Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Mama Rwakatare aichongea JamiiForums

Zipo nchi zinafunga mitandao kama hii au kuwekewa sheria kali kama ikitumika vibaya na washiriki kama china, korea kasikazini, saudi Arabia, Irani
Zote hizo ni nchi za kidictator wananchi hawana uhuru wa habari, unataka kuanzusha taifa la kidectator nini, watu wawe kimya wasitoe maoni yao????????

 
JF NA UKOSOAJI MCHUNGU ULIOTUKUKA: RAIS KIKWETE SASA APATA DIRA MPYA KUTUPUNGUZIA MZIGO WA SAFARI ZA NJE WALIPAKODI WA TANZANIA KUFUATIA MICHARAZO BILA HURUMA YA MTANDAO HUU

MhRais Kkikwete,

Nakushukuru sana katika hili la kusoma sehemu ya ukosoaji wetu hapa JF na hatimaye kuona mantiki ya kupunguza idadi ya watu unaosafiri nao kwenda nchi za nje.

Hadi hapa naomba naye mama yetu, Mchungaji Mama Lwakatare, aliyekaririwa majuzi kutamani kuona mtandao wetu huu wa JF ikifungwa atambue kwamba hata na sisi huku TUNAFAIDI KWA WATANZANIA tena kuliko hata uwakilishi wao bungeni huku sisi tukiwa hatulipwi mshahara na mtu yeyote wala hizo posho wanazozigombania hivi sasa huko mjengoni Domz.

Nasema mama yetu huyu naye sasa aone jinsi gani Rais Kikwete anavyotumia mtandao huu wa JF kurekebisha mambo hata kule ndani mwake Magogoni.

Ni majuzi tu hapa tumemtifua kweli kweli RaisKikwete juu ya safari zake nje ya nchi na tukahoji tupewe mchanganuo wa faida na tija tulizozipata kutokana na safari zake hizo tangu aingie madarakani ikilinganishwa na thamani ya gharama tulizozitumia kama walipa kodi kufadhili safari hizo.

Isitoshe, tulikwenda mbali kidogo kwa kutahadharisha ya kwamba walipakodi wa nchi hii tusije tukajikuta
tukifika mahali sawa na KUUZA ZIZI ZIMA LA NG'OMBE WETU WA PEKEE KUTUMIKA KUFADHILI SAFARI ZA RAIS NA JOPO LAKE KUBWA AMBALO MWISHO WA SIKU TUNAJIKUTA IKITULETEA FAIDA YENYE THAMANI YA YAI LA KUKU. This was a very candid and bitter criticism on President Kikwete BUT with a bottomline of AGGITATING FOR A CHANGE FOR THE BETTER.

Hadi hapa nimefarijika kugundua kwamba kumbe Mkulu hata ulivyo huko Davos kumbe bado uliweza kujipatia japo kijinafasi (kama mwana JF mwenzetu Prof Mwandosia alipokua matibabuni India) walau kuchungulia humu na kukutana na jinsi nilivyokukosoa kwa HASIRA ZOTE na wala haujachukulia chuki badala yake umeamua kuchukua hatua kurekebisha mambo.

Kimsingi Rais wetu, kama ulikua hujui, ujue leo kwamba hatufurahishwi hata chembe na uvujishaji wa kodi zetu bila kutuletea tija ya kuonekana. Madaktari wanatiji kubwa kwetu; kawaboreshee malipo yao, wabunge hasa wa CCM ni mzigo kwetu kwa tabia yao ya kugeuka muhuri wako kupitisha kila uchafu serikalini; kawapokonye posho zote, rekebisha mfumo wa mishahara na marupurupu kitaifa kuleta uwiano na kulinda morali ya watumishi wetu wa serikali

Jamii isiokua na kundi lenye kujenga mawazo tofauti yenye kukosoa kwa nia ya kujinga ni sawa na jamii iliokufa. Mimi ni mwananchi wako mkereka na mambo mengi ya hovyo pamoja na ufisadi serikalini na mkosoaji wako mwaminifui nisiyekuonea haya hata kidogo katia jambo lolote lile lenye kubeba MASLAHI MAPANA YA UMMA.

Hivyo, katika hatua yako hii ya kuwazia kutupunguzia mzigo wa safri za nje, nasema asante kwa kupokea ukosoaji wangu mchungu sana na kuligeuza kuwa ni sehemu ya ratiba yako kuturekebishia mambo.

