Manabii wanaokwenda na wakati

Manabii wanaokwenda na wakati

Forbes inamtambua kwa biashara zake na hakuna sehemu imegusia kanisa, mwambie Bwege huyo
Ndugu, hakuna jaribu kubwa katika njia ya msalaba kama lile la kushindana na mwanamke. Hapa watumishi wengi sana huwa wanarudi nyuma na kushindwa kuifikia nchi ya Roho na Ukweli.

Hatua hii huwa ni ngumu sana kwani mtumishi lazima awe kwenye mateso makali, njaa kali, kiu n.k

Sasa kutokana na ukata huo, wengi hukimbilia kuzini + kupewa raha na mwanamke huyo; Safari yao huishia hapo , na kisha wanapewa majukumu ya kufanya kwa niaba ya huyo mwanamke.


Jiulize, Kwanini Yesu hakuoa mwanamke au kwanini hakuwa na Biashara? Kumbuka pia, kuishi chini ya Hisia zako hukufanya kuusumbukia mwili wako...mfano: Ukiona mwanamke kavaa vibaya uume wako unasimama... Tamaa ya vitu, kutoridhika, kushindana na watu, kutojitambua kuwa hapa upo kwa muda tu etc

Je umewahi kukutana na MTU anayeishi juu ya Hisia zake? MTU aliye pita kwenye maji mengi, milima, mabonde, mito, kwenye moto? Mimi ni mmoja wao... Nakueleza yote Haya kwa dhamira njema ili uyatafakari , hata roho Mtakatifu ni shahidi yangu hapa , kwamba ninachokueleza ni ukweli mtupu!

Mungu akubariki! Amani na iwe juu yako!
 
Wewe ndio zwazwa kweli, KRISTO ni mmoja tu. Kina yesu wako kibao huko Latin America.
Ndugu, Hapa tatizo ni Uelewa. Wakristo wapo wachache na Kiongozi wao ni Yesu Kristo. Andiko "Christ" au "Kristo" ni Cheo , maana yake ni " The Annointed One" au the Son of God.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya Wafuasi wa Kristo na Wakristo au Wanafunzi wa Kristo na Wakristo.

Hapa watu wengi huwaita watu majina ya wao wakristo pasipo hata kuelewa nini wanatamka.

Kwa taarifa yako, TANZANIA nzima haina wakristo hata wanaofika wa tano tu... Tena watano ni Wengi sana.

Hao unaowasikia na kuwaona, ni Wafuasi na Wanafunzi wa Kristo.

Kuna Mkristo anaandaliwa , siku akitolewa; utamuona; kila jicho litamuona.

Kama ni wewe, basi Jina lako litakuwa " Mugajamii Kristo " au " Frank Christ"
 
jibu swali kikamilifu mkuu.Anafanya biashara gani?
Hawawezi kukujibu vyema; kwasababu wanaishi kwa hisia. Kwa nje wanaonekana vizuri lakini kwa ndani Mioyo yao imejaa maji machafu; Ukiwakoroga kidogo hawachelewi kukuita "bwege" au kukutukana. Hayo ndio mafundisho wanayojengewa au maji wanayojazwa ndani ya Mioyo yao na hao MANABII feki

Slogan yao kuu ni " MIRACLE MONEY "
 
Yeah ni mfanyabiashara mkubwa UK.anafanya biashara za real estate.na anatumia pesa zake kwa ajili ya kuhubiri injili matangazo yote anayorusha kupitia satelaite analipia mwenye kwa pesa binafsi
Ndugu, unaweza kutoa mstari wowote kwenye Biblia ambao unaonyesha MTU mwenye cheo cha Nabii, Kuhani au Mtume ni Mfanyabiashara?

Na kama haujauona, Unaelewa kwanini vyeo hivyo ni marufuku MTU wa Mungu kuwa mfanyabiashara?

Je unafahamu Purpose na Mission za Nabii au Mtume anapotumwa Ulimwenguni na Mungu?

Amini nakwambia kweli, hao MANABII unaowasifia missions zao kubwa ni kuiba Utukufu wenu, destiny, kuharibu na kuua ili muende motoni.
 
