Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Nawasalimu wanaJF.kuna taarifa isiyokuwa rasmi kuwa Nape nnauye anaweza kuwa katibu mwenezi wa ccm,kama taarifa hizi ni za kweli basi hizi zitakuwa jitihada maalum za ccm kuhakikisha wanarudisha hadhi ya chama mbele ya vijana(kujivua gamba) kwani vijana ndio wapiga kura wajao.
Je kwa maoni yako unadhani Nape ana mvuto kwa vijana kiasi cha kubadilisha sura ya ccm kwa jamii haswa vijana?
Ni wale wale mtoto wa nyoka ni nyoka kaka hata akijivua gamba anabaki nyoka,niliwahi kumsikia Nape wakati wa kampeni za uchaguzi wa mbunge wa Kinondoni alikuwa na Tambwe Hiza ,katika kutoa hoja sikuona tofauti yoyote kati yake na Tambwe (ambaye huongea pumba wakati wote)mi nafikiri angekuwa yule kijana wa Arusha aliyesema inabidi tufikirie kwa kutumia kichwa badala ya tumbo,kwani ni kijana jasiri ,usipokuwa jasiri CCM unakuwa sawa na wale wale wa zidumu fikra za mwenyekiti wa CCM
 
wadau wa jf tuwe na utamaduni wa kupongezana pale mtu anapofanya jambo jema, nadhani jk anastahili pongezi kwangu ni mara ya kwanza kuona anatimiza ahadi zake anazozitoa, hivi karibuni mwezi februari alihaidi kuwa ccm itajivua gamba ili kurudisha taswira yake na mvuto kwa jamii na hili limetimia nadhani wansatahili bravoo

bravoo jk bravoooo,

bravo kwa ccm yenyewe kwa kukubali mabadiloko, daima wamekuwa watu wenye mawazo mgando na chama kushikiliwa na misimamo ya wachache lakini kwa sasa angalau wamekubaliana na kelele za magazeti na wananchi

bravoooooo ccm bravoooo
 
Kwani ndugu zangu si tunawataka viongozi bora au tunachokitaka ni kipi????????????????????mbona kwenye ukweli bado mnazungukazunguka tu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!nani hajui kuwa hata mnyika anamkubali Nape?cha kujiuliza hapa ni je,Nape ataweza kuwamudu hawa mafisadi wengine na siyo kumlinganisha na Mnyika,NAPE ni Jembe kubwa sana kwa Mnyika na hata Lema,hajaanza siasa leo na isitoshe amezaliwa ndani ya siasa,hakurupuki na ndio maana CCM ya Makamba walipomtosa kugombea Ubunge jimbo la Ubungo hakuropoka wala kuhamia chama chochote cha upinzani,alibaki na CCM yake,this was what impressed Jk hadi akamteua kuwa DC na hatimaye kumteua tena kuwa Katibu wa Siasa Itikadi na Uenezi wa Taifa,this guy ni mvumilivu.
Ishu ya kuwa anamvuto inategemea na your look kwake,ila kisiasa ana mvuto sana tu,kwani hata CHADEMA walimuwinda sana baada ya kutoswa kule ubunge,hata kuthubutu kumvalisha bendera yao.BILA CCM IMARA TANZANIA ITAYUMBA,by JK wa kwanza.
 
wadau wa jf tuwe na utamaduni wa kupongezana pale mtu anapofanya jambo jema, nadhani jk anastahili pongezi kwangu ni mara ya kwanza kuona anatimiza ahadi zake anazozitoa, hivi karibuni mwezi februari alihaidi kuwa ccm itajivua gamba ili kurudisha taswira yake na mvuto kwa jamii na hili limetimia nadhani wansatahili bravoo

bravoo jk bravoooo,

bravo kwa ccm yenyewe kwa kukubali mabadiloko, daima wamekuwa watu wenye mawazo mgando na chama kushikiliwa na misimamo ya wachache lakini kwa sasa angalau wamekubaliana na kelele za magazeti na wananchi

bravoooooo ccm bravoooo


am totally against ccm mpaka kifo!!
 
Mbona sasa hatupati mrejesho mpya mlioko frontline semeni basi au wamewakwepa? inteligensia tuleteeni mrejesho tunataka tuanze kutathmini uwezo wa chama baada ya kujivua gamba eti!!!!?
 
Cha kufurahia ni nafasi ya vijana katika siasa na kizazi hiki tufike wakati tusifungwe na itikadi za vyama bali tufungwe na malengo ya vijana kulikomboa taifa popote pale walipo pasipo kujali wewe ni wa chama gani.............Nape ni miongoni mwa wanaharakati safi katika vijana cha msingi nae asije akawa limbukeni wa sifa na vyeo anavyopatakwani vijana wengi ukiwapa cheo ndio unawamaliza kabisa

Hivi ni vigenzo gani vinavyotumiwa na JF kwa member kuwa Premium member?
 
Tunashukuru kwa taarifa endelea kutujuza maana sisi wengine tuko mbali na Dom.
 
Ni kweli kabisa tena kwa vigezo vingi Nape hawezi kumfikia mnyika. Vile vile kuna DAVID SILINDE Mbunge wa Mbozi Magharibi naye ni mkali anafaa kuwa mwenyekiti wa vijana na Nape hana ubavu wa kupambana naye
wa sura au kisiasa? kama ni sura Nape hamzidi Mnyika au Lema. Kama kisiasa Nape Hamzidi Mnyika, hata yeye mwenyewe (Nape) analijua hilo.
 
cdm ina vijana wengi ngazi ya uongozi wenye mvuto.mfano lema,mdee,wenje,sugu,mnyika n.k. isitoshe wazee walioko cdm wana maono ya ujana,kila mtu analijua hili hata JK pia.kwa ufupi naweza kusema kuna vita ya kugombea vijana na mshindi wa vita hiyo ndio atakayeongoza nchi hii miaka ijayo.