Endelea kutarajia mashambulizi zaidi kwako na kwa serikali yako toka kwangu endapo kuna mahala mambo wala si mambo, na ninakutakia safari njema nyumbani uje ukamalize ubishi wa posho za wabunge kwa kuendana na matarajio ya umma na ukawalipe zaidi madaktari wetu.

Mwananchi Wako,



UWEZO TUNAO


katika magazeti ya leo kuna habari inayosema kikwete aagiza wanaoratibu misafara yake kwenda nje ya nchi kupunguzwa.
Mytake
1. Hivi ni kweli alikuwa ajui kuwa misafara yake ni mikubwa?
2. Kilio cha wananchi kimekuwa yeye kusafiri mara kwa mara nje ya nchi
3. Je kwa hilo agizo lake litakuwa mwarobaini kwa kilio cha wananchi?
 
Kwa nini kitakachofuata kiwe moto zaidi? Ina maana JF ni kwa ajili gani au wengine hatujui? Mimi ninanvyojua JF upo kwa ajili ya ku-interchange views, kutoa mawazo yenye tija kwa maendeleo ya taifa na mambo mengine kama hayo. So naamini uamuzi wowote wenye kutaka kufunga JF utakuwa umefanyiwa tafiti za kutosha na kujiridhisha kuwa mtandao huu hauna tija kwa maslahi ya taifa.

Wang'anyo nini tfsiri ya tija kwa tifa mana unajichanganya mwenyewe ati.
 
wakuu,
jf inapata promo bila malipo. Alianza mzee wetu msekwa, sasa waheshimiwa wanatumia milioni 64(za posho kwa siku) kuijadili! Duh
hii inapeleka ujumbe kuwa wanaisoma kwahiyo ni dhima yetu kuiboresha kwani sisi tuna uhakika sasa wanapata maoni yetu kiulaini.

Kinachomsumbua mama mchungaji pamoja na mambo mengine, ile habari iliyoeleza kuwa amemilikishwa kiwanda cha mang'ula, mama akaamua kuchukua mashine na kuzifanya vyuma chakavu.
Wapo waliohoji utaratibu uliotumika kumpa mmililki wa 'academy' uendeshaji wa kiwanda cha spea.
Hili linamsumbua mama wa kiroho maana yanawezaibuka yatakayo compromise integrity yake mbele ya wanakondoo.

Mpeni salaam ametukumbusha na soon atakuwa mada jf in fair and respected way but not in favor

tuongeze kasi kutafuta members wajiunge ili wanafiki waumie sanaaaaaaaaaaaaaaa
 
Kwa nini mama usibaki kanisani ona watu wanakutukana matusi mazito,kama sio wakil wa kristo..je muumin wako akipita hapa atajisikia,je?kwa kristo kuna kila kitu mwanadamu anachotaka...ningekushauri urudi kulea kundi la kristo
 
Huyu mama amekosa la kufanya.....JF tutazidi kufichua maovu wanayoyafanya... Hata wakiifunga japo huo uwezo hawana... Inawezekana kibonde haijui.. Jf cku akiijua hata tamani kuiacha..
 
Msameheni jamani, huyu hajui analosema amekurupuka, Suala sio mtandao wa JF ila kama kuna taarifa inayomuharibu ndiyo angeisema. Hii ianasikitisha sana kuona mchungaji kiongozi anakimbilia mjengoni wakati mlima wa moto unamuhitaji sana.
 
kweli ktk katiba mpya inabidi tufute ubunge wa viti maalum, Mbunge unaacha kujadili mgomo wa madaktari unapoteza muda kujadili nani mmiliki wa jf!! Baadae una sign unachukua 330,000 hata humuogopi Mungu?
Kwa nini wasijadili wizi wa wazi wazi wa rasilimalizetu dhahabu Tulawaka aliko fukuzwa MHESHIMIWA LEMBELI, Geta mine,Kahama mine, wote hawa kulipa kodi ni zero!!!! Halafu tunasema nchi yetu ni masikini, kumbe ni uzembe wa kufikiri tulionao hasa bungeni!!! Maovu mengi kibao kwa taifa hili, Mchungaji ameona JF kuwa ni kero amechokoza moto wacha aungue sasa!!!!!