"vCTRMA, post: 15809518, member: 348463"]hivi watu wanajua maana ya nabii ni nini??????????
tatizo watu hawasomi neno la MUNGU,."


JIBU

Ndugu, Kuna tofauti kubwa sana kati ya Neno la Mungu na Andiko La Mungu.

Tunasoma Maandiko ya Mungu , sio Maneno ya Mungu. Maneno ya Mungu hayasomwi bali yanapatikana kwa njia ya kutafakari ( kwa njia ya Roho Mtakatifu, katika Kristo Yesu)

Kumbuka, andiko linauwa, bali neno linajenga ( linatupa uzima)

Huwezi kupata neno la Mungu kutoka kwenye maandishi ya Mungu kama wewe sio mfuasi wake ( I mean, kama haujaitwa kujumuika katika njia ya msalaba through Repentance)

Tatizo hapa ni kwamba, watu wanasoma andiko la Mungu lakini hawalielewi kwasababu hawajaitwa na kufanywa kuwa wafuasi au kutokana na kuishi katika hali ya dhambi.

Kumbuka pia, Uelewa ni zawadi kutoka kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.
unamaanisha nini,neno la MUNGU likoje na andiko likoje,.biblia ni andiko au neno,.usichanganye watu kwa akili zako binafsi,.
 
"vCTRMA, post: 15809518, member: 348463"]hivi watu wanajua maana ya nabii ni nini??????????
tatizo watu hawasomi neno la MUNGU,."


JIBU

Ndugu, Kuna tofauti kubwa sana kati ya Neno la Mungu na Andiko La Mungu.

Tunasoma Maandiko ya Mungu , sio Maneno ya Mungu. Maneno ya Mungu hayasomwi bali yanapatikana kwa njia ya kutafakari ( kwa njia ya Roho Mtakatifu, katika Kristo Yesu)

Kumbuka, andiko linauwa, bali neno linajenga ( linatupa uzima)

Huwezi kupata neno la Mungu kutoka kwenye maandishi ya Mungu kama wewe sio mfuasi wake ( I mean, kama haujaitwa kujumuika katika njia ya msalaba through Repentance)

Tatizo hapa ni kwamba, watu wanasoma andiko la Mungu lakini hawalielewi kwasababu hawajaitwa na kufanywa kuwa wafuasi au kutokana na kuishi katika hali ya dhambi.

Kumbuka pia, Uelewa ni zawadi kutoka kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.
we ni mroma alafu vCTRMA kaokoka.....hamuwezi kuelewana apo,wewe umemezeshwa na kukalilishwa mapokeo waliookoka ni tofauti ni nyie,.naomba nikuulize swali,.unajua roho mtakatifu ni nini maana yake?
 
tunakuja pale pale tatizo watu hawasomi neno la MUNGU
tatizo la wakristo siku hizi ni kufata miujiza kila kukicha,.na kutabiliwa,watu wanahangaika yani,neno la kristo halijaakaa ndani ya Watu kabisa,.watu hawasomi maandiko kabisa na ndomaana wanachanganywa hovyohovyo,.watu hawatulii makanisani,hii ni shida sana
 
Ndugu, unaweza kutoa mstari wowote kwenye Biblia ambao unaonyesha MTU mwenye cheo cha Nabii, Kuhani au Mtume ni Mfanyabiashara?

Na kama haujauona, Unaelewa kwanini vyeo hivyo ni marufuku MTU wa Mungu kuwa mfanyabiashara?

Je unafahamu Purpose na Mission za Nabii au Mtume anapotumwa Ulimwenguni na Mungu?

Amini nakwambia kweli, hao MANABII unaowasifia missions zao kubwa ni kuiba Utukufu wenu, destiny, kuharibu na kuua ili muende motoni.
sahihi,uko sahihi
ila mtume ni nani??unajua kaz za mtume
unajua nabii ni nani???na kaz zake effectively????
according to bible sio mapokeo
 
BIBLIA ni nini kwa post yako,naona unajichanganya ndugu...,...
2.maana yako njia ya msalaba ndo inaondoa dhambi??????????
Ndugu, Biblia ni kitabu kikubwa kuliko vyote hapa ulimwenguni. Ni kitabu kilichojaa maandishi ya Mungu , ambamo ndani yake kuna maneno ya Mungu.

