Ndugu, suala kubwa hapa ni Uelewa. Hakika huelewi unachoandika.
Katika ufalme wa Mungu kuna safari mbili. Safari ya pili ndio inakufanya uitwe Mungu ( Au Mungu wa Nyakati)
Nakujibu kimahesabu sasa ( Safari ya pili)
1. Jesus + Emmanuel + Jesus Christ
2. Word + Word with God + God
3. Man + Man of Dust ( Man of God) + Man of Heaven
Hayo maelezo uliyoyatoa pamoja na mistari uliyoitoa pasipo kuielewa, aliitumia akiwa katika njia hizo kuelekea katika Ukuu. Ndio maana aliweza kusema yeye ni Mkuu kuliko Abraham au Solomon - ( sababu hawa walikua men of God )
Narudia tena kukwambia, ni vigumu sana kuelewa mambo ya Mungu kama haujawahi hata siku moja kukanyaga Mawingu.
Kuna tofauti kubwa sana kati ya Mtu anayeyaona mawingu kwa Hekima zake na Yule anayeyaganyaga kila siku.
Kuna baadhi ya watu wachache sana wanaonielewa humu sio wote.
#1Corinthians 2:14, "The natural person does not accept the things of the Spirit of God, for they are folly to him, and he is not able to understand them because they are spiritually discerned."
#1Cor 2:13,"And we impart this in words not taught by human wisdom but taught by the Spirit, interpreting spiritual truths to those who are spiritual."
Kwa kauli hii una maa Mungu alifanya KUSUDI baadhi tu ya watu Waweze kuelewa UWEPO WAKE na wengine wasielewe ili APATE KUWAADHIBU bila Kosa lao au sio?
Kwa kauli hizi We huoni km Tayari umeshamtukana Mungu kwa kumuita Mbaguzi?
Hizo Hesabu umetoa kutokana na Fikra zako na Kamwe Mungu hawezi Kuuficha Ufalme wake kwa Baadhi ya watu Tu.
Nimekupa Mistari iliowazi ilioandikwa KISWAHILI, Badala ya wewe kunidadavulia Hio Mistari na maana zake Kwa unavyoelewa Wewe unaniandikia namba ambazo umetoa KICHWANI KWAKO.
Kuna Binaadamu ameshawahi Kukanyaga mawingu ? Au unatumia Methali ambazo hata yesu hakuwahi Kuzitumia ili kupotosha Ukweli?
We umeshawahi kuyakanyaga hayo mawingu?
Na wapi andiko linasema haya?
Nimekuuliza Km Yesu alikuwa MUNGU kabla ya kuja hapa Duniani ina Maana alipokuja hapa Duniani yale maombi aliokuwa anayafanya ya KUOMBA MSAADA NA KUEPUSHWA NA KIFO alikuwa ANAJIOMBA MWENYEWE?
Na kwa Mujibu wa Imani yako alipoUAWA MSALABANI ina maana MUNGU ALIKUFA ili AJIRIDHISHE MWENYEWE?
Mnadai Mungu ni Mwingi wa Rehema Na Mwenye kusamehe Mwenye Nguvu zote na uwezo wote.
Sasa KUAMUA KUJIUA YEYE MWENYEWE KWA KIFO CHA LAANA cha MSALABA ili AJIRIDHISHE MWENYEWE hio Ni Huruma na Rehema kwako?
Km yeye ni Muweza wa Kila kitu alishindwa Kusamehe Wanaadamu Mpk AJITOE UHAI WAKE?
Ndio nikasema Usiwe unapenda Kupewa maneno na Watu kinyume na Maneno aliyotamka YESU YEYE MWENYEWE.
Yesu anakwambia BWANA ni Mkuu kuliko Mimi. Wewe unasema Yesu ndio huyo huyo Bwana! Hii inaingia AKILINI?
Katika kitabu cha Matendo ya Mitume inasimuliwa kuwa Stefano alisema aliyoyaona yaliyo mbinguni. Alisema:
Tazama! naona mbingu zimefunguka, na Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wa Mungu.