 
Nadhani dunia inahitaji wawepo watu kama akina Lwakatare, watu kama akina Kibwetere. Kazi hubakia kwa wale wanaowaamini. Wajinga wapo ili werevu wawatumie, wawabebeshe mizigo na kuwafanya watumwa wao.
 
Si kwanza kuitaja JF na nadhani huko aliko hadi hapa atakuwa anajuuuuta kuishambulia JF. ANasahau kuwa hao anaowataka wafute nao ni wanachama wa JF...... Labda Pius Msekwa si mwanachama
 
Huyu mama mchungaji kama kayasema hayo basi kuna nyuzi zimemgusa humu. Hawa wana siasa wasiokubali kupokea "criticism" walikuwa hawafai kabisa kuwa wana siasa. Anafikiri JF ni kanisani kwake humu, kila atakalo sema watu watamchekelea tu.

Hawa ndio wale wanaoingia siasa kwa sifa na pesa zao na si kwa kuwa ni wana siasa. Mie alivyoingia nikajuwa anhaa sasa, tumepata msemaji ambae atakwenda mjengoni kufanya mambo, kumbe si lolote si chochote. Waondoe tu hivi viti vya kupeana.
Mkuu FF siku hizi you are so positive keep it up!!!!!!!!!!!!
 
hatimae nimejua id ya huyu mama. nimehangaika sana hadi nmeipata. juzi kadeletiwa jf ndo maana kalalamika. id yake ilikuwa dorisnelson.
 
Hakika hii ndiyo JF mlango wa ufahamu kiboko cha wezi na wanasiasa uchwara,na huyu mama yetu ambae kwa umri tayari anatosha kuitwa ni bibi kwa sasa,natumai alipitiwa na kama alitumwa waliomtuma walitaka kujua taarifa zake.Na kwa kuwa Mama huyu si mwelevu nae akalidaka na kulikumbatia kama mchango wke kwa kuliwakilisha kama mtumwa asiye na fikra na utashi binafsi.

Hakika waumini wote wa dini za kikristo sijui kwa dini ya kiislamu,kuna msemo unasema VYA MUNGU MPE MUNGU NA VYA KAISALI MPE KAISALI.Matamshi ya mama huyu ambae kwa umri wake anapaswa kuwa n huruma na Taifa hili siku zake za hapa duniani zitakapokwisha wajukuu wa mama Tanzania wa mkumbuke kwa kutoa mchango mzuri kwenye sekta ya elimu,na si kujuta kwa kusoma shule ambazo muasisi wake ameishi na kutoweka duniani akiwa ameacha jina baya na chafu ambalo limetokana na tuhuma ambazo zinatajwa humu ndani ya JF.

Natamani kusikia mama huyo akiomba msamaa kuwa alipitiwa na kuwa ya Mungu yataenda kwa Mungu na Kaisali nae atapewa yake.Vinginevyo kama anategemea JF kuwa itafungwa HASAHAU kwa kuwa Rais wake anajua umuhimu wa JF,na kuwa kama ni kufungwa JF basi ingefungwa wakati wa EPA na RICHMOND na Dada yake DOWANS.

Pamoja na kuwa Rais wake anajua maumivu ya JF,lakini kwa kiwango kikubwa anafaidika na ujumbe anaoupata toka jukwaa la Siasa ndani ya JF.Kwa Lugha nyepesi Rais wake anajua technlojia ya Internet sio kitu kinachoweza kugandamizwa kwa style ya mawazo ya wazee wa CCM wa miaka ya alobaini na saba bali ulimwengu mzima unajua kuwa ndio kitu bora na hatari ambacho raia wa kawaida anakimilki kama haki yake ya msingi ya kuwasiliana na jamii yake.

Hivyo kama mama yetu huyo anajipenda kweli kwa dhati kabla wanaJF awajamlipua kwa ushahidi wa wazi ambao utamnyima usingizi Rias ambae alimteua kuwa mwakilishi wake ndani ya Bunge basi awaombe radhi wanaJF.Kwa kuwa kwa tabia ya wanaJF wapatao elfu sitini na mbili [ 62,000] walivyo kila mmoja atakuwa yuko bussy kutafuta taarifa muhimu zinazomuhusu mama huyu, na bahati mbaya yeye ni Public figure na kuwa kama binadamu kuna mabaya na mazuri yake lakini kwa uchokozi alioanzisha na JF wataegamia kwa mabaya yake na ambayo kama moto wa gesi utalipuka mpaka kwa waumini wake na hatimae vyombo vya habari kutawanya yale yanayojili ndani ya JF na kwa kuwa ni yeye aliyenzisha basi itakuwa ni kanuni ya akuanzae mmalize.Na kwa vile alipeleka jambo hilo public tena bungeni ategemee yatakayojili pia yatakuwa wazi kwa umma yani public.