Ni kitabu kichoandikwa na Roho wa Mungu kupita Kristo Yesu ( Who was, Who is and Who is to come)

Kitabu hiki ni vigumu sana kukielewa kama haujaalikwa kwenye njia ya msalaba through Repentance.

Kumbuka, Mungu / Yesu hutuelewa sisi kwa kila kitu ; anaelewa MTU aliyetayari kujumuika nae katika njia hiyo; Hakuna MTU anayeweza kujificha mbele zake.

Anawaelewa wale wote wanaotaka kujumuika kwa muda na kutoka; Hakika sisi tu uchi mbele ya kiti chake.

Sasa basi, wale ambao sio wake, ni vigumu kuisikia sauti yake na kuona matendo yake ( I mean, kilichoandikwa kwenye Biblia na kinachoendelea katika Maisha yako+ Mazingira yako)

Kumbuka, Uelewa ni zawadi kutoka kwa Mungu. Uelewa huu ni tofauti na huo unaotumia shuleni kujibia mitihani na kusomea.

Swali la pili;

Ni njia ya msalaba pekee ndio inayoweza kukuondolea dhambi, hakuna njia nyingine kaka. Yesu ndiye njia, kweli na uzima.

Lazima utubu kwanza ( kama utapata nafasi ya kuitwa) , ndipo uingie msalabani, kukombolewa, kuokolewa, kuchaguliwa/ kuteuliwa na kisha unatumwa...

Hii ni process sio ya siku moja, bali ni ya siku tatu.

NB; Faith is not a pressing button
 
tunakuja pale pale tatizo watu hawasomi neno la MUNGU
Ndugu, neno la Mungu Huwezi kulisoma. Neno la Mungu sio Hisia bali Ni roho na kweli, ; Neno la Mungu ni pumzi;

Unaweza kuiona pumzi kwa macho au kuishika? Inawezekana kiroho tu kama utakuwa connected na Kristo Yesu ( Yeshua Ha-Mashiach)
 
Ndugu, Biblia ni kitabu kikubwa kuliko vyote hapa ulimwenguni. Ni kitabu kilichojaa maandishi ya Mungu , ambamo ndani yake kuna maneno ya Mungu.

Ni kitabu kichoandikwa na Roho wa Mungu kupita Kristo Yesu ( Who was, Who is and Who is to come)

Kitabu hiki ni vigumu sana kukielewa kama haujaalikwa kwenye njia ya msalaba through Repentance.

Kumbuka, Mungu / Yesu hutuelewa sisi kwa kila kitu ; anaelewa MTU aliyetayari kujumuika nae katika njia hiyo; Hakuna MTU anayeweza kujificha mbele zake.

Anawaelewa wale wote wanaotaka kujumuika kwa muda na kutoka; Hakika sisi tu uchi mbele ya kiti chake.

Sasa basi, wale ambao sio wake, ni vigumu kuisikia sauti yake na kuona matendo yake ( I mean, kilichoandikwa kwenye Biblia na kinachoendelea katika Maisha yako+ Mazingira yako)

Kumbuka, Uelewa ni zawadi kutoka kwa Mungu. Uelewa huu ni tofauti na huo unaotumia shuleni kujibia mitihani na kusomea.

Swali la pili;

Ni njia ya msalaba pekee ndio inayoweza kukuondolea dhambi, hakuna njia nyingine kaka. Yesu ndiye njia, kweli na uzima.

Lazima utubu kwanza ( kama utapata nafasi ya kuitwa) , ndipo uingie msalabani, kukombolewa, kuokolewa, kuchaguliwa/ kuteuliwa na kisha unatumwa...

Hii ni process sio ya siku moja, bali ni ya siku tatu.

