Malori Mabovu kuegeshwa Barabarani, mamlaka Inawajibika kukagua Hivi Vyombo vya usafirishaji?

Makamura

JF-Expert Member
May 19, 2022
356
550
Barabara ya ubungo-Mbezi mwisho inaongoza kwa Kuegeshwa malori njiani, Malori yanasababisha foleni kubwa sanaa, Nashindwa kuelewa kuwa Mamlaka Huwa haifanyi ukaguzi wa magari haya?
malori.png

Yanaachwa yafanye safari zake yakiwa mabovu cha ajabu yanazima njiani, inakuwa kero kwa Watumiaji wa barabara wengine. Pia Wamiliki wa malori haya wanahatarisha maisha ya madereva wao na watumiaji wengine wa barabara. Unakuta Boss anajua gari mbovu na dereva kamwambia ila anamjibu "Si linatembea? Endelea kufanya kazi mpaka tutakapopata Mbadala"
 
Back
Top Bottom