Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Mambo mazito CCM Dodoma: Wajivua gamba?

Wanajf

Baada ya kufanya kazi kubwa ya kukisafisha Chama sasa hivi kinaanza kumeremeta

Nakumbushia mkoa wa DAR es salaam kuandaa maandamano makubwa ya kumpokea na kumpongeza

Hata wanaJF wenye mapenzi mema na JK na MUkama kuwapa nguvu maana TANzania inazaliwa upya
Muwape pesa maana wenye fedha za EPA bado wapo!!!!!!!!!!!! SISIEMU kwa ghiliba hamjambo!!!!!!!!!!
 
Nadhani safari yetu bado ni ndefu, si dhani kama huko ni kujisafisha naogopa kwani inaweza kuwa ni kujipaka matope zaidi. Isipotumika busara ya wazee wetu wa asisi ambao nina mashaka kama mwenyekiti huwa anawasikiliza na kuelewa mambo yanaweza kurudi kule kule ikawa ni anguko jingine kwa CCM.
 
Hebu tuangalie mkuu....km ikiwezekana tuanzie maandamo hapa a-town to kivukoni......mbona ufisadi upo pale pale????????????? Tuende kwny maandamano au kwenye ngoma?
 
Wanajf

Baada ya kufanya kazi kubwa ya kukisafisha Chama sasa hivi kinaanza kumeremeta

Nakumbushia mkoa wa DAR es salaam kuandaa maandamano makubwa ya kumpokea na kumpongeza

Hata wanaJF wenye mapenzi mema na JK na MUkama kuwapa nguvu maana TANzania inazaliwa upya

Kwani nyoka akijivua gamba nakuwa kondoo? Nyoka ni nyoka tu, awe kijana au mzee, nyoka ni nyoka tu.
 
Sijaona cha kupongeza mtu hapo. Naye angejiuzulu uenyekiti na kuruhusu mchakato wa policy ndani ya chama kutoa ulazima wa rais kuwa m/kiti angestahili pongezi zangu. Hapo tunazugana tu. Nungunungu akimwagiwa maji hawi paka. Atabaki nungunungu tu.
 
TULIPO WAMBIA MAKAMBA MSEMA OVYO NA NI MWONGO MBONA MLIKATAA NA MKASEMA TUNADANGANYA. SASA MPAKA MAMBO YAMEKUWA SHINGONI NDO MNAGUNDUA. kWA NINI MSIFANYE MAANDAMANO YA KUPONGEZA VYAMA VYA UPINZANI? SABABU UPINZANI WALILIONA HILO KABLA YENU NYINYI. BIG UP UPINZANI
 
Jamani!! Pongezi kwa matunda gani yaliyoonekaana??? It is too early!!! Plse wait for the work first!!\
 
Yaa, Nape anafaa, he is good fighter! apewe nafasi aongoze.
 
Kwani cdm nani ana mvuto kuzidi nape?

wa sura au kisiasa? kama ni sura Nape hamzidi Mnyika au Lema. Kama kisiasa Nape Hamzidi Mnyika, hata yeye mwenyewe (Nape) analijua hilo.
 
Hii ni kiini macho,msitu wa zamani nyani wapya patakuwa na tofauti gani maana kazi za nyani sote tunazojua.Kwenye maandamno wataenda MAFISADI tu pamoja na watoto wa Jakaya,yaani mbampongeza raisi wakati Serikali yake na viongozi wake ni vinara wa kuiba fedha za walipa kodi masikini?Au mmesahau pana chenchi ya rada imeenda wapi?Richmond mpaka Dowans mmejua mwisho wake?Kagoda je ilishatolewa maamuzi!!?,Haya wale wezi wa EPA waliambiwa na raisi unaemshangilia kuwa anawajua hivyo warudishe taratibu!!!!hii inaingia akilini kweli!!?MABADILIKO YA UONGOZI NDANI YA CCM YANAFAIDA AU TIJA GANI KWA TAIFA!!??
 
Huyu Mukama ni kada wa CCM au yeye kuwa UwT mstaafu kutawasaidia CCM? Alikuwepo Mzee Gama hakuwasaidia kitu.
 
Kova tayari ameyapiga marufuku hayo maandamano baada ya kupata taarifa za kiintejisia kutoka kwa Mwema!!
 
Kwa mawazo yangu, muuaji mkubwa wa CCM ni mwenyekiti wake Jakaya Kikwete ambaye rafiki zake walio mafisadi wanafanya lolote wanalotaka.Kwanza wakisikia uteuzi huu watauliza....'Who is Mukama by the way?...Who is this young man Nape?...Huwezi kutenganisha perfomance ya Kikwete serikalini na kwenye chama!...Amefanya madudu kwenye uongozi wa serikali na amefanya madudu kwenye uongozi wa Chama.Kwa ufupi CCM haijajivua 'gamba' ila kilichotoka ni jasho tu!..Gamba la kweli litatoka pale Kikwete atakapoondoka....KIDUMU CHAMA CHA MAENDELEO!.
 
Hiki ndio kipimo kizuri cha kupima akili za Watanzania, kama maigizo wanayachukulia kama hali halisi au lah! Kwanza mimi binafsi mabadiliko yao ccm hayanihusu hizo ni taratibu zao walizojiwekea wao wenyewe, mimi nataka kuona hatima ya DOWANS, EPA, MEREMETA, N.K, hayo maigizo yao ya Dodoma mimi hayanihusu.
 
Cha kufurahia ni nafasi ya vijana katika siasa na kizazi hiki tufike wakati tusifungwe na itikadi za vyama bali tufungwe na malengo ya vijana kulikomboa taifa popote pale walipo pasipo kujali wewe ni wa chama gani.............Nape ni miongoni mwa wanaharakati safi katika vijana cha msingi nae asije akawa limbukeni wa sifa na vyeo anavyopatakwani vijana wengi ukiwapa cheo ndio unawamaliza kabisa
 
kundi la RA au EL plus Makamba?
hili ndio gamba gumu kuliondoa,halihitaji mwamba bali linataka kisu kikali cha kuliondoa,bila kuliondoa gamba hili sina uhakika kama ccm itarudisha mvuto!
 
Nyoka akivua gamba anakuwa nani? Anabaki nyoka au anakuwa kenge? CCM imejivua gamba, itabadilika? Mbona gamba lenyewe limeanzia shingoni kushuka miguu, kichwani kunani? Au ngozi ya kichwa haikuchuja mbele ya macho ya wanachama na jamii? Soma KISIMA CHA FIKRA huku ukijiuliza zaidi?
 
Mnaongelea mvuto wa sura au mvuto wa brain? Kama ni wa sura tanzishe shindano la kumtafuta.
Kapenga, katutoa kwenye dhumuni letu nasi tumemruhusu.

Haya maswala ya mvuto wa sura ndio yaliyotufikisha hapa tulipo. Badala ya kuangalia sura za kazi tunatafuta mvuto sijui ili tuufanyie nini.
 
Back
Top Bottom