NB; Faith is not a pressing button
we ni mroma?????
 
hivi nabii ni nani wakuu? inakuwaje mpk mtu anaitwa nabii? mwnye definition ya nabii msaada please
 
nahisi hukuelewa dhima yangu
ni kuwawweka watu aware wawe wanazingatia neno la Mungu,......maana kuhumu tumezuiwa kwa namna yoyote ile,...
tusije tukahukumiwa sisi,...
matunda ya Yaliyo ktk misingi ya MUNGU ni dhahili na ya ibilisi ni dhahili thats why YESU akasema mtawatambua kwa matunda yao,...tukiwa ndani ya YESU pekee ndo tunaweza kuwatambua wenye matunda YA MUNGU na ya ibilisi......

kwenye red hapo,....kuutambua huo mti ni lazima uwe kwenye njia ya wokovu uwe na ukaribu na Mungu,...roho mtakatifu ndiye kiongozi kwa kila jambo unaposema mtu akijibanza sijui ningumu kumtambua unamaanisha kuwa roho mtakatifu unapinga uwepo wake.......
katika blue unazunguzia kuchaguliwa kivipi????????
minajua hadi unaokoka unakuwa tayari umepata neema,..maana paul anasema ktk waefeso tumeokolewa kwa neema
yaani tumechaguliwa tumeokoka kwa neema na sikwa akili zetu.........
Ndugu, na kuelewa vyema sana, tena sana Ndugu yangu.

Kuingia kwenye njia Takatifu ya Msalaba kuna hatua zake ( madaraja). I mean, the more unavyokua mtiifu na humble mbele za Mungu kupitia Yesu ndipo unapanda daraja la uelewa.

Kuna tofauti kubwa sana kati ya kuokoka ( wokovu ) na kukombolewa. Pia kati ya kuokoka na kuchaguliwa. Haya ni madaraja ambayo yanakuwa na hatua zake za Uelewa katika Ufalme wa Mungu.

Ni vyema ukatambua kwamba, Mungu/ Yesu ; yupo interested sana kwenye Mioyo yetu. Kama tukipewa Uelewa kidogo, ni lazima tuutumie kuuliza maswali ili tupate nguvu za kuendelea kuutafuta uso wake mpaka hatua ya mwisho ya kufunguliwa mlango wa mbinguni.

Hapa utaona Uelewa ni muhimu sana katika hatua zote.

Nataka kusema kwamba , daraja la kuokoka ( salvation) ( ambalo ni la pili, si la kwanza kama watu wanavyofikiri - katika ufalme wa Mungu) linaweza kumfanya MTU kuchaguliwa kama itampendeza Mungu ( kupitia Yesu)

Kuna watu wengi sana huwa wanaifikia hatua hii, lakini huwa hawawezi kuchaguliwa kutokana na Tamaa za miili yao pamoja na nguvu zilizopo kwenye Mazingira yao.

Hii ni sehemu ambayo huwaandaa watu kwenda kuvuna walichopanda. Na wengi huishia kula au kuvuna matunda ya miti ya Hisia ( sio ile waliyoipanda). I mean, wanaikana miti yao na kutamani kwenda kuvuna miti ya Ulimwengu huu.

Ushauri; Jichunguze njia zako; Tubu , rudi msalabani. Kumbuka , asiye elewa maana hana maana. Namaanisha, unaweza kuisoma Biblia nzima na kuikariri, lakini usielewe kilichoandikwa. Hili ni tatizo linalikusumbua kwasasa...,

Tafuta mzuri na Mungu/ Yesu ..... Mazingira unayoyatumia kusoma maandiko ya Mungu ndio yanakufanya usilielewe vyema neno lake. Hii itakufanya kuwa mjuaji tu lakini sio Muelewa.

Mungu akubariki sana. Damu ya Yesu ukutakase!
 
we ni mroma?????
Ndugu, Ufalme wa Mungu unajengwa kupitia Yesu Kristo.

Ukisema wewe ni Mkatoliki na ukasema unamuelewa Mungu utakuwa unajidanganya na ukweli hautakuwa ndani yako...