Bado nimapema sana anaweza kujitoa muhanga akajisajili humu JF na ID yake Original kisha akawaomba msamaa wana JF.na kwa kuwa mamia ya WanaJF humu ni Intellectuals watamwelewa na kuamua kumsamehe na kuwa anajuta kwa kosa hilo na atwapa ushirikiano katika ujenzi wa Taifa kwa faida ya wajukuu zake na Watot wa Tanzania waliopita kwenye mikono ya shule alizo anzisha yeye za ST Marys.

Kwa kuwa kesho na keshokutwa watoto waliosoma shule hizo za umilki wa mama huyo wasijione ni sehemu ya uovu utakaoibuka ulio nyuma ya pazia kama kweli upo.Kwa kuwa isiwe kila kijana akiulizwa umesoma wapi na akataja ST Marys [Mbagala au Mikocheni] kisha wanajamii wenzie waaanze kumbeza shule ya wavuta bangi na waluka ukuta na maneno mengine mbofumbofu hakika ni aibu kwa watoto na wazazi waliowasomesha kwenye shule hizo.

Ni vyema Mama huyo akaanza na NUSU SHARI KULIKO SHARI KAMILI ni mapema sana mama Rwakatale.ukichelewa wanaJF ni moto mzuri na hatari kuliko chochote asivyotegemea,ukiishi na watu intellectuals ufanane nao mawazo ukipishana nao jua utaumia.Asifanye tukajifunza tusiyoyajua kumhusu yeye kwa tiketi ya JF ambayo ni bustani ya wema kwa wapenda haki na ni jera na sindano kwa wasiotenda haki.
 
Huyu mama amekosa la kufanya.....JF tutazidi kufichua maovu wanayoyafanya... Hata wakiifunga japo huo uwezo hawana... Inawezekana kibonde haijui.. Jf cku akiijua hata tamani kuiacha..
kibonde+timu yote ya clouds fm/tv wanaijua saaana jf...!
 
Hv ile skendo ya Mama Rwakatare na Kakobe imeishia wapi? Najua na Mtikila alihusika kwa namna moja ama nyingine. Leo anaibuka na hoja ya JF...kazi ipo jamani. Na yeye naye mchungaji dah!!!. Kha Ptu..

Huko kote ni kukosa maneno ya kuongea na ili auze sura kwenye public na hv Tv zote zinarusha taarifa za bunge ndio basi tena.
 
Mama Mch Rwakatare kwa nini unapomualika muimbaji kanisani watu wakienda kumtuza hela zinachukuliwa na kupelekwa ndani? badala ya kumpa mwimbaji mwenyewe hela zake? hata kama mlishamlipa bado ile ni bahati yake unavyofanya si haki,kumbuka wewe ni Mchungaji.
 
Kila kunapokucha tunapata sababu za msingi za kufuta nafasi za ubunge wa viti maalum.

Wastage of resources kwa hawa watu wasiokuwa na msaada wowote kwa watanzania.

Pamoja na utapeli wote anaowafanyia watu masikini ukiongezea na posho za makalio lakini huyu mama hana kitu chochote cha kujivunia katika utumishi wake.

Lazima katika katiba mpya tuvifute hivi viti ili kupunguza mizigo bungeni na kuipunguzia nchi mzigo wa kupoteza fedha kuwalipa watu wasiokuwa na mchango wowote kwa maendeleo ya nchi.
 
JF Founder/team ilienda bungeni mwaka jana kama uzee haujafuta kumbukumbu zangu, huyo Mh Mchungaji Dr Mama Rwakatare siku hiyo hakuwepo bungeni?
Mbona unaproud sio Dr.huyo bali Dr. Wa uizi wa waumini wa wenzie kuna cku alimwandaa mumini wake kuwa eti msukule ili avute waumini wa wenzie.
 
Back
Top Bottom