Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Kwa upande wake, aliyekuwa Naibu Katibu Bara, George Mkuchika, alisema kuwa muundo wa chama kwa sasa utahakikisha kuwa wajumbe wote wanaoingia kwenye sekretarieti wasiwe wabunge wala mawaziri, ili waweze kufanyakazi za chama kwa ukamilifu.
“Safari hii hatutakuwa na kofia mbili. Awali wajumbe wengi walikuwa mawaziri na wabunge, hali ambayo ilisababisha shughuli za chama kusimama,” alisema. Hata hivyo, baadhi ya wanachama walikaririwa wakisema kama lengo la chama ni kutenganisha kofia ili kuleta ufanisi, utaratibu huo uwekwe hata kwa rais ili abaki na kofia moja ya urais.

hii itawezekana kweli? tungoje
 
kimsingi nakubaliana na hoja yako, lakini Chilligati na Mkuchika hakuna hata mmoja mwenye uwezo wa uongozi. wote hao ni nyoko kabisa.
 
Sijui kwa viatu hivi kama Nape vinaweza kumtosha ukiangalia upande wa pili wa shilingi kuna watu walioshika makali ya ufisadi hapo ndipo tunaona ugumu wa Nape kuweza kuhimili mikikimiki
 
Originally Posted by Mohammed Shossi Mkuu mie sikubaliani na wewe yaani unamfananisha Nape na Sugu? tuzungumze ku ukweli Nape ni miongoni wa vijana wenye CV kubwa kiutawala na jina la Nape tumeanza kulisikia kabla ya hayo majina ya mengine labda jina la Sugu ndio la kitambo tena sio kwenye siasa ni kwenye bongo fleva....


hivi Shoss inaelekea ww ni CCM Mbona huwa unawatetea sana ulivyokuwa CBE sikuona ukereketwa wako sasa imekuwaje?
 
wadau wa jf tuwe na utamaduni wa kupongezana pale mtu anapofanya jambo jema, nadhani jk anastahili pongezi kwangu ni mara ya kwanza kuona anatimiza ahadi zake anazozitoa, hivi karibuni mwezi februari alihaidi kuwa ccm itajivua gamba ili kurudisha taswira yake na mvuto kwa jamii na hili limetimia nadhani wansatahili bravoo

bravoo jk bravoooo,

bravo kwa ccm yenyewe kwa kukubali mabadiloko, daima wamekuwa watu wenye mawazo mgando na chama kushikiliwa na misimamo ya wachache lakini kwa sasa angalau wamekubaliana na kelele za magazeti na wananchi

bravoooooo ccm bravoooo
Una macho lakini bado hauoni bora hata yule ambaye ni kipofu
 
Nisaidieni wataalam wa KATIBA. Kamati Kuu ya CCM imejiuzuru. Mwenyekiti wake anabaki vipi? Katiba ya CCM inaruhusu haya?
 
Ndugu zangu uimara wa chama unategemea sana uongozi thabiti wa mwenyekiti wa chama.Hawa wote mliowalazimisha kujiuzulu walikuwa wanafanya hayo walioyafanya kwa baraka za mwenyekiti!...

Kumbukeni msemo wetu wa enzi zile "Zidumu fikra za mwenyekiti"...hii ilitokana na uongozi dhabiti wa Mwalimu Nyerere katika kukiongoza chama mpaka watu wakatamani fikra zake zidumu.John Chiligati ana upeo na uwezo mkubwa tu wa kiuongozi kuliko hata hawa mlioteuwa,..George Mkuchika vilevile na hata Makamba ambaye aliyokuwa anayafanya alijua mwenyekiti wake atayafurahia!...

Ninachosema hapa ni kwamba mlichokifanya mmetoa jasho na wala siyo gamba!..Gamba lenyewe ni mwenyekiti ambaye marafiki zake ambao ni manyangumi ya ufisadi yanakiyumbisha chama huku yeye akitabasamu.
Halafu wameishaota sugu kabisa kiasi kwamba zinatumika kila njia ili wasiguswe
 
Hata kama mkijivua magamba mara 10 kazi bure, nafikiri hamjui kama kansa inabaki kwenye damu,...! Huyo fake doctor wenu anawaogopa waliomuingiza madarakani wakina Rost....Az, Low...., kwanini asiwatoe hao na wengine, anamwonea Makamba, toeni ufisadi, kidooogo tutawaamini, lakini otherwise, kiini macho tu, HATUDANGANYIKI, maandamao hayo labda wahudhurie JK, Mkewe, Ridhiwan na wewe kibaraka wake unaeshadadia...... MAKAZAFA......!
 
Ndugu zangu uimara wa chama unategemea sana uongozi thabiti wa mwenyekiti wa chama.Hawa wote mliowalazimisha kujiuzulu walikuwa wanafanya hayo walioyafanya kwa baraka za mwenyekiti!...