Kuna baadhi ya madhehebu yana moja kati ya vipande vya mwili wa Yesu na Damu yake... Mfano katoliki, rutheran, sabatho, waislamu n.k

Hawa wote wana vipande vipande.

Kwa MTU anayeutafuta USO wa Mungu kweli , ni lazima akusanye vipande vyote ili ukweli umuweke Huru. Sio kung'ang'ania dini moja na kisha unaanza kuhukumu watu vibaya pasipo kuwa na Imani au uhakika na unachosema.


Hivyo, basi, ninaelewa kwanini umeniuliza swali hilo! Lakini nakwambia kweli, Ni vigumu sana Mwanadamu kuingia mbinguni bila kupitia njia ya Msalaba ( katika Kristo Yesu)
 
sahihi,uko sahihi
ila mtume ni nani??unajua kaz za mtume
unajua nabii ni nani???na kaz zake effectively????
according to bible sio mapokeo
Maswali yako, yanamaanisha ulikuwa huelewi nilichoandika awali; na kwamba ulikuwa unabisha na kutumia ujuaji pasipo kuelewa nini unaandika.

Kama umeshindwa kunijibu , Mimi pia sitaweza kukujibu maswali yako. Asante
 
WEZI wanawaibia Na Kuishi maisha Ya Juu halafu nyie watoa hizo pesa mnaishi ka Mbuzi zizini.
Halafu hapo hapo mnawaita Manabii na Kuwapigia magoti wawasamehe madhambi yenu.

Teh teh teh.

Yule aliyewaita KONDOO aliwapatia sana aisee.
Duh..
 
we ni mroma alafu vCTRMA kaokoka.....hamuwezi kuelewana apo,wewe umemezeshwa na kukalilishwa mapokeo waliookoka ni tofauti ni nyie,.naomba nikuulize swali,.unajua roho mtakatifu ni nini maana yake?
Huelewi unachoandika. Kiufupi dini yangu ni kumsujudia na kumuabudu Mungu peke yake kupitia Yesu Kristo. Roho Mtakatifu ni Msaidizi wangu , MWALIMU na Ananiongoza mpaka kujibu maswali yenu.

Sio kila MTU anayesema kaokoka , au anaandika maandiko ya Mungu, ni Mtoto wa Mungu; wengine ni watoto na vijana wa shetani; Kazi yao kubwa ni kuhadaa watu kwa hisia zao.

Shetani analugha yake, Pia hata Mungu ana lugha yake.

MTU anayeishi chini ya Hisia zake hawezi kamwe kuielewa lugha ya MTU anayeishi juu ya Hisia zake. Ila ni rahisi sana kwa MTU anayeishi juu ya Hisia zake kuielewa lugha ya MTU anayeishi chini ya Hisia zake.

Mimi, naelewa lugha ya kila mmoja anayejibu post zangu.

Nina andika kizanaki, watu wengi wanajibu kisambaa. Wengine kizanaki feki. But , nashukuru na kufurahi kuwa Yesu Kristo anatajwa! He must be magnified forever and always, for God's Glory
 
kabanga;
Huyu ni nabii wa neno la Mungu na makao yake makuu ni Zimbabwe. Ila, ana ofisi nyingi pia hukooo majuuu. Wengi wamemkubali
Nani kampa unabii ?
We unadhani unabii ni km Kondakta wa Daladala?
Hata Konda anapewa kazi hio na mtu.
Hawa Wote ni Wezi tu. Km wale wa Agape tv
Yule mnaemuita Mtume kaja Dar hata Kiswahili hajui. Anaongea kigoa tu.
Kaajiriwa na muislamu alipoona Kuna Biashara ya Kupiga debe kaanzisha Kanisa lake.
Leo.anavaa shati na Tai. Anapiga hela kilainiii.
Kazi kupiga kelele tu na Kurudiarudia maneno yale yale km matangazo ya kifo.
Ovyoo.
 
the meek Nahitaji kuwajua kampani ya huyu bwana,nadhani ulisema wako Sijui watano all over Africa,pia ningependa kumjua vyema yule baba yao wa imani mghana,na picha au links kama hutojali
 
Back
Top Bottom