Mkuu mie sikubaliani na wewe yaani unamfananisha Nape na Sugu? tuzungumze ku ukweli Nape ni miongoni wa vijana wenye CV kubwa kiutawala na jina la Nape tumeanza kulisikia kabla ya hayo majina ya mengine labda jina la Sugu ndio la kitambo tena sio kwenye siasa ni kwenye bongo fleva....
 
Hapo umsesma Kiloni, Makamba yawezekana ni hopeless lakini usisahau wameshughulikia mapaka sasa the 'official leadership' lakini siyo yenye shida, yenye shida ni defactor leadership - hiyo haijaguswa na huenda haitaguswa. Mara nyingi CCM wameshakaribia sana kuigusa ile 'point of pain' lakini ghafla kigugumizi huwapata na wakaamua kuingia mitini kila mtu na lwake.

Yetu Macho!
 
The issue is not Nape Vs mnyika bali ni kweli nape ataweza kusababisha vijana waipende ccm?
 
WADAU SASA HIVI AJENDA INAYOTAWALA NI KUJIVUA GAMBA KWA CCM BALI ANGALIZO LANGU NI KUWA CHAMA HICHO KISIJIVUE GAMBA ILI HALI BADO SUMU HAWAJATEMA, NASEMA HIVI KWA KUWA GAMBA WALILO LIVUA NI KUBADILISHA SURA ZA KAMATI KUU NA SEKREATARIET WAKATI SUMU HAWAJAITEMA.

SUMU ILIYO ICHAFUA CCM NI MAFISADI KAMA ANDREW CHENGE, ROSTAM AZIZ, EDWARD LOWASA KWA UCHACHE KUWATAJA, ILI WATEME SUMU NI KUWA VUA UONGOZI WOTE WANAOSHIKILIA NDANI YA CHAMA NA MADARAKA WALIYO YAPATA KUTOKANA NA CHAMA km. UJUMBE WA HALAMASHAURI KUU, UBUNGE NA UENYEKITI NA UJUMBE WA KAMATI ZA BUNGE ILI WATANZANIA WASIENDELEE KUWAONA HAWA WATU WAKIWAKILISHA AU KUPEPEA BENDERA YA CHAMA POPOTE PALE
 
Hapo umsesma Kiloni, Makamba yawezekana ni hopeless lakini usisahau wameshughulikia mapaka sasa the 'official leadership' lakini siyo yenye shida, yenye shida ni defactor leadership - hiyo haijaguswa na huenda haitaguswa. Mara nyingi CCM wameshakaribia sana kuigusa ile 'point of pain' lakini ghafla kigugumizi huwapata na wakaamua kuingia mitini kila mtu na lwake.

Yetu Macho!

Now your taking.
 
sasa mwataka ****** ajivue nae gamba si maandiko yatatimia ya kuwa kimekosa dira na mwelekeo....saratani bado inakitafuna kujivua gamba bado hakujasaidia kitu wanahitaji x-ray ya nguvu la sivo 2015 watakiona cha moto.wasiwasi wangu MUkama ana skendo kibao,Nape ndio kabisa zero, Zakhia mhhhhhh hata uwaziri ulimshinda nashangaa hadi leo hajapanda Kisutu kwa tuhuma za ufisadi wa majengo pacha na EPA, KInana sidhani kama ana jipya.Ni sawa na kuweka kiraka kilichozeeka kwenye nguo iliozeeka...

Oooooooooooooooooooooooooh! kweli Mzee wangu aliniambia kuwa ukitaka siasa jiandae kuambiwa hata nguo ya ndani uliyovaa.Katika imani,tunaamini yakuwa hakuna mkamilifu ila ni Mwenyezi Mungu pekee.Iwapo manabii pia walipatwa na skendo nadhani haiwezi kukosekana kwa binadamu wa kawaida asiye na upako.Tuache majungu kwa wale ambao hawakuwahi kutajwa ama kunenwa mafisadi.Mkama naye ni binadamu kama wewe na tena wewe na ujana wako ukiingia jukwaani utakutwa na skendo kibao kama sio wizi,ubinafsi,uchochezi,ufuska na mengine mengi.Ebu tuwe wakati mwingine unprejudice for the reality.
 
kujivua kwa gamba kiukweli ni kuachana na mafisadi wote, kuwa vua nafasi zote walizo zipata zinazotokana na chama
 
Waiteme hiyo sumu vizuri wasijewakatupofusha macho tuu kwa sumu yao ilivyo kali
 
Mkuu mie sikubaliani na wewe yaani unamfananisha Nape na Sugu? tuzungumze ku ukweli Nape ni miongoni wa vijana wenye CV kubwa kiutawala na jina la Nape tumeanza kulisikia kabla ya hayo majina ya mengine labda jina la Sugu ndio la kitambo tena sio kwenye siasa ni kwenye bongo fleva....
kama kuwasemea wananchi basi sugu ameanza kufanya hivyo zamani.mashairi ya nyimbo zake yalidhihirisha hivyo.ni kweli Nape aweza kuwa na C.V nzuri kuliko sugu lakini ujiulize mbele ya mtanzania kijana wa manzese,unga Ltd na ilemela nani atauteka umati?hili ndio jambo muhimu ambalo ccm wanatakiwa kujiuliza,pia ccm wakumbuke kuwa kwa vijana shati la kijani=ufisadi.kwa maoni yangu sitta,magufuli na mwakyembe wanaweza kuvutia vijana kuliko Nape na wenzake.
 
Back
Top Bottom