Matendo 7.56
Mwana wa Adamu ndiye Yesu, na kwa jina hilo ndio mwenyewe akipenda kujiita, sio Mwana wa Mungu.
Hapo basi huko mbinguni Stefano anasema anamwona Yesu kakaa mkono wa kulia wa Mungu.
Mwenye kukaa mkono wa kulia wa fulani hawezi kuwa ndiye yule yule fulani.
Hayo ni maelezo ya mbinguni. Ni wazi basi kwa ushahidi wa Biblia kuwa Yesu hakuwa Mungu mbinguni kama alivyokuwa si Mungu duniani.
Yesu alipokimbilia kwenye Mlima wa Zaituni na huku akisakwa na Mayahudi alijitenga na wanafunzi wake. Huko faraghani aliomba hivi:
Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako, uniondolee kikombe hiki; walakini si mapenzi yangu, bali yako yatendeke. Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu.
Luka 22.42-43
Hapa tunaona mambo matatu muhimu:
1.Yesu anamwomba Mungu.
Yesu anamwabudu Mungu. Wawili hao ni mbali mbali, na vyeo vyao ni mbali mbali. Yesu ni mtumwa mnyonge mwenye kuomba na kuabudu. Na Mungu ni Mwenyezi Mungu mwenye uwezo wote na mwenye kustahiki kuabudiwa pekee, hata na Yesu, mwenye kutakiwa msaada pekee, hata na Yesu.
2.Mapenzi ya Mungu ni mbali na yale ya Yesu.
Yesu hataki kuuliwa, ananyenyekea na kuomba kwa Bwana wake: "uniondolee kikombe hiki" cha mauti. Yesu hana azma hata chembe ya kufa msalabani, kifo cha mhalifu, kifo cha laana kama maadui zake Mayahudi walivyoazimia kumpatilisha nacho. Lakini anakiri kuwa ni mapenzi ya Mungu sio yake yeye yatendeke. Yeye hana hila wala nguvu za kuzuia kudra ya Mwenyezi Mungu.
3.Yesu, Mwana wa Adamu, anakata tamaa. Imani inampunguka. Kavunjika moyo. Ikabidi "Malaika kutoka mbinguni akamtokea akamtia nguvu."
Jee, yaelekea kuwa Yesu ndiye Mungu?
Je,Yaelekea kuwa yeye na Mungu kuwa ni sawa?
Kama upo wasiwasi wo wote wa kujibu hayo, mwenyewe Yesu anajibu kama anavyo hadithiwa na Yohana kuwa kasema:
Baba ni mkuu kuliko mimi.
Yohana 14.28
Na mwishoni naye yupo mslabani:
Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha?
Mathayo 27.46
Yafaa hapa tujiulize:
Yesu akimlilia Mungu gani hapo msalabani ikiwa naye mwenyewe ni Mungu? Au nini alikusudia aliposema: "Mungu wangu naye ni Mungu wenu"? Maneno hayo kama yanaonyesha cho chote basi yanaonyesha unyenyekevu wa Yesu mbele ya Mungu wake.
La kustaajabisha ni kule kukata tamaa kwake na kuvunjika moyo. Huwaje mtu wa imani, licha ya nabii na mwana pekee wa Mungu, akate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu.
Ama kuwa Mungu akate tamaa na Mungu, na kumyayatikia: "Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha", ni jambo ambalo halimkiniki kuwa.
Kwa uthibitisho ulio wazi Biblia inatwambia kuwa Yesu si Mungu, wala Mungu si Yesu.
MI nakupa Maandiko Yalio wazi Ndugu. Wewe unatoa yalio Kichwani kwako. Hivi ndivyo alivyofundisha YESU?
Umri wetu ni Mfupi mno. Na baada ya KUFA HAKUNA kuomba msamaha tena.
Usimpe MTU cheo cha UUNGU.
Hio ni KUFURU isio na msamaha mbele ya Mungu.
MUNGU NI MMOJA TU. sio YESU wala Sio Utatu mtakatifu. Hii habari NI SHRKI NA KUFURU iliowazi. Na wala YESU HAKUWAHI KUUDAI UUNGU ktk Maisha yake yote.
Ahsante kwa kunisoma.