HENRY14
JF-Expert Member
- May 13, 2021
- 3,643
- 7,073
Nadhani hamis anachosema ni Arteta alisajiliwa 20 Dec 2019, hivyo huu ni msimu wake wa 5 (19-20, 20-21, 21-22, 22-23, 23-24). Mimi napenda kusema ni msimu wa 4 kwa sababu wa kwanza alikuja December na huu bado haujaisha 😀.Hivi Khamisi kwa nini huwa unapenda Kuongopa!?
Arteta Yupi alikwenda "Toe to Toe" na Pep? Imemchukua Arteta Misimu 5 kupata Matokeo Mbele ya Pep katika EPL mechi takribani 8 kafungwa zote hana hata Suluhu.
Mechi Arteta anamfunga Pep hakuna hata Mchezaji Mmoja aliyeanza wakati anacheza Mechi ya kwanza na kufungwa 3-0. ETH ana mapungufu ila Msimu wa kwanza tu alipata Matokeo kwa Hao "Giants" wawili wa Ligi kwa kipindi hiki.
View attachment 2924969
Mechi hii ni Msimu wa 3 wa Arteta anacheza na "BACK 5" Mechi nzima ana Shambulizi 1 na hana ON-TARGET hata Moja! Wewe na Castr mlishakataaga mwalimu wenu hajawahi tumia Mabeki 5, sasa hapa alitumia wangapi?
Hoja yako kwamba wewe Ulisema ETH sio Mwalimu, Itazame Ajax tangu ameiacha hali yake na imeshaweka walimu wangapi, Hawezi kuwa Daraja la PEP ama Klopp, ila kwa Muundo sahihi toka Juu anaweza badili kitu UTD {Mpaka sas UTD ina wachezaji wa Tangu Fergiee} Arteta ameshasajili wachezaji zaidi ya 25.
UTD ilipofika Matatizo ni mengi sana kuanzia Juu. De Zerbi, TT, Poch ulikuwa unawajaza sifa wote humu ila Mpira uwanjani unasema tofauti. Tuna shida ya Kufunga tangu OGS, Tizama GD hapo msimu umeisha bado ilikuwa ni 0!
Hayo matokeo ya hapo nakumbuka ndiyo wakati Arsenal fans karibia wote kwenye jukwaa letu tulikuwa tunataka Arteta aachishwe kazi ila nadhani Hamis peke yake ndiye alikuwa anamtetea. Tulikuwa tumeanza kujipata licha ya matokeo mabovu mfululizo. Tulikufa 2-0 kwa Brentford, 2-0 kwa Chelsea, 5-0 kwa City.
Tukawa chini kabisa hatuna point, hatuna goli, tumeshapigwa 9. Ila tulianza kunyanyuka na mwishowe tuliboronga tukaingia Europa. Kabla ya hapo tulimaliza wa 8 mara mbili, yaani ule nusu msimu, na msimu mzima wa kwanza wa Mikel. Baada ya hapo kuna mechi angalau moja ambayo tumempiga City msako (Hamis alikuwa anauita huu msako 'utatoa hotoi'), Partey alitawala dimba, ila tulipoteza mechi dakika za mwisho kabisa.
Tulizingua tukafungwa nyingine ila hapo tulikuwa tumeanza kukataa kuwa wateja kwa City. Kwamba tutawachezea mtindo wetu hata tukifungwa. Nadhani hii ndiyo 'toe to toe' anayoongelea Hamis na kweli tumeanza kuona mwanga baada ya muda mrefu. Shida hii tumeipata kwa United kiasi fulani, Liverpool na hata Chelsea na Tottenham ambao walitunyang'anya ufalme wa London kwa muda ila tumepambana kurejesha utawala wetu na tukikaa vizuri tutaumiliki mazima tena.
Arteta alipewa kazi ya kurejesha Arsenal katika kupambania ubingwa. So far ameweza kufika hapo. Sasa kazi yake ni kushinda mataji. Mtihani huu bado hatujui kama atauweza ila ameonyesha kuwa anauwezo huo.
Tukija kwa Ten Hag, kweli amepata matokeo na giants na msimu wa kwanza alishika nafasi ya 3. Hamis huwa anasema pamoja na kupata matokeo, aliita style ya Ten Hag 'pira janja janja' ambao hauwezi kuwasaidia mara nyingi na kwamba anavyoendelea nao, matokeo yatazidi kuwa mabaya kwake kadri ligi inavyomzoea.
Ukiangalia mwenendo wenu wa sasa, maneno ya Hamis yanaonekana kutimia.
Binafsi naamini baba ubaya ni bonge la kocha ila kuna vijimambo vidogo vidogo vikiclick ataleta usumumbufu mkubwa sana.

