King faisal
JF-Expert Member
- Jun 7, 2022
- 2,068
- 5,281
Hapa nimekuelewa vizuri flano.Binafsi sitamani kabisa kuona wachezaji wenye majina makubwa wanasajiliwa msimu huu, haya majina makubwa hayajawahi kua na msaada wowote tangia kuondoka kwa Ferguson, msimu huu ningependa kuona Amorim anawaamini zaidi madogo na kuwapatia nafasi ya kutosha, na kama kuna umuhimu mkubwa wa kusajili mchezaji mwenye uzoefu basi tusisajili nje ya Epl na mchezaji mwenyewe atakaesajiliwa aoneshe nia ya dhati ya kuipenda timu kama ilivyokua kwa Brian Mbeumo.
Siamini kama timu haina pesa ya kusajili wachezaji wa bei ghali maana juzi tu matajiri walikuja na project ya kutaka kujenga uwanja mpya, ila ninaamini msimu huu management imejitathmini kwa kina na kuona ni kwa namna gani jinsi wao wenyewe wanavyochangia kurudisha nyuma maendeleo ya timu kwa sajili zao za gharama kubwa kwa malengo ya kibiashara zaidi kuliko kuboresha ufanisi wa club.
