi, kisha kila mtu akarudi nyumbani. Baadaye nikapokea mshahara wangu, na nikagundua wamekata paundi moja (pauni 1 – takriban shilingi 3,500). Nikashangaa, nikampigia meneja wa timu:"
‘Samahani, mbona wamekata paundi moja kwenye mshahara wangu?’
Akanijibu: ‘Ni kwa sababu ya ile juisi uliyokunywa kwenye mini bar ya hoteli.’
Nikasema: ‘Unaongea kweli? Hii ni mzaha?’
Akasema: ‘Hapana, hapa kwetu ukiagiza kitu chochote, lazima ukilipe.’
Zlatan akaendelea:
"Lakini sikuenda hotelini kwa mapumziko yangu binafsi, nilikuwa kazini – kwa ajili ya Manchester United. Kama nipo kazini na nahisi kiu, lazima nijinyweshe. Siwezi kwenda kucheza mpira nikiwa nimekauka! Hata hivyo walinikata pesa hiyo. Unaweza kuamini? Paundi moja tu! Hii ni aina ya mambo madogo ambayo hayawezi kutokea nchini Italia. Ni mambo kama haya madogo madogo yanayofanya mchezaji aheshimu klabu au ahisi kutothaminiwa."
"Kila siku nilipokuwa naingia kwenye uwanja wa mazoezi, nilitakiwa kuonyesha kitambulisho changu. Nilikuwa nashusha kioo cha gari na kumwambia mlinzi:
'Sikiliza ndugu yangu, nimekuwa nikija hapa kila siku kwa mwezi mzima sasa. Mimi ni mchezaji bora duniani. Kama bado hunitambui, basi uko kwenye kazi isiyokufaa.'”
Kenny Anjelina Maradona