Kumbukeni msemo wetu wa enzi zile "Zidumu fikra za mwenyekiti"...hii ilitokana na uongozi dhabiti wa Mwalimu Nyerere katika kukiongoza chama mpaka watu wakatamani fikra zake zidumu.John Chiligati ana upeo na uwezo mkubwa tu wa kiuongozi kuliko hata hawa mlioteuwa,..George Mkuchika vilevile na hata Makamba ambaye aliyokuwa anayafanya alijua mwenyekiti wake atayafurahia!... Ninachosema hapa ni kwamba mlichokifanya mmetoa jasho na wala siyo gamba!..Gamba lenyewe ni mwenyekiti ambaye marafiki zake ambao ni manyangumi ya ufisadi yanakiyumbisha chama huku yeye akitabasamu.


Mzanaki, Shida ni huyo wa kumfunga paka KENGERE. Tatizo kubwa la Tanzania ni kuwa watawala wetu hawatofautishi kati ya Chama na Serikali. Kwao yote ni sawa tu. Hapa ndipo tunapoanza kupata matatizo. Kiongozi wa Chama anaweza kulitolea uamuzi na maelezo jambo kubwa la kitaifa utadhani naye yupo serikalini kumbe ni TAWI TU LA VIJANA AU WANAWAKE! Tunachekesha dunia nzima!
 
tena gamba gumu mpaka limeweka na ukoko kabisa
 
Umejitahidi sana kumpigia debe kuhusu Mapokezi..Umeahidiwa Cheo? Ningemwona Kikwete ana Busara na ningeandamana Kumpongeza iwapo angeongoza kikao cha kUMVUA UANACHAMA Rostam Aziz na Edward Lowasa.
Lakina kwa Kujiuzulu kwa CC......Hakuna Cha Kupongeza kwani kwa taarifa za ndani ya Kikao KIKWETE alikuwa anataka Makamba na CC yake waendelee hadi Uchaguzi wa Mwakani..Sioni unataka Kumpongeza kwa Lipi Hapa!
 
Hivi tulimpaje mswahili kuongoza nchi? u have said it well mkuu, Chikwete ndo gamba lenyewe! fake smile, *****!
 
Mkuu umesema ukweli mtupu fitina kwako ni mwiko! Mimi nadhani ili CCM irudi kwenye mstari ni lazima wakubali watu kama waliochafuka (Wanajulikana) kuwaondoa kwenye nafasi nyeti za chama kama si kuwatimua kabisa kwanini wanaogopa, hii inaonyesha M/kiti ndiye anawakumbatia watu kama hao, tumemsikia Mkuchika akisema shida kubwa ya chama kutokubalika ni ufisadi na je nataka kujua inamaana wao waliokwisha kuachia madaraka ndio wanatuhumiwa kwa ufisadi? Kama sivyo hao mafisadi watatolewa lini kafara? Hii bila ya kificho inabidi wale wote wenye kashfa mbaya wawamwage kabisa na ndio hapo M/kiti ataonyesha ukomavu wa kisiasa. Jamani zama za kulinda sasa hazipo lkn kama kwa wanaccm hizo zama bado zipo basi wasubirie adhabu toka kwa wanachama wao.
 
Ukweli kulitakiwa kuwe na Kamati Kuu Tendaji ya Mpito ,Mwenyekiti wa CCM akiwa si mmoja wao lakini jinsi wanachama walivyo mazuzu na waoga,Jakaya atafanya anavyotaka,kubandua na kubanduka,kwa namna hiyo gamba halitavuliwa ila litasilibwa silibwa na kumeguka vipande vipande
 
Kwa upande wake, aliyekuwa Naibu Katibu Bara, George Mkuchika, alisema kuwa muundo wa chama kwa sasa utahakikisha kuwa wajumbe wote wanaoingia kwenye sekretarieti wasiwe wabunge wala mawaziri, ili waweze kufanyakazi za chama kwa ukamilifu.
"Safari hii hatutakuwa na kofia mbili. Awali wajumbe wengi walikuwa mawaziri na wabunge, hali ambayo ilisababisha shughuli za chama kusimama," alisema. Hata hivyo, baadhi ya wanachama walikaririwa wakisema kama lengo la chama ni kutenganisha kofia ili kuleta ufanisi, utaratibu huo uwekwe hata kwa rais ili abaki na kofia moja ya urais.

hii itawezekana kweli? tungoje

Na kama hivyo ndivyo, basi mama Sophia Simba aachane na uwenyekiti wa UWT, maana ni mbunge na waziri.
 
Umejitahidi sana kumpigia debe kuhusu Mapokezi..Umeahidiwa Cheo? Ningemwona Kikwete ana Busara na ningeandamana Kumpongeza iwapo angeongoza kikao cha kUMVUA UANACHAMA Rostam Aziz na Edward Lowasa.
Lakina kwa Kujiuzulu kwa CC......Hakuna Cha Kupongeza kwani kwa taarifa za ndani ya Kikao KIKWETE alikuwa anataka Makamba na CC yake waendelee hadi Uchaguzi wa Mwakani..Sioni unataka Kumpongeza kwa Lipi Hapa!

Sio kuwavua uanachama tu na kuwaburuta mahakamani kwa tuhuma walizonazo ili 'iwasafishe' pamoja na viongozi wote walioko serikalini wanaohusika na ubadhirifu kwa njia moja ama nyingine..
 
Back
Top